Mimi nachofahamu HAKUNA CHAKULA CHA KUONGEZA HIZO NGUVU ZA KIUME
Kitu cha msingi ni kuangalia matendo yako mwenyewe. Mfano kama ni mtu wa kupiga MKONO sasa nguvu zisikimbie kweli wakati unajiharibu mwenyewe. Mkono ni hatari coz hata ule karanga kilo 1 kwa siku kazi bure. Mkono ni Ibilisi mbaya sana coz unakua unauabudu. Kwa wakati unaotaka wenyewe lazima Uobey hata kama uko taiti vipi.
Pili nguvu zinakimbia kwa sababu ya kula ovyo vyakula na kupitiliza viwango. Mfano kipimo cha kula mafuta(fat) kwa mwanaume ni 95g kwa siku ,lakini unakuta watu wanakula 120g kwa siku au zaidi. Sasa haya mafuta yanaenda kulundikana kwenye tumbo,mapaja,kifua n.k. Huu ndiyo mwanzo wa kuzorotesha misuli yote muhimu inayoshirikiana na viungo vya uzazi. Mfano mwanaume usipokuwa na nguvu za miguu itakuwia vigumu sana kukamilisha shughuli hasa mzunguko wa pili na tatu. Hapa watu wanasingizia kuchoka,wakati ukweli upo wazi nguvu za miguu hakuna.
Mazoezi muhimu.Fanya mazoezi kuimarisha misuli yako hiyo hasa ya miguu na tumbo. Mazoezi yanasaidia kutoa sumu mwili hasa kwa njia ya jasho. Mwingine hujijui kwa kiasi gani mwili wako umebeba sumu ndiyo maana wataalam wakatengeneza masauna na stimu ruum kwa ajili ya kuondoa jasho. Inawezekana huna tatizo kabisa ila hiyo sumu mwili inakuzingua