LOTH HEMA
JF-Expert Member
- Dec 6, 2015
- 28,532
- 44,760
Vyakula hupikwa ili viliwe, sio kula tu kwa kuwa una njaa na unataka ule. Kula ni kula tu sio kujaza tumbo ili ushibe. Kuna vyakula vyenye hadhi na heshima huandiliwa maalumu kwa watu maalum wanaostahili heshima. Mathalani, viongozi wakubwa, watu wenye hadhi na heshima katika jamii, nyumbani kunakuwa na chakula maalum kwa wageni na wenye hadhi katika familia. Wengine wote wataishia kula chakula kisicho na ubora wala hadhi mradi tu wajaze matumbo yao na waone wameshiba. Hebu shusheni orodha ya vyakula vyenye hadhi na heshima kwa watu maalumu wenye heshima na hadhi zao katika jamii, familia na kaya