Wababa wengine bwana

Mhhh kwanza kabisa kichwa cha habari yako na swali ulilouliza haliendani kabisaaaaaaa..........

1)Umeshasema kwamba hii messeg inaweza kuwa haina nia mbaya sasa kwa nini kichwa cha habari umekiandika kama amekutendea au kakupigia simu a kukuambia mabaya???Au labda kakutumia messeg ya mapenzi???

2)Umesema kwamba familia zenu zinaheshimiana sasa iweje uwe na shaka la kuwa anakutaka???Sasa hapo nadhani kichwa cha habari na swali lako umeona kwamba haviendani kabisa

Think first before you talk something.........Unajichanganya mwenyewe hapo maana usimuhisi mtu kwa kitu fulani wakati sio.........Mawazo yangu!!
 
ndio maana nikaja hapa, maana najiuliza nimjibu au nijikaushe tu, na je nikiamua kumjibu, nitamjibu nini? maana anaweza akasema yeye alikuwa ananisalimia tu.

Nadhani hapo hujajua nia yake nini na kashasema anasimu yako sasa muulize simu ya aina gani umeninunulia simu au unataka kunipigia simu????Usikilize atakujibu nini ndio ujuwe sasa hapo utamjibu vipi.....ila nadhani kwa sasa hivi hapa kwenye jamvi hutopata jibu la kuweza kukusaidia zaidi ya uwongo!!
 
 
...yawezekana pia ikawa ni mke wa jirani kwa simu ya mumewe, anakupima uaminifu wako, mjibu '...zis is wrong namba', au ...'ze namba iz not richabo' 😀.


Jibu lako zuri katika majibu yote niliyosoma maana wadau hapa wanajibu lakini hawafikilii mbali zaidi ila wanafikiria hapa hapa..........
 
asante kwa ushauri.
ivi, nikiamua kunyamaza itakuwaje? si anaweza kuelewa kuwa am not interested, au nyie mnaionaje hii. Je nimueleze mume wangu?

huyu baba ni mtu mzima kidogo, yani anapishana umri kidogo tu na baba yangu.


Utu uzima ndio ni sawa lakini sasa umueleze mme wako ili iweje???Haitasaidia kitu labda jamaa hana nia mbaya????Fikiria kwanza kama hujatenda
 
Wala sina time naye, naheshimu sna ndoa yangu, na pia nahemuheshimu sana mke wake. yeye pia nilimuheshimu sana, ila amejiaharibia



Mhhh MREMBO kwanza kakutongoza?????Au amekuambia kwamba anakupenda???Au kuna messeg mbaya yoyote kakutumia???
 
Mrembo, uchune kwanza na usubiri move yake ya pili upate uhakika. Baada ya hapo utajua mwenyewe


Jibu zuli sana maana asiende tu kwa pupa hajajua mzee wa watu anania gani au anawaza nini!!
 


Jibu zuli mkuu!!!
 
asante kwa ushauri.
ivi, nikiamua kunyamaza itakuwaje? si anaweza kuelewa kuwa am not interested, au nyie mnaionaje hii. Je nimueleze mume wangu?

huyu baba ni mtu mzima kidogo, yani anapishana umri kidogo tu na baba yangu.

Haa kumbe ni sawa na baba yako? Mpe heshima yake mjibu, haina shida innawezekana pia kuna jambo la faida kwako anataka kukuambia, ila akileta za kutongoza ndo hapooooo muelekeze haswaaa hadi aache hiyo tabia ta kutongoza watoto wake.
 
Familia zikiheshimiana ndio kinga ya kutotakwa kimepenzi?

nimeleta hii issue hapa kwa sababu imenichanganya. kwa mtazamo wangi nahisi anaweza kuwa ananitaka kimapenzi ila I am not sutre 100% ndio maana nikaomba ushauri.
 
kweli? mbona kuna majibu umesema ni mazuri?
 
Jibu zuli mkuu!!!
sasa Yassin mbona unanichanganya? mara unakubaliana kuwa nimueleze mume, mara nimueleze mume wa nini.

Sasa ushauri wako ni Upi?
 
We kwa kumuona katika mnavyo ishi..unamuonaje?...kwanza lazima uwe na personal obsarvation kwa mhusika ili uweze kuwa kwenye position nzuri ya kuelewa msg yake!!.

Ukimtizama machoni anakuwaje...anakuwa na sign?..je kuna wakati ulihisi anataka kukutogoza?Je tabia zake zikoje kwa watu wengine?anavyo ishi nao?anafahamika ni mtu wa wanawake japo kuwa ana familia yake(mhuni)?

Nafikiri kuna sign ya mizee ya hovyo katika jamii kama unaishi nayo utajua tu..so na wewe check the njoo na jibu...baada ya hapo naweza kuwa kwenye position nzuri ya kukushauli.
 
Pole Sana, I know you gotta brain - be smart enough to smash him . Take care
 
Familia zikiheshimiana ndio kinga ya kutotakwa kimepenzi?

nimeleta hii issue hapa kwa sababu imenichanganya. kwa mtazamo wangi nahisi anaweza kuwa ananitaka kimapenzi ila I am not sutre 100% ndio maana nikaomba ushauri.

Kwanini huwe na mawazo ya kutakiwa.....!!!? Try to be Positive sometimes.
 
Kwanini huwe na mawazo ya kutakiwa.....!!!? Try to be Positive sometimes.
we unafikiri kwanini anasema anasita kunipigia simu? na kama ni maswala mengine, sisi ni majirani na yupo free kunitembelea nyumbani kama ilivyo kawaida.
 
 
Wala sina time naye, naheshimu sna ndoa yangu, na pia nahemuheshimu sana mke wake. yeye pia nilimuheshimu sana, ila amejiaharibia


...kajiharibia nini? Labda anata kukuambia kuwa mmeo anatembea na mke wake! Watu wengi sana, hasa wabongo huwa wanapoteza bahati zao kwa kudhani kwanza badala ya kujaribu! We jibwage kivyotevyote tu. Najua final stage ya room ndiyo hutaingia kama kweli hutaki.
 
Jibu rahisi sana, just as

.... Mama Nanihii (mke wake) alishanipa hii namba muda mrefu, alisema angekuwa ananitafuta hata kwa namba hii yako muda mwingine.

Lakini kuwa makini, kila maamuzi unayofany, sms yoyote ya ajabu unayopata na unayoihisi vibaya ni vyema ukamwambia mume wako kungali mapema, kuliko kuficha halafu baadaye uje kuharibiwa.

keep loving your husband
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…