Vizuia moto maeneo ya Biashara

Vizuia moto maeneo ya Biashara

Masalu Jacob

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2017
Posts
1,339
Reaction score
1,493
Habari Tanzania !

Nawaomba sana watu wote wanaomiliki maeneo ya biashara, makazi na maeneo yenye mikusanyiko ya watu wengi; wawe wanaweka vifaa vya kukinga moto. Hii iwe ni utamaduni wetu tusipuuze na pia tukumbuke tuna sheria ya utunzaji mali hasa majengo na maeneo yenye bidhaa za milipuko.

Kuna vikinga moto vya aina nyingi;
1. Fire extinguisher (Zipo aina nyingi inategemea na bidhaa, mali unazomiliki)

2. Mchanga laini (Huu unaweza uweka kwenye ndoo ndogo, kubwa au zile ndoo za kuhifadhia maua ambazo watu huzipenda kama urembo majumbani nk ).

3. Blangeti nzito (Hii unapaswa kuwa nazo za kutosha itategemea na mali ulizonazo)

NB

Tuache kuwa wanajimu wa majanga ya moto; maana dunia inabadilika na hali ya hewa inazidi kuwa tofauti mara kwa mara sambamba na shughuli za kibinadamu.
 
Weka Bima ya MOTO maana kuna moto huwezi uzima
 
Weka Bima ya MOTO maana kuna moto huwezi uzima
Hmmm !
Sijawahi kuona Bima ya moto ikizima moto. Isipokuwa nafahamu ya kuwa Bima inafanyakazi ya fidia dhidi ya janga la moto.
 
Tutavichoma vyote hivyo hadi magari ya kuzima moto nayo huungua mpaka waondoke.
 
Tutavichoma vyote hivyo hadi magari ya kuzima moto nayo huungua mpaka waondoke.
Hata sehemu unapokaa jitahidi uweke hata ndoo ya mchanga au ununue fire extinguisher aina ya powder (Iwe upangaji au umejenga) ufanye hivyo.
Gharama zake ni rafiki na nafuu sana..
 
Hata sehemu unapokaa jitahidi uweke hata ndoo ya mchanga au ununue fire extinguisher aina ya powder (Iwe upangaji au umejenga) ufanye hivyo.
Gharama zake ni rafiki na nafuu sana..
Hatuhitaji kuzima moto, tumahitaji kuwasha moto.
 
Back
Top Bottom