Watawala wanazidi kuishusha hadhi JWTZ

Watawala wanazidi kuishusha hadhi JWTZ

Kiranja wa jamii

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2023
Posts
1,132
Reaction score
2,675
Katika miaka ya hivi karibuni watawala wa nchi hii wamezidi kushusha hadhi ya jeshi letu pendwa lililojijengea heshima kubwa kwa miaka mingi

Kwa miaka niliyonayo nimekua na kuona namna JWTZ wanavyoheshimika mtaani na raia wa kawaida, jinsi wenye mamlaka ya kisiasa walivyokuwa wamejitenga mbali na makamanda hawa waliojenga heshima ndani na nje ya mipaka ya nchi yetu

Ilikuwa nadra sana kuwaona wakilandalanda mitaani bila shughuli maalum

Ilikuwa nadra sana kuwaona kwenye vyombo vya habari isipokuwa kwenye shughuli maalumu za kitaifa

Ilikuwa vigumu kuona wanafanya "press" na waandishi wa habari

JWTZ ilizingatia misingi na nidhamu ya kulilinda Taifa bila kulazimika kuja hadharani kupiga watu "mikwara". Hii ni kwasababu walichokifanya walikifanya baada ya kujiridhisha kinatakiwa kufanywa na kikifanyika kinaleta heshima kwa nchi

Miaka yote katika maswala ya ulinzi na usalama wa nchi hawa watu ndio walikuwa tegemeo la mwisho kuleta heshima hiyo

Hata hivyo, siku hizi imekuwa tofauti sana

Wanasiasa wamewaleta hadharani sana kiasi kwamba wao wenyewe wanaanza kujiona wakawaida sana

Hali hii ikishazoeleka na raia nao watawaona wa kawaida sana na hapo ndipo shida itakapoanzia

Raia hawatawaheshimu na wao hawatakubali kutoheshimiwa. Wale wachache watakaokataa dharau wataweka magwanda yao chini na kufanya wanalolijua wao

Naiona hatari kubwa sana huko mbele watakaokuwepo watakuwa mashuhuda

Hatari ya kuchoka kukaa maporini badala ya kukaa kwenye ofisi za kifahari;

Hatari ya kuvaa magwanda muda wote badala ya kunyonga suti na tai;

Hatari ya kukataa kutembea msituni wakila biscuit na maji badala ya kula kwenye hoteli za nyota tano bila kutoka jasho jingi;

Hatari ya kutaka heshima badala ya wao kuendelea kuheshimu na kupiga saluti muda wote,

Htari ya kutaka umaarufu na kutajwa tajwa sana kwa kusifiwa kama ilivyo kwa wengine

Hizi hatari na nyinginezo ni sehemu ya ajali itakayokuwa imesababishwa na wanasiasa waliowalazimisha JWTZ kuja hadharani kuona wao wanavyoifilisi nchi bila huruma na bila kutoka jasho badala ya kuwaacha huko huko mafichoni wakiilinda nchi kwa siri

Katika ulimwengu huu ni nani asiyependa heshima? Ni nani asiyependa mali? Ni nani asiyependa kula vinono? Ni nani anayatamani kuona hawaachi watoto wake katika hali nzuri? Ni nani asiyependa maisha ya kifahari?

Hawa watu wamefundishwa uzalendo, kufa kwa wajili ya nchi, kufa wakitetea maslahi ya nchi yao, kufa wakilinda mali za nchi dhidi ya wageni.

Wanasiasa mmeamua kuwaleta waone mnavyoitafuna nchi hii.

Mmewaleta hadharani washuhudie namna mnavyokula pasipokutoka jasho. Namna mnavyoteketeza rasilimali za nchi kwa manufaa yenu na vizazi vyenu

Hivi mnauhakika wao hawayatamani hayo maisha yenu? Mnauhakika wao hawazitamani hizo mali mnazomiliki? Mnauhakika wao watakubali kuendelea kuwalindeni tu kila siku huku wakiona namna mnavyozidi kujilimbikizia mali kwa kuuza nchi?

Kwamba wao ni maroboti hawaoni yanayoendelea? Kwamba wao kwenye mtaala wa mafunzo yao walifundishwa kumiliki mali ni dhambi na wote wakaelewa?

Chondechonde wanasiasa, waacheni hawa watu wabaki na kazi yao ya msingi. Wabaki na viapo vyao, watumikie mafunzo yao. Msiwalazimishe kufanya kitu ambacho hakikuwa sehemu ya mtaala wao itakuja kuleta taharuki kubwa sana
 
downloadfile.jpg
 
Katika miaka ya hivi karibuni watawala wa nchi hii wamezidi kushusha hadhi ya jeshi letu pendwa lililojijengea heshima kubwa kwa miaka mingi

Kwa miaka niliyonayo nimekua na kuona namna JWTZ wanavyoheshimika mtaani na raia wa kawaida, jinsi wenye mamlaka ya kisiasa walivyokuwa wamejitenga mbali na makamanda hawa waliojenga heshima ndani na nje ya mipaka ya nchi yetu

Ilikuwa nadra sana kuwaona wakilandalanda mitaani bila shughuli maalum

Ilikuwa nadra sana kuwaona kwenye vyombo vya habari isipokuwa kwenye shughuli maalumu za kitaifa

Ilikuwa vigumu kuona wanafanya "press" na waandishi wa habari

JWTZ ilizingatia misingi na nidhamu ya kulilinda Taifa bila kulazimika kuja hadharani kupiga watu "mikwara". Hii ni kwasababu walichokifanya walikifanya baada ya kujiridhisha kinatakiwa kufanywa na kikifanyika kinaleta heshima kwa nchi

Miaka yote katika maswala ya ulinzi na usalama wa nchi hawa watu ndio walikuwa tegemeo la mwisho kuleta heshima hiyo

Hata hivyo, siku hizi imekuwa tofauti sana

Wanasiasa wamewaleta hadharani sana kiasi kwamba wao wenyewe wanaanza kujiona wakawaida sana

Hali hii ikishazoeleka na raia nao watawaona wa kawaida sana na hapo ndipo shida itakapoanzia

Raia hawatawaheshimu na wao hawatakubali kutoheshimiwa. Wale wachache watakaokataa dharau wataweka magwanda yao chini na kufanya wanalolijua wao

Naiona hatari kubwa sana huko mbele watakaokuwepo watakuwa mashuhuda

Hatari ya kuchoka kukaa maporini, hatari ya kutotaka kuvaa sare badala ya suti, hatari ya kutaka kula bila kutoka jasho jingi, hatari ya kutaka kuheshimiwa badala ya kuheshimu muda wote, hatari ya kutaka umaarufu na kutajwa tajwa sana kwa kusifiwa kama ilivyo kwa wengine

Hizi hatari na nyinginezo ni sehemu ya ajali itakayokuwa imesababishwa na wanasiasa waliowalazimisha JWTZ kuja hadharani badala ya kubaki mafichoni wakiilinda nchi kwa siri

Jeshi la polisi limekwisha potoka, tegemeo pekee lilikuwa hili JWTZ.

Chondechonde wanasiasa, waacheni hawa watu wabaki na kazi yao ya msingi. Wabaki na viapo vyao, watumikie mafunzo yao. Msiwalazimishe kufanya kitu ambacho hakikuwa sehemu ya mtaala wao itakuja kuleta taharuki kubwa sana
Ndo maana walipigishwa kwata na M23
 
Katika miaka ya hivi karibuni watawala wa nchi hii wamezidi kushusha hadhi ya jeshi letu pendwa lililojijengea heshima kubwa kwa miaka mingi

Kwa miaka niliyonayo nimekua na kuona namna JWTZ wanavyoheshimika mtaani na raia wa kawaida, jinsi wenye mamlaka ya kisiasa walivyokuwa wamejitenga mbali na makamanda hawa waliojenga heshima ndani na nje ya mipaka ya nchi yetu

Ilikuwa nadra sana kuwaona wakilandalanda mitaani bila shughuli maalum

Ilikuwa nadra sana kuwaona kwenye vyombo vya habari isipokuwa kwenye shughuli maalumu za kitaifa

Ilikuwa vigumu kuona wanafanya "press" na waandishi wa habari

JWTZ ilizingatia misingi na nidhamu ya kulilinda Taifa bila kulazimika kuja hadharani kupiga watu "mikwara". Hii ni kwasababu walichokifanya walikifanya baada ya kujiridhisha kinatakiwa kufanywa na kikifanyika kinaleta heshima kwa nchi

Miaka yote katika maswala ya ulinzi na usalama wa nchi hawa watu ndio walikuwa tegemeo la mwisho kuleta heshima hiyo

Hata hivyo, siku hizi imekuwa tofauti sana

Wanasiasa wamewaleta hadharani sana kiasi kwamba wao wenyewe wanaanza kujiona wakawaida sana

Hali hii ikishazoeleka na raia nao watawaona wa kawaida sana na hapo ndipo shida itakapoanzia

Raia hawatawaheshimu na wao hawatakubali kutoheshimiwa. Wale wachache watakaokataa dharau wataweka magwanda yao chini na kufanya wanalolijua wao

Naiona hatari kubwa sana huko mbele watakaokuwepo watakuwa mashuhuda

Hatari ya kuchoka kukaa maporini badala ya kukaa kwenye ofisi za kifahari;

Hatari ya kuvaa magwanda muda wote badala ya kunyonga suti na tai;

Hatari ya kukataa kutembea msituni wakila biscuit na maji badala ya kula kwenye hoteli za nyota tano bila kutoka jasho jingi;

Hatari ya kutaka heshima badala ya wao kuendelea kuheshimu na kupiga saluti muda wote,

Htari ya kutaka umaarufu na kutajwa tajwa sana kwa kusifiwa kama ilivyo kwa wengine

Hizi hatari na nyinginezo ni sehemu ya ajali itakayokuwa imesababishwa na wanasiasa waliowalazimisha JWTZ kuja hadharani kuona wao wanavyoifilisi nchi bila huruma na bila kutoka jasho badala ya kuwaacha huko huko mafichoni wakiilinda nchi kwa siri

Katika ulimwengu huu ni nani asiyependa heshima? Ni nani asiyependa mali? Ni nani asiyependa kula vinono? Ni nani anayatamani kuona hawaachi watoto wake katika hali nzuri? Ni nani asiyependa maisha ya kifahari?

Hawa watu wamefundishwa uzalendo, kufa kwa wajili ya nchi, kufa wakitetea maslahi ya nchi yao, kufa wakilinda mali za nchi dhidi ya wageni.

Wanasiasa mmeamua kuwaleta waone mnavyoitafuna nchi hii.

Mmewaleta hadharani washuhudie namna mnavyokula pasipokutoka jasho. Namna mnavyoteketeza rasilimali za nchi kwa manufaa yenu na vizazi vyenu

Hivi mnauhakika wao hawayatamani hayo maisha yenu? Mnauhakika wao hawazitamani hizo mali mnazomiliki? Mnauhakika wao watakubali kuendelea kuwalindeni tu kila siku huku wakiona namna mnavyozidi kujilimbikizia mali kwa kuuza nchi?

Kwamba wao ni maroboti hawaoni yanayoendelea? Kwamba wao kwenye mtaala wa mafunzo yao walifundishwa kumiliki mali ni dhambi na wote wakaelewa?

Chondechonde wanasiasa, waacheni hawa watu wabaki na kazi yao ya msingi. Wabaki na viapo vyao, watumikie mafunzo yao. Msiwalazimishe kufanya kitu ambacho hakikuwa sehemu ya mtaala wao itakuja kuleta taharuki kubwa sana
Sasa hv hatuna jeshi pale, kwanza, wana recruit failures wa, form 4,pili viongozi wa juu, ni machawa wa ccm, wanawaza kisiasa, na, kidini, litakuwa, kama, jeshi la DRC, ukiwaona hawa, wajeda siku hz, wapo kama vibaka, kupenda swaga za hovyo,ubabe wa kijinga, nidhamu hamna,
Niliwakuta, pale mwenge mbeya, wamejiachia tu kihasara hazard kama boda boda
 
Back
Top Bottom