bathlomew
Senior Member
- Apr 3, 2012
- 124
- 28
Mimi ni wakala wa Mpesa.
Leo kuna mteja kaja kutoa pesa, kabla ya kutoa pesa salio lilikuwa ni 1,183,900.
Baada ya mteja kutoa 3500 salio likawa ni 1,183,000.
Hapo kuna pungufu ya 900+3500=4400.
Nimejarbu kuwapigia simu. Wamenijibu kuwa hawaoni tatizo lolote.
Acheni wizi. Nirudishieni pesa zangu.
====_==================
Inaonekana kuna watu Hesabu za kutoa na kujumlisha zinawasumbua sana.
Ok!
Ni hivi kabla mteja kutoa
pesa salio lilikuwa Milioni
moja mia themanini na tatu
elifu na mia tisa i.e
1,183,900.
Baada ya mteja kutoa pesa,
Salio likapungua na kuwa
Milioni moja na mia
themanini na tau elifu i.e
1,183,000.
Ingepaswa iwe hivi:
Baada ya mteja kutoa pesa
ingepaswa salio langu
liongezeke kwa kiasi
alichotoa i.e 3500
Salio jipya lingekuwa
1,183,900+3500=1,187,400.
Baada ya mteja kutoa pesa:
Baada ya mteja kutoa pesa
salio langu jipya likawa ni
1,183,000
Ikiwa na maana kuwa
wamekata 900 ktk salio la
mwanzo + 3500 aliyotoa
mteja
NB.
Nilipokea sms kuwa mteja
ametoa 3500.
Nadhani nimeeleweka.
Waambie wasome zaburi ya 49..