Mimi ni wakala wa Mpesa.
Leo kuna mteja kaja kutoa pesa, kabla ya kutoa pesa salio lilikuwa ni 1,183,900.
Baada ya mteja kutoa 3500 salio likawa ni 1,183,000.
Hapo kuna pungufu ya 900+3500=4400.
Nimejarbu kuwapigia simu. Wamenijibu kuwa hawaoni tatizo lolote.
Acheni wizi. Nirudishieni pesa zangu.
====_==================
Inaonekana kuna watu Hesabu za kutoa na kujumlisha zinawasumbua sana.
Ok!
Ni hivi kabla mteja kutoa
pesa salio lilikuwa Milioni
moja mia themanini na tatu
elifu na mia tisa i.e
1,183,900.
Baada ya mteja kutoa pesa,
Salio likapungua na kuwa
Milioni moja na mia
themanini na tau elifu i.e
1,183,000.
Ingepaswa iwe hivi:
Baada ya mteja kutoa pesa
ingepaswa salio langu
liongezeke kwa kiasi
alichotoa i.e 3500
Salio jipya lingekuwa
1,183,900+3500=1,187,400.
Baada ya mteja kutoa pesa:
Baada ya mteja kutoa pesa
salio langu jipya likawa ni
1,183,000
Ikiwa na maana kuwa
wamekata 900 ktk salio la
mwanzo + 3500 aliyotoa
mteja
NB.
Nilipokea sms kuwa mteja
ametoa 3500.
Nadhani nimeeleweka.
Mteja wake ndiye aliyetoa hicho kiasi; ili muamala ukamilike unahusisha watu wawili, mwenye kibanda cha mpesa ambaye ndo huyu anayelalamika na mteja wake ambaye alitoa hicho kiasi, kama mtoa mada anasema ukweli kuna tatizo ambalo halijulikani; lakini kwa ufahamu wangu inawezekana kabisa mtoa mada kuna kiasi alichokuwa anadaiwa. hii hutokea mara nyingi sana unakuta mteja anatoa hela halafu anakosea namba ya wakala badala ya kuingiza namba ya wakala alipo anajikuta anaingiza namba ya wakala mwingine, sasa aliyekosea akilalamika lazima hicho kiasi kivutwe kutoka kwa wakala ambako kimeingia kwa makosa kurudishwa kwa mteja aliyekosea. nadhani inawezekana kimetokea kitu kama hicho kwa mdau lakini si kweli kwamba Vodacom wamwibie kwa jinsi hiyo, kama ni kweli afuatilie maana system zinaonyesha kila kitu ikiwezekana wamprintie aangalie tatizo liko wapi asione kwamba ni hela ndogo sio ujinga kuuza mbuzi kwa kesi ya kuku kama unachotafuta ni haki.
Kwenye nyekundu maana yangu ilikuwa ni kwamba kuna mteja mwingine some where ambaye nadhani alikosea badala ya kuingiza namba ya wakala ya alipokuwa yeye akaingiza namba ya mtoa mada kwa hiyo hela ilivyovutwa ikasababisha balaa kwa mtoa mada.
Kwenye nyekundu maana yangu ilikuwa ni kwamba kuna mteja mwingine some where ambaye nadhani alikosea badala ya kuingiza namba ya wakala ya alipokuwa yeye akaingiza namba ya mtoa mada kwa hiyo hela ilivyovutwa ikasababisha balaa kwa mtoa mada.
Muamala maana yake ni transaction, ni mchakato wa kutoa na kuweka hela na kwa maelezo ya mtoa mada transaction ilikamilika ndo maana hata yeye alipata message kwa hiyo muamala haukuwa na mashaka yoyote.
Wewe vipi? Huko some where huko, hata kama pesa ilikuja kwa mtoa mada kwa makosa kwa kawaida kiasi hicho huzuiliwa kwa saa zisizopungua 24. Haitumiki aidha kwa wakala ilipokosewa ama kwa mteja aliyekosea kwa kipindi chote mpaka kuwepo na mwafaka. Wote WATAPIGIWA simu ku indicate scenario hiyo na baada ya saa hizo 24 pesa itarudishwa kwa aliyekosea ilihali kwa huyu wakala zinakotoka akipewa message ya notification ikiwa na transaction ID number. Umenisoma jembe?
Habari,ninachoamini ni kuwa pesa haiwezi kupotea kwenye M-PESA,lazima kuna mahali salio litajulikana lilipo.Pia kabla hatujaanza kusema tumeibiwa tujaribu kwanza kupata suluhisho,Vodacom haiwezi kuiba salio na kama inafanya hivyo basi wateja wangeshaacha kutumia mtandao huo.
piga 15366, ingawa kuna makato, tena ukitumia line yako unayofanyia biashara ni rahisi zaidi kusaidiwa.Rogie
Hebu tueleze mahala pa kupatia ufumbuzi zaidi ya kupitia kitengo cha "Huduma kwa Wateja"???.
Hilo nimefanya.
Mzee,
Nisaidie tafadhali ingawa wewe ni wakala tu. Hivi nahitaji kutimiza vigezo gani lil nipewe uwakala. Natamani kufanya kazi hiyo na Vodacom.
Masuke
Nilifanya hivyo zaidi ya mara moja ila sikupata jibu sahihi.
mshahara wa 280000 wanaolipwa hao customer care bila benefit zozote unategemea watatoa huduma gani hapoYaani customer services ya voda wanatia kichefuchefu.Bora tu tuhamie ...! Juzi nilihamisha salio kwa mtu, ikaingia kwengine.Nikapiga voda kuomba msaada, hawakutaka hata kunisikiliza! Wakabakia na kamsemo chao '..aksante sana kwa kuchagua vodacom..'nadhani wanabweteka na customer base walionayo! Ole wao, ipo siku..
Una uhakika na hili mkuu?? Unaweza kusimama Mahakamani??