Viwanda Pwani, ni sera ama ukanda hapa Tanzania?

Rweye

JF-Expert Member
Mar 16, 2011
17,052
7,609
Naelewa nchi yetu imejikita katika hii kauli mbiu ya viwanda. Halikuonekana wazi katika hawamu ya nne lakini sasa linaanza kutia shaka, hivi kujenga viwanda vyote eneo la ukanda wa pwani wa nchi yetu huku maeneo mengine ya nchi yakionekana kuachwa ni sahihi kweli? Na je hiki ni kitu gani hasa kinafanyika.

Inatia ugumu kuelewa adhima hii ni nini pale mfano unaposikia eti mkoa mmoja tu 'mkoa wa Pwani' mfano una viwanda zaidi ya 30 huku kukiwa na mikoa isiyokuwa na hata viwanda 5. Hii maana yake ni nini? Mkoa kama Tabora mfano hauna hata kiwanda1 na haionekani kama kuna hata wa kufikiri katika hili, ni kwanini mikoa mingine ifanywe kama vile si sehemu ya Tz.

Kutoka kanda ya magh, kusini mpaka kati ya Tz unaweza ukakuta viwanda vilivyo katika kanda hizo tatu ama ni vichache kuliko vilivyoko mkoa mmoja wa pwani kwa sasa hivi. Huu si ukanda mwingine huu? Wakati mwingine unajiuliza kama lengo la kwanza kuwa na viwanda ni kutoa ajira, utawezaje kupunguza hili tatizo kama viwanda vipya vyote vinaelekezwa mikoa ya pwani, Tanga, Pwani, Dar, Mtwara?

Ama ndo tunafanya zile zile sera za kikoloni, kupeleka vitu muhimu kwa maeneo fulani tu kwa sababu zao maalumu. Ama tunamaanisha watu wote wahame toka kanda zingine na mikoa mingine wazifate ajira pwani tu? Ni kwanini nchi hii kwa sasa hivi kila kitu kinaelekezwa huko tu? Utasikia magari, pikipiki, baiskeli, matrekta, vigae, mabati n.k kila kiwanda kinasemwa pwani tu. Is this fair kwa maeneo mengine ya nchi?

Najua wenye akili finyu wataona nimeleta kitu cha hovyo kwasababu sasa hivi wanataka za Makonda tu, lakini wengine tunajua ili nchi yetu iendelee Makonda si chochote sana, kesho Makonda hatokuwepo lakini Tz yetu itakuwepo na itabidi izidi kuwepo na isonge mbele.
 
Naelewa nchi yetu imejikita katika hii kauli mbiu ya viwanda. Halikuonekana wazi katika hawamu ya nne lakini sasa linaanza kutia shaka, hivi kujenga viwanda vyote eneo la ukanda wa pwani wa nchi yetu huku maeneo mengine ya nchi yakionekana kuachwa ni sahihi kweli? Na je hiki ni kitu gani hasa kinafanyika.

Inatia ugumu kuelewa adhima hii ni nini pale mfano unaposikia eti mkoa mmoja tu 'mkoa wa Pwani' mfano una viwanda zaidi ya 30 huku kukiwa na mikoa isiyokuwa na hata viwanda 5. Hii maana yake ni nini? Mkoa kama Tabora mfano hauna hata kiwanda1 na haionekani kama kuna hata wa kufikiri katika hili, ni kwanini mikoa mingine ifanywe kama vile si sehemu ya Tz.

Kutoka kanda ya magh, kusini mpaka kati ya Tz unaweza ukakuta viwanda vilivyo katika kanda hizo tatu ama ni vichache kuliko vilivyoko mkoa mmoja wa pwani kwa sasa hivi. Huu si ukanda mwingine huu? Wakati mwingine unajiuliza kama lengo la kwanza kuwa na viwanda ni kutoa ajira, utawezaje kupunguza hili tatizo kama viwanda vipya vyote vinaelekezwa mikoa ya pwani, Tanga, Pwani, Dar, Mtwara?

Ama ndo tunafanya zile zile sera za kikoloni, kupeleka vitu muhimu kwa maeneo fulani tu kwa sababu zao maalumu. Ama tunamaanisha watu wote wahame toka kanda zingine na mikoa mingine wazifate ajira pwani tu? Ni kwanini nchi hii kwa sasa hivi kila kitu kinaelekezwa huko tu? Utasikia magari, pikipiki, baiskeli, matrekta, vigae, mabati n.k kila kiwanda kinasemwa pwani tu. Is this fair kwa maeneo mengine ya nchi?

Najua wenye akili finyu wataona nimeleta kitu cha hovyo kwasababu sasa hivi wanataka za Makonda tu, lakini wengine tunajua ili nchi yetu iendelee Makonda si chochote sana, kesho Makonda hatokuwepo lakini Tz yetu itakuwepo na itabidi izidi kuwepo na isonge mbele.
Naunga hoja. Haiingii AKILINI kuona mkoa mmoja PWANI ndo kila kitu. Kwani mikoa mingine haiihitaji hivyo VIWANDA?

Ndo maana serikali ya devolved government INAHITAJIKA. Hii ndo njia pekee ITAKAYOONDOA kutokuwa na usawa katika MAENDELEO MIKOANI.
As long as KATIBA ndo hii. Vituko kama hivi HAVITAISHA.
Kama ni hivyo basi IWANDA vigawanywe- EVENLY/ katika USAWA.
 
kwani huko kuna bahari,kujenga kiwanda bara inategemea na raw material zilizopo sehemu usika,kujenga kiwanda cha tiles singida ni gharama,mali ghaf itoke china ifike dar iende singida then tiles zije tena dar ambako ndo kuna soko zaidi,huko bara jengeni kulingana na malighafi iliyopo mfano kiwanda cha juice cha bakhresa angejenga tanga ingekuwa powa zaidi
 
Kwa kielimu changu kidogo nilichonacho ninafahamu kuwa kuanzisha kiwanda unategemea vitu kama; upatikanaji wa malighafi (raw materials), miundombinu ya kuendesha kiwanda kama nishati, umbali wa kiwanda kutoka kwenye port of entry na vitu vingine. Hii access to the port of entry inaplya vital role, katika uletaji wa malighafi ambazo hazizalishwi localy.

Mwenye kiwanda pia kama atakua na biashara nyingi nyingine, angependa kukaa sehemu ambayo kwake ni rahisi kusafiri. Hii ni moja ya sababu zinazofanya mikoa ya Pwani kuwa na viwanda vingi kwasababu ya bandari na air port.
 
Kwa kielimu changu kidogo nilichonacho ninafahamu kuwa kuanzisha kiwanda unategemea vitu kama; upatikanaji wa malighafi (raw materials), miundombinu ya kuendesha kiwanda kama nishati, umbali wa kiwanda kutoka kwenye port of entry na vitu vingine. Hii access to the port of entry inaplya vital role, katika uletaji wa malighafi ambazo hazizalishwi localy.

Mwenye kiwanda pia kama atakua na biashara nyingi nyingine, angependa kukaa sehemu ambayo kwake ni rahisi kusafiri. Hii ni moja ya sababu zinazofanya mikoa ya Pwani kuwa na viwanda vingi kwasababu ya bandari na air port.
Kuna kitu unakizungumza kwa uzuri sana na kinaeleweka sana. Lakini hebu ngoja tuone, kweli ni ishu ya raw material? Kweli ni ishu ya miundombinu tu? Kweli ni ishu ya entry ama kuna kingine chini chini?

Hivi ni kwa kiasi gani serikali inaonekana kushiriki kuona inahakikisha viwanda vinasambaa mikoa mingine?
Kwa maana nyingine inamaanisha malighafi zilizoko mikoa mingine hazitakuja kupata viwanda kwasababu ni mbali na airport na harbour?
Mbona tulisikia Kigoma kutajengwa viwanda cha mawese wakati ni mbali na dar, mbona tuliambiwa kitajengwa kiwanda cha mabati ngara, tuamini hii yote ilikuwa ni usanii na haiwezekani?

Ngoja tuangalie, ni kwanini kuna viwanda Kilimanjaro, Kagera, Mwanza, Iringa na Mbeya, inamaana hao hawakujua kwamba itahusisha gharama za usafiri na kwamba ni mbali na dar inakoonekana ni kituo cha biashara?

Halafu tuangalie, ni kwanini tumbaku inalimwa Tabora na kiwanda kiwekwe Moro wakati gharama ndo zile zile kiusafiri na solo?
 
Naunga hoja. Haiingii AKILINI kuona mkoa mmoja PWANI ndo kila kitu. Kwani mikoa mingine haiihitaji hivyo VIWANDA?

Ndo maana serikali ya devolved government INAHITAJIKA. Hii ndo njia pekee ITAKAYOONDOA kutokuwa na usawa katika MAENDELEO MIKOANI.
As long as KATIBA ndo hii. Vituko kama hivi HAVITAISHA.
Kama ni hivyo basi IWANDA vigawanywe- EVENLY/ katika USAWA.
Sema pia HAIKUINGII akilini Gesi kuwa Mtwara
 
Kuna kitu unakizungumza kwa uzuri sana na kinaeleweka sana. Lakini hebu ngoja tuone, kweli ni ishu ya raw material? Kweli ni ishu ya miundombinu tu? Kweli ni ishu ya entry ama kuna kingine chini chini?

Hivi ni kwa kiasi gani serikali inaonekana kushiriki kuona inahakikisha viwanda vinasambaa mikoa mingine?
Kwa maana nyingine inamaanisha malighafi zilizoko mikoa mingine hazitakuja kupata viwanda kwasababu ni mbali na airport na harbour?
Mbona tulisikia Kigoma kutajengwa viwanda cha mawese wakati ni mbali na dar, mbona tuliambiwa kitajengwa kiwanda cha mabati ngara, tuamini hii yote ilikuwa ni usanii na haiwezekani?

Ngoja tuangalie, ni kwanini kuna viwanda Kilimanjaro, Kagera, Mwanza, Iringa na Mbeya, inamaana hao hawakujua kwamba itahusisha gharama za usafiri na kwamba ni mbali na dar inakoonekana ni kituo cha biashara?

Halafu tuangalie, ni kwanini tumbaku inalimwa Tabora na kiwanda kiwekwe Moro wakati gharama ndo zile zile kiusafiri na solo?
Mkuu hizi geographical division mara nyingi ndio zinasababisha tofauti ya uchumi kati ya mikoa na mikoa. Kwa uelewa wangu mdogo ni kuwa, kwa issue kama hizi serikali inabidi kufikiria nje ya box juu ya kuinua uchumi kwa sehemu ambazo haziko karibu na bahari na pia air port kubwa mfano elimu kama chuo cha UDOM kimeweza kutoa ajira na wanafunzi wanatumia pesa hii inakuza uchumi wa Dodoma, vitu vingine ni kama IT industry pia inaweza kuboreshwa.
 
Asubuhi mnasema serikali haijajenga kiwanda hata kimoja, kabla haijafika jioni mnaanza kusema viwanda vinajengwa pwani - Ukiwa bavicha unakuwa na akili nyumbu mpaka huruma
Haya mambo tunayaongea kama watanzania mkuu na wala si kwasababu ya vyama. Na nikuhakikishie, wenzio kama wewe wengine mie uniita kada wa CCM lakini leo wewe unahisi leo tunaoongea ni bavicha. Hii ni nzuri kwasababu huitaji kuwa na itikadi ndo uongee haya, ni fikra tu za mwanadamu kwamba unaweza kufikiri na kuyatafutia majibu yale maswali ya msingi sana. Kwa maana hiyo na wewe jisikie huru kuchangia, sie ni watanzania na tunaongea kuhusu nchi yetu.
 
Asubuhi mnasema serikali haijajenga kiwanda hata kimoja, kabla haijafika jioni mnaanza kusema viwanda vinajengwa pwani - Ukiwa bavicha unakuwa na akili nyumbu mpaka huruma
Haya mambo tunayaongea kama watanzania mkuu na wala si kwasababu ya vyama. Na nikuhakikishie, wenzio kama wewe wengine mie uniita kada wa CCM lakini leo wewe unahisi leo tunaoongea ni bavicha. Hii ni nzuri kwasababu huitaji kuwa na itikadi ndo uongee haya, ni fikra tu za mwanadamu kwamba unaweza kufikiri na kuyatafutia majibu yale maswali ya msingi sana. Kwa maana hiyo na wewe jisikie huru kuchangia, sie ni watanzania na tunaongea kuhusu nchi yetu.
 
N
Mkuu hizi geographical division mara nyingi ndio zinasababisha tofauti ya uchumi kati ya mikoa na mikoa. Kwa uelewa wangu mdogo ni kuwa, kwa issue kama hizi serikali inabidi kufikiria nje ya box juu ya kuinua uchumi kwa sehemu ambazo haziko karibu na bahari na pia air port kubwa mfano elimu kama chuo cha UDOM kimeweza kutoa ajira na wanafunzi wanatumia pesa hii inakuza uchumi wa Dodoma, vitu vingine ni kama IT industry pia inaweza kubworeswa.
Umenikuna sana aisee, before Udom Dom palionekana choko sana lakini leo ni habari nyingine. Kusema kweli tunataka hivi vitu vikubwa visambazwe badala ya kurundikwa kwani vina athari kubwa kiuchumi na hakuna wa kulisimamia hili zaidi ya serikali.
 
N

Umenikuna sana aisee, before Udom Dom palionekana choko sana lakini leo ni habari nyingine. Kusema kweli tunataka hivi vitu vikubwa visambazwe badala ya kurundikwa kwani vina athari kubwa kiuchumi na hakuna wa kulisimamia hili zaidi ya serikali.
Ni kweli kabisa, elimu ni biashara nzuri kama inawekezwa vizuri. Fikiria kama ukisikia kuna shule nzuri ya A-level hata kama iko Kigoma au Mtwara lakini watoto wanafundishwa vizuri na wanafaulu, kwa gharam yeyote utampeleka mtoto wako.
 
Viwanda vinajengwa na wawekezaji siyo serikali .
Mwekezaji anachagua sehemu kulingana na mahitaji yake kama ardhi iliyopimwa tayari kwa eneo la viwanda,maji,umeme,malighafi,usafirishaji wa bidhaa zake na malighafi ,soko nk.
Sasa jiulize mikoa mingine kama wana maeneo ya viwanda yenye miundombinu kama maji,umeme, Barabara.
Je malighafi zinapatikana kiurahisi.
Wakuu wa mikoa wasimamie kuvutia wawekezaji watangaze mikoa yao tatizo wamekaa tu maofisini wanasubiria mshahara mwisho wa mwezi hawana mikakati yoyote.
Mkoa kama Tanga ilibidi wawe na kiwandani kikubwa cha kusindika machungwa ya Muheza,mkoa wa Iringa,Njombe,Ruvuma ilibidi wawe na viwanda vikubwa vya kusindika unga wa sembe,viwanda vya mbolea,madawa ya mimea nk.
Kwahiyo ni jukumu la mikoa husika kupambana katika kuvutia wawekezaji.
 
Mkuu Rweye

Hilo unalolifahamu liweke bayana tu, nina uhakika sababu za viwanda kuwa maeneo hayo unaijua.

Kulikuwa na mpango wa kupiga pipe kutoka kwenye GEEEZ mpaka kwenye bahari ili kuuzwa kwa urahisi, ingawa nadhani GEEEEZ ile iko baharini.

Ndio vivo hivyo...
 
Back
Top Bottom