Vyombo vyetu vya habari vimenikera sana

Vyombo vyetu vya habari vimenikera sana

Megawatt B

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2011
Posts
259
Reaction score
69
Tangu jumamosi kule Zimbabwe na ukanda wa afrika ya kusini habari kubwa ilikuwa birthday ya Mugabe na hasa wito wake wa kumuhenzi Nyerere. Lakini vyombo vyetu vya habari haikuipa uzito habari hii kama ilivyostaili. Ukiangalia vichwa vya habari magazeti yote na TV tangu jumapili na hadi leo ni posho, posho, posho, posho tu za wabunge wale kule Dodoma. Nilitarajia vyombo vyetu kuipa habari hii uzito unaostahili, badala yake, ukisoma magazeti haraka haraka unaweza usione habari hii wasababu imewekwa kama kahabari kasiko na uzito wowote. Kweli nabii akubaliki kwao!

Hongea JF maana mliitupia habari hii na kachangiwa vilivo.
 
Vyombo vya habari vipo kabatini kwa lowassa na membe
 
Vyombo vya habari vipo kabatini kwa lowassa na membe


Ni kweli, kama vyombo vya habari vingeandika repeatedly juu ya speech ya Mgabe kumuenzi Mwl. Nyerere, huenda hata hao wanaposho Family wangekumbuka uadilifu wa Mwl. Nyerere na kuacha kuweka masilahi binafsi mbele
 
Waishupalie birthday ya Mugabe kwani yeye Mugabe alishawahi kuwapa bahasha kina Manyerere Jackton/
 
Last edited by a moderator:
waandish wa kibongo ni wachumia tumbo,wengi wao wanaandika si kwa wito,na ukifika uchaguz utawakuta kwa wagombea wakipokea hongo,achen kusoma magazet ya kibongo kama mimi
 
utafiti wa kisayansi umeonyesha kuwa 42% ya watanzania waliwahi kupata utapiamlo utotoni, na hata hao ambao wazazi wao walikuwa wana uwezo bado kuna wengine hawakupata malezi mazuri yenye maadili kwa maana ya kwamba wavuta bangi, madawa ya kulevya n.k., hivyo 50% ya watanzania hawana uwezo wa kufikiri vizuri, kwa lugha rahisi ni kwamba mkikaa mahari kujadili jambo au kufanya shughuli fulani basi ujue nusu ya hao hawana uwezo wa kufikiri vizuri na hiyo ni mpaka kwa viongozi wetu, na ndiyo maana unaweza kuona au kusikia kiongozi anatoa tamko ambalo watu wanabaki wanashangaa tu. leo hii akitokea mtu akaonyesha miujiza 2 au 3 atatangazwa huyo na mambo yote ya msingi yataachwa ikiwemo bunge la katiba.
 
Back
Top Bottom