Vodacom nitawachukia milele

Tigo sasa wamekuwa na speed internet...

Voda byebyee...
Acha nirudi zangu tigo aisee. Hawa Vodacom nimeshindwana nao rasmi. Tatizo wanaliona lakini linachukua zaidi ya masaa yote hayo. Hela yenyewe nina shida nayo vibaya mno
 
Vodacom Tanzania kama mpo humu naomba hizi habari ziwafikie. Mimi ni mteja wenu mkubwa sana. Tena mteja kindaki ndaki. Sina line ya mtandao mwingine wa simu zaidi ya line hii moja iliyonayo. Ndugu zangu wengi wapo mitandao mingine, najitahidi kumudu gharama kuwasiliana nao ili tu nisiachana na nyie.

Sasa nasema basi. Huduma yenu ya #songesha imenifanya niwachukie sana. Haiwezekani niwalipe deni lenu lote alafu mshindwe kunipa mkopo mwingine. Hilo nimelikubali na nikaamua kuachana na huo mkopo. Leo nimetumiwa hela kwaajili ya mahitaji muhimu, mmekata tena hela yote wakati sina deni na nyie.

Hakika hapa nilipo nimekasirika hakuna mfano. Maana nimewasiliana na watoa huduma wenu, wananiambia changamoto itatatuliwa ndani ya masaa 96. Hii sio haki. Hata kama ni utaratibu mliojiwekea, lakini hii haikubaliki. Hela tunazotumiana kwenye mitandao hii ya simu ni hela za mahitaji ya haraka. Leo mnaweza sababisha mtu akafatiki kwa kuikosa hiyo hela yangu ambayo ilitakiwa ikafanye mahitaji ya muhimu.

Japa nilipo mpaka naogopa kuomba hela sehemu nyingine maana inaweza ikatumwa halafu ikakatwa nikaendelea kusubilishwa masaa 96.

Tumia formula ya KILL ME BEFORE I KILL YOU wacha kulalamika wewe kila siku unawalipa kabla hujatumia Ila wewe ukitaka kutumia kabla hujalipa wanakutoza zaidi.

Fanya changamoto kuwa fursa Kama maandishi ulioandika n fursa huwezi kosa hata ka 20m kutoka kwao Kama ukiamua Sheria ifate mkondo wake Mana wewe mtumiaji ukimkosea ndo imekula kwako Ila wao wakikosea unataka kuwaomba samahani.

#NoRoomForExcuse
 
Tumia formula ya KILL ME BEFORE I KILL YOU wacha kulalamika wewe kila siku unawalipa kabla hujatumia Ila wewe ukitaka kutumia kabla hujalipa wanakutoza zaidi.

Fanya changamoto kuwa fursa Kama maandishi ulioandika n fursa huwezi kosa hata ka 20m kutoka kwao Kama ukiamua Sheria ifate mkondo wake Mana wewe mtumiaji ukimkosea ndo imekula kwako Ila wao wakikosea unataka kuwaomba samahani.

#NoRoomForExcuse
Hili nalo neno aisee. Maana hii ni kero sana. Wanafanya kazi kwa mazoea na kuchukulia kama kawaida tu linapotokea tatizo bila kujali athari upande wa mteja
 
Wanasema ni mtandao wa matajiri.....voda nawatumia zaidi kwenye M-PESA, kwenye internet halotel ni baba la mji, TTCL kwenye kupiga...
 
Kama kweli umeshawalipa nenda.kwenye maduka au ofisi zao ukiwashe
Utoe upuuzi hapa
Hawa watu sio wa kuwachekea tena
 
halotel mwendo wa konokono hamna kitu mule
Duh! sijui itakuwa tatizo la location ulipo au device unayotumia......mimi nikinunua kile cha 5000 GB 7 kwa wiki, yaani natiririka wiki nzima kwa kasi ya 4G na hadi wiki inaisha najikuta nimemaliza kama GB 4 tu....halotel ni baba la mji kwenye internet aisee..
 
Screenshot_20210719-121020_Messages.jpg
 
Vodacom Tanzania kama mpo humu naomba hizi habari ziwafikie. Mimi ni mteja wenu mkubwa sana. Tena mteja kindaki ndaki. Sina line ya mtandao mwingine wa simu zaidi ya line hii moja iliyonayo. Ndugu zangu wengi wapo mitandao mingine, najitahidi kumudu gharama kuwasiliana nao ili tu nisiachana na nyie.

Sasa nasema basi. Huduma yenu ya #songesha imenifanya niwachukie sana. Haiwezekani niwalipe deni lenu lote alafu mshindwe kunipa mkopo mwingine. Hilo nimelikubali na nikaamua kuachana na huo mkopo. Leo nimetumiwa hela kwaajili ya mahitaji muhimu, mmekata tena hela yote wakati sina deni na nyie.

Hakika hapa nilipo nimekasirika hakuna mfano. Maana nimewasiliana na watoa huduma wenu, wananiambia changamoto itatatuliwa ndani ya masaa 96. Hii sio haki. Hata kama ni utaratibu mliojiwekea, lakini hii haikubaliki. Hela tunazotumiana kwenye mitandao hii ya simu ni hela za mahitaji ya haraka. Leo mnaweza sababisha mtu akafatiki kwa kuikosa hiyo hela yangu ambayo ilitakiwa ikafanye mahitaji ya muhimu.

Japa nilipo mpaka naogopa kuomba hela sehemu nyingine maana inaweza ikatumwa halafu ikakatwa nikaendelea kusubilishwa masaa 96.
Mi nlishaachana na vodacom nna miaka sita sasa
 
Back
Top Bottom