Marumeso
JF-Expert Member
- Oct 3, 2009
- 1,410
- 1,313
kumekuwa na katabia ka waajiri walio wengi hasa wa mashirika/taasisi ya serikali kudai mwombaji aweke picha (mara nyingi picha moja au mbili) pindi wanapotangaza nafasi za kazi kwenye vyombo ivyo. mi nashindwa kuelewa hizo picha ni za nini hasa ukizingatia kuwa waombaji walio wengi huchujwa na kuachwa ktk hatua za awali tu. Hi sio ni kuchezea hela za watu tu?
Kumtaka mtu alete picha ni kumnyima haki mwombaji kwa sababu ya gharama ya pesa na muda wa upatikanaji wa picha hasa ukizingatia wanataka pia umwone mwanasheria wa kuhakiki vyeti.
Labda mnisaidie wadau hizo ndo sheria za uajili au ni utaratibu tu ambao mtu anaamka nao. Mtazamo wangu hii sio haki kabisa hasa kwa mtu aliye mtaani na anatafuta kazi.
Kumtaka mtu alete picha ni kumnyima haki mwombaji kwa sababu ya gharama ya pesa na muda wa upatikanaji wa picha hasa ukizingatia wanataka pia umwone mwanasheria wa kuhakiki vyeti.
Labda mnisaidie wadau hizo ndo sheria za uajili au ni utaratibu tu ambao mtu anaamka nao. Mtazamo wangu hii sio haki kabisa hasa kwa mtu aliye mtaani na anatafuta kazi.