Vodacom internet yenu mbona spidi mmepunguza sana?

Vodacom internet yenu mbona spidi mmepunguza sana?

real G

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2013
Posts
5,227
Reaction score
5,303
Hi, nimekuwa mtumiaji wa huu mtandao kwa muda mrefu sasa, sijabadilisha line, na kilichonifanya nisibadili ni kutokana na huduma zake za uhakika na mtandao ulioenea kote


sasa naona tatizo, japokuwa vifurushi vyenu mmevipunguza bei yaani mnatoa data (mb) nyingi kwa hela ndogo ila kasi ya mtandao imepungua sana,
7d8a64a6afe1bcdde909c0ed7e49789a.jpg


yaani hata kuanzisha huu uzi hapa jf umenichukua kujaribu jaribu kwa dakika kama 20 hivi
jaribuni kurudisha ile kasi iliyokuwepo zamani, hata kama mmeshusha bei ila msifanye hivyo kwa expense ya ubora
ni afadhali hata ikawa bei juu ila ikawa ya uhakika kuliko huu usumbufu ninaopata sasa hivi
fanyieni kazi plz!!
 
Tena wanakata internet kwanzia saa mbili asubuhi Hadi saa tisa..hata msg za whatsup hazitiki .
VODA MNABOA, BADILIKENI MNAZIDIWA HADI NA HALOTEL
 
54beff2e14c2527aaf7955c26d00c702.jpg
Tumia Halotel wewe check speed hiyo....
,simu ni ya line 1, line ina muda mrefu kuibadilisha nitapoteza vitu vingi sana na kusababisha usumbufu mkubwa kwa wengine
ila ikiwa too much nanunua simu nyingine kwa ajili ya line ya internet nzuri
 
Pole sana mkuu kwa uvumilivu wako na unapata shida kwa sababu ya mazoea. Kama umefikia sehemu umetambua tatizo ni kuchukua hatua.

Leo hii ulimwengu uko faster sana kimawasiliano na utoaji wa huduma ya data hvi Voda wameshindwa wapi kutoa huduma ya h+ na 4g kama halotel na tigo? Ni aibu kwa voda kampuni ya miaka tele ya uzoefu.
 
Ni wiki 3 toka Vodacom Internet na Calls waanze kuzingua, Me nitawatema muda si mrefu.
 
Bongo hatuna mobile Internet. Sijui hao smart maana sijatumia ila Voda na airtel walikuwa wanatia moyo lakini kwa sasa hamna kitu. Tigo mi nahesabu tu hawana kabisa Internet. Labda Halotel ipo kasi, ambao pia sidhani kama net yao itaendelea kuwa kasi maana kila siku inazidi kupunguza spidi na sometimes inakata temporarily.
 
,simu ni ya line 1, line ina muda mrefu kuibadilisha nitapoteza vitu vingi sana na kusababisha usumbufu mkubwa kwa wengine
ila ikiwa too much nanunua simu nyingine kwa ajili ya line ya internet nzuri
Tafuta kitochi mkuu.cha samsung ama nokia.then line ya mawasiliano inakuwa kwenye tochi kwenye smartphone unaweka line ya intanet.na watsap unatumia namba ileile tu ya zamani
 
Tafuta kitochi mkuu.cha samsung ama nokia.then line ya mawasiliano inakuwa kwenye tochi kwenye smartphone unaweka line ya intanet.na watsap unatumia namba ileile tu ya zamani
ok, hii voda ndio ipo WhatsApp nikiiweka kwenye tochi bado nitaweza kuitumia kwenye WhatsApp ikiwa kwenye tochi?
 
ok, hii voda ndio ipo WhatsApp nikiiweka kwenye tochi bado nitaweza kuitumia kwenye WhatsApp ikiwa kwenye tochi?
yeah we jaribu tu utaona.unaotoa unaweka mfano halotel then unaendelea kuchat kama kawaida.whatsapp huwa shida yao ni verification tu kuwa namba uliyoiweka ni yako na iko hewani.mi natumia namba ya marekani watsap na nipo zangu bongo
 
Voda na tigo kwa sasa ni majipu makubwa sana Network. Mtu hata kutuma sms kwa whatsApp inachukua muda kibao utadhani upo kule Ugalla Katavi.
 
Bongo hatuna mobile Internet. Sijui hao smart maana sijatumia ila Voda na airtel walikuwa wanatia moyo lakini kwa sasa hamna kitu. Tigo mi nahesabu tu hawana kabisa Internet. Labda Halotel ipo kasi, ambao pia sidhani kama net yao itaendelea kuwa kasi maana kila siku inazidi kupunguza spidi na sometimes inakata temporarily.
Ina maana Halotel kadiri wateja wanavyozidi kuongezeka na kasi yake inapungua?
 
Back
Top Bottom