Mkwaruzo
JF-Expert Member
- Feb 21, 2011
- 563
- 98
Kutokana na kuwepo ongezeko la tatizo la unene, kampuni moja ya vinywaji ilijitolea kutengeneza kinywaji kitakachowezesha kupunguza unene wa mtu. Watu wengi duniani walinufaika na kinywaji hicho isipokuwa wenzetu wa mataifa ya kiarabu kwani wao walinenepa zaidi. Uchunguzi ulifanyika na kugundulika kuwa, wanaenda kinyume na uses iliyokuwa imewekwa kwa mchoro wa picha inayo onyesha utumiaji ni kuazia na kiwango kidogo na kumalizia kikubwa. Tatizo, wao waliusoma mchoro kutokea kulia kwenda kushoto.