Mr Mayunga
JF-Expert Member
- Jun 11, 2011
- 313
- 40
Ni ndani ya mji wa ikwiriri hapa rufiji,kuanzia jana alfajiri wakulima (wandekereko) wakilipiza kisasi kwa wakulima(wasukuma) kwa madai kua mkulima ameuwawa na msukuma.Chakusikitisha,wakulimu walijichukulia sheria mikononi kwaku haribu biasharara za wasukuma ,kuchoma nyumba 2 na nyingine zaidi ya 2 kuharibiwa vibaya.Mbaya zaidi mkuu wa mkoa wa pwani wakiambatana na mkuu wa wilaya walifika eneo la tukio mnamo sa 7 mchana wakitaka kuongea na wananchi, ila wananchi walisema 'hawataki kuongea na mwanamke'.Hii inatufundisha nini?Hali haikuishia hapo,wakulima waliendelea kuziba barabara huku mabomu yakiendelea kupigwa mpaka sa 12 jioni.Sasa je,viongozi wetu hawana mass influence kiasi hicho mpaka kusababisha shughuli yoyote yakiuchumi isiendelee zaidi ya masaa 9!?