Voda Mnaleta kinyaa kwa wateja wenu!!

Voda Mnaleta kinyaa kwa wateja wenu!!

Kabla ya Kuwashitaki TCRA,

Napenda kuwatangazia kuwa hii kampuni ya vodacom wanaleta usumbufu usio wa kawaida kabisa kwa wateja wake napenda kusema kuwa ni WIZI wa wazi kwa wateja wake!

Unaweka vocha ya sh 5000, ukitaka huduma unayotaka kama kupiga simu nk unaambiwa hauna salio la kutosha, ukiangalia salio limekuwa 0.00 DUH!! ukiwapigia wanaleta lingolongo ohh piga baada ya nusu saa, tatizo lako tumeliwasilisha kwenye kitengo maalum, ohh jaribu tena kutupigia kesho!

tunaandaa charge kwa ajili ya kuwashtaki TCRA, ndo mtajua kuwa TZ sio ile tena mliyozoea ya kuwaonea wateja, kila mtakapo!

this is all ----!!

sio tu hawa voda ovyo sana wanavujisha siri za wateja,wanashirikiana na ccm kuhujumu vyama vingine kma walivomfanyia lema na sms ya mulungo
 
Sasa nyie mnataka wakale wapi??
wabongo bwana!!
kila mbuzi anakula urefu wa kamba yake!
 
Voda na tigo kuna matatizo,mimi sasa hivi nipo na airtel.
 
siku zao zinahesabika eee wanaboa sana hawa jamaa!!!
 
nilikuwa na tg nikatupa, voda nao chaaa!!! sasa afadhali eatel aisee
 
dah nilifikiri mimi tu ndio ninakerekwa na huduma ya hawa watu. two weeks ago nilijiunga na supa cheka, baada ya kunitumia ujumbe wao wa kuungwanishwa katika dakika 10 wakanitumia ujumbe kuwa dakika zangu zimekwisha. kwa kuwa nilikuwa na issue mlimani city nikawapitia, piga folen isiyo na msamaha pale nikawaeleza, wakachukua details za simu, wakarudisha hela baada ya siku moja na nusu. wiki iliyopita nikapiga simu nikiwa na salio kama sh elfu moja na kitu hivi, kuongea kiasi simu ikaisha salio nikaongeza 3,000 kutoka m-pesa, nikamalizia kumpa msg niliyekuwa naongea nae it took less than 2 min tukakata simu 3,000 zote zimekombwa.
kesho yake asubuhi nikaingiza 3,000 tena halafu nikajiunga na supa cheka sh.400, nikapata msg ya kuunganishwa na baada ya muda mfupi ikafuata msg kuwa sekunde zimeisha, bila kuongea! nikawa bored na bado nawatafakari nifanyeje, wizi usio na kifani
 
Kabla ya Kuwashitaki TCRA,

Napenda kuwatangazia kuwa hii kampuni ya vodacom wanaleta usumbufu usio wa kawaida kabisa kwa wateja wake napenda kusema kuwa ni WIZI wa wazi kwa wateja wake!

Unaweka vocha ya sh 5000, ukitaka huduma unayotaka kama kupiga simu nk unaambiwa hauna salio la kutosha, ukiangalia salio limekuwa 0.00 DUH!! ukiwapigia wanaleta lingolongo ohh piga baada ya nusu saa, tatizo lako tumeliwasilisha kwenye kitengo maalum, ohh jaribu tena kutupigia kesho!

tunaandaa charge kwa ajili ya kuwashtaki TCRA, ndo mtajua kuwa TZ sio ile tena mliyozoea ya kuwaonea wateja, kila mtakapo!

this is all ----!!

Kijana pole sana, weka no yako hadharani wakuangalizie humu wako wengi!!!
 
Mie nimejisajili, ninesafiri nje ya nchi namba yangu wamempa mtu mwingine wamenibore sana
 
Mimi nishahamia Airtel, sasa hivi nanunua vocha ya mwezi sihangaiki kununua vocha wala internet. Voda huduma zao ghali sana. Nasubiri hata Airtel money ikae vizuri ili hela zangu niwe natumia airtel money voda nitaiacha kabisa. Tigo nimeshatupa kabisa line yake. Voda imebaki kwaajili ya Mpesa na kupokelea simu only.
 
Kinachonikera voda ni kwamba hawataki kuongea na wateja wao. Longo longo nyingi ukitaka kujua salio bonyeza 1, ukitaka kugegeda mke wa mtu bonyeza 2........................................................................... 100
Just talk to us
 
me wanachoniudhi ni tabia yao ya kutaka kunivurugia ndoa yangu, yaan msg zinachelewa kufika sio kwd na mke wangu ni mkorofi/wivu kupita maelezo na tuko mbalimbali kwa sasa. VODA, KAMA MMESHINDWA KAZI, ACHEN!
 
Back
Top Bottom