Kwa sasa vyuo vilivyokuwa vinatoa advanced diploma (kiswahili chake kinanichanganya) sasa vinatoa digrii. Kwa kutaja vichache ni km vile Mipango Dom, IFM, CBE, DSA(TIA), n.k. Hofu yangu ni pale tutapoanza kuzibagua digrii hizi kwa vigezo vilivyotumika na Msemakweli. Hizi ni digrii za kweli? Mbona vyuo vyenyewe havijaitwa Universities? Tuelimishane