Vodacom kuanza kuuza hisa Machi 9

Mkuu mimi binafsi naona ni opportunity nzuri sana kuwekeza kwenye Telecoms. nilitumiwa prospectus yao nikaisoma ipo vizuri wanatengeneza profit baada ya kodi ni bil. 29. ingawa imeshuka kutoka bil 32 mwaka 2015 na bil 128 mwaka 2014. hii inatokana na competition kuwa kubwa lkn wanaongoza kwenye market share. na pia ukiongelea Vodacom unaongelea global kila mtu anaitolea macho. Dividend ni 50% profit itakayopatikana kwa mwaka. Najua wengi wetu ni speculators na tunategemea price appreciation ili kufaidika. Vodacom haitofilisika leo wala kesho na kama opportunity kama hii ikipatikana ya ku participate katika IPO sio ya kuacha wakuu.
Tena ukisoma vizuri hio tofaut ya faida ilisababishwa na hasara kwenye kampuni yake ya minara Helios Towers ambayo wameamua kuuza hisa zao na kuachana nayo,vinginevyo ni uwekezaji mzuri sana,tukizubaa tutakuja sikia baadae akina Manji ndio wana hisa za kutosha huko na kama kawaida yetu tutalalamika kana kwamba tulikatazwa kuwekeza wakati fursa tulipewa tukaipuuzia.
 
makampuni na taasis za serekali kama NSSF, PSPF Na mabenki ndio hununua hisa nyingi watanzania wa kawaida ni wachache
 
Sijui kuna nini
nimeenda Crdb wanasema Vodacom hisa hawajui lolote

nasikia ni bank moja tu NBC ndo watauza

sijaelewa kuna nini?

Halafu kumbe market share ya voda ni 31 tu asilimia?
na Tigo 29? tofauti ni asilimia 2 tu?

Voda si waliwahi kushika soko zaidi ya asilimia 50?

Naona kama hizi hisa zina longo longo hivi...

i think hujaelewa kuhusu matket share ilivyotumika. Hapa walimaanisha ile mobile subscribers wa vodacom katika watz wote ni 31% put of 100 then the 8 companies get their shares from the remaining 69%.
so inamaana watje wengi ni wa vodacom.
 
Sijui kuna nini
nimeenda Crdb wanasema Vodacom hisa hawajui lolote

nasikia ni bank moja tu NBC ndo watauza

sijaelewa kuna nini?

Halafu kumbe market share ya voda ni 31 tu asilimia?
na Tigo 29? tofauti ni asilimia 2 tu?

Voda si waliwahi kushika soko zaidi ya asilimia 50?

Naona kama hizi hisa zina longo longo hivi...
Vodacom hawajawahi kufikisha market share 50%
 
ila mimi bado nahsi ni ghali kidogo na sijui zinaeza kwenda mpaka wapi kwasasa
Hizi hisa hata sio ghali,angalia jedwali la bei ya hisa ya makampuni mbalimbalk
143a5093c7a091c70e0b906e89c5494f.jpg
 
Napendekeza wenye ufaham zaidi na waliochambua prospectus has financial statements watuelimishe zaidi kidogo.
 
Mkuu si ghali kama unavyofikiri. Swissport alianza kuuza kwa Tshs. 225 kwa hisa mwaka 2003 leo anauza kwa Tshs. 5,400.
Hivi unaruhusiwa kununua kwa installments?Mfano ununue kadhaa wiki hìi halafu ununue tena nyingine wiki ijayo?
 
Tena ukisoma vizuri hio tofaut ya faida ilisababishwa na hasara kwenye kampuni yake ya minara Helios Towers ambayo wameamua kuuza hisa zao na kuachana nayo,vinginevyo ni uwekezaji mzuri sana,tukizubaa tutakuja sikia baadae akina Manji ndio wana hisa za kutosha huko na kama kawaida yetu tutalalamika kana kwamba tulikatazwa kuwekeza wakati fursa tulipewa tukaipuuzia.
Ukiangalia kesi nyingi Vodacom,TRA na wengineo kama wafanyakazi kama wakishindwa ni zaidi ya billion 100. Faida ya 124bn 2014 na kushuka mpaka 32bn mwaka 2015 hapa na mashaka kidogo kama ni hiyo minara peke yake.
 
Hivi unaruhusiwa kununua kwa installments?Mfano ununue kadhaa wiki hìi halafu ununue tena nyingine wiki ijayo?
Yah inaruhusiwa kaka. Kiwango cha chini ni hisa 100 so unaweza kununua kidogo kidogo mpaka soko litakapofungwa tarehe 19 april.
 
Ukiangalia kesi nyingi Vodacom,TRA na wengineo kama wafanyakazi kama wakishindwa ni zaidi ya billion 100. Faida ya 124bn 2014 na kushuka mpaka 32bn mwaka 2015 hapa na mashaka kidogo kama ni hiyo minara peke yake.

Mhh...hilo nalo neno!@ Babu wa Loliondo na NIMITZ naomba mtufafanulie huku kushuka kwa faida sharp kiasi hiki.
 
Naombeni kufaham kwa hiyo ukiwa n hisa 100 ambayo ni kiwango cha cchini gawio huja kiasi gani?na je huwa hakhna magawio kwa kila mwezi?
 
Naombeni kufaham kwa hiyo ukiwa n hisa 100 ambayo ni kiwango cha cchini gawio huja kiasi gani?na je huwa hakhna magawio kwa kila mwezi?
Gawio sio kama mshahara utaupata kila mwezi,bali gawio hulipwa mwisho wa mwaka baada ya kampuni kujua faida kias gani imepatikana baada ya kulipa kodi,na kiwango chake hutegemea na ukubwa wa faida kwa huo mwaka husika.
 
Back
Top Bottom