Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Patashika ya Ligi Kuu Tanzania Vodacom Premier League VPL, kuendelea kutimua vumbi leo December 28, 2019 ambapo KMC FC Kino Boys, kukinukisha na Mabingwa wa Nchi, Simba SC, Mnyama Mkali Mwituni, kwenye dimba la Uwanja wa Uhuru.
KMC FC, ambao ndo wenyeji wa mchezo huo kwa upande wao wanaingia uwanjani wakiwa na maumivu ya kupoteza mchezo wao wa VPL uliopita baada ya kuchapwa na Polisi Tanzania kwa mabao 3-2 hivyo kwa mechi ya leo KMC FC imejipanga kuhakikisha wanarejesha hali ya furaha.
Akiingia kwa mara ya pili ndani ya kikosi cha Simba, akishinda mchezo wa FA, kwa kuichapa Arusha United 6-0 na kuirarua Lipuli FC 4-0 kwenye VPL, kocha mkuu Sven Vanderbroeck, ameweka wazi kabisa kuwa kikosi chake kipo tayari kusaka alama tatu muhimu huku akiongeza kwamba, anahitaji kuona timu yake inapata ushindi kwa idadi kubwa ya mabao katika kila mchezo utakaochezwa ili kuweza kutimiza malengo klabu.
Nani kuibuka na ushindi? Dakika 90 zitaamua, Kumbuka mechi ni kuanzia saa 10:00 Alasiri..Usikose Ukaambiwa
•••••••••=========••••••
Klabu ya Simba SC, imeibuka na ushindi wa mabao mawili kwa bila dhidi ya KMC FC kwenye dimba la uhuru.
Ikicheza kandanda safi la kuvutia na pasi za hapa na pale, Simba walianza kuhesabu bao la kwanza dakika ya 46 lililofungwa na Deo Kanda
Wakati mechi ikikisiwa kuwa itakuwa 1-0, Greson Fraga alipigilia msumari wa mwisho kwa kuongeza bao la pili kunako sekunde za jioni kabisa 90+3..
Kwa matokeo hayo Simba SC imeendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa VPL kwa alama 31 kwa michezo 12
FT: KMC FC 0-2 Simba SC
KMC FC, ambao ndo wenyeji wa mchezo huo kwa upande wao wanaingia uwanjani wakiwa na maumivu ya kupoteza mchezo wao wa VPL uliopita baada ya kuchapwa na Polisi Tanzania kwa mabao 3-2 hivyo kwa mechi ya leo KMC FC imejipanga kuhakikisha wanarejesha hali ya furaha.
Akiingia kwa mara ya pili ndani ya kikosi cha Simba, akishinda mchezo wa FA, kwa kuichapa Arusha United 6-0 na kuirarua Lipuli FC 4-0 kwenye VPL, kocha mkuu Sven Vanderbroeck, ameweka wazi kabisa kuwa kikosi chake kipo tayari kusaka alama tatu muhimu huku akiongeza kwamba, anahitaji kuona timu yake inapata ushindi kwa idadi kubwa ya mabao katika kila mchezo utakaochezwa ili kuweza kutimiza malengo klabu.
Nani kuibuka na ushindi? Dakika 90 zitaamua, Kumbuka mechi ni kuanzia saa 10:00 Alasiri..Usikose Ukaambiwa
•••••••••=========••••••
Klabu ya Simba SC, imeibuka na ushindi wa mabao mawili kwa bila dhidi ya KMC FC kwenye dimba la uhuru.
Ikicheza kandanda safi la kuvutia na pasi za hapa na pale, Simba walianza kuhesabu bao la kwanza dakika ya 46 lililofungwa na Deo Kanda
Wakati mechi ikikisiwa kuwa itakuwa 1-0, Greson Fraga alipigilia msumari wa mwisho kwa kuongeza bao la pili kunako sekunde za jioni kabisa 90+3..
Kwa matokeo hayo Simba SC imeendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa VPL kwa alama 31 kwa michezo 12
FT: KMC FC 0-2 Simba SC