benteke
JF-Expert Member
- Apr 3, 2014
- 1,305
- 1,069
Jumamosi nikasema Benteke wacha niache mkokoteni wangu ofisini niende kigamboni nikapumzike kidogo maana foleni zinachosha, huyooo mpaka posta, nikarukia UDA, lilikua limejaa ,niliingilia mlango wa nyuma nikashika bomba,... kaja mtu mwingine nyuma yangu na mbele kulikua kuna mdada.Uda limeanza mwendo naona mbona kama kuna ubnormal contact huku nyuma,nikasema labdahisia tu, kufika pale bunge nikasema hapana this is not normal, kwashida nikacheki kiupande, yalaaaa, busha. kumcheki jamaa usoni ni mtu mzima alafu ananitabasamia, sikufikiria mara mbili nikasema konda shuuushaaa, konda kajibu hamnakituo mpaka feri. Dada wa mbele naye kajibenua kiuno anazidi kunikandamizia kwa mzee wa busha, nikasema leo Benteke nimeliwa na hivi kikoi hakina zipu mbona nimeumbuka. Nikamnongoneza yule dada "dada lainika kidogo " dada akanijibu NINI? nikamnong'oneza"huyu mzee nyuma yangu ataniuaaa" dada naona hanielei, ikanidi nimteneknye kiuno akaruka, basi nikapumua. Nimefika fery nimeshuka mbio, si nikajikuta niko huku Utumishi badala ya kule pa kupakilia boti, nikasema wacha nirudi geto nikalale maana nimekoswakoswa kwenye UDA sio dalili nzuri kabisaaa.