Viwanda 1,845 vyaanzishwa mwaka mmoja

Viwanda 1,845 vyaanzishwa mwaka mmoja

Ni utani au wako serious?

Inawezekana hata kufunga maji ya kandoro wanahesabu kama ni kiwanda
 
Kwa mindset kama hizi hakuna mtu yeyote makini atayetuchukulia serious!

Pamoja na maendeleo ya teknolojia sijawahi kuona wala kusikia duniani popote pale ambapo kuna KIWANDA kilichoajiri MTU 1.

Japan pamoja na advancement in robotics technology lakini mpaka sasa hivi hawana hata kiwanda kimoja kilichoajiri mtu mmoja.

Huu utakuwa ni UTANI mbaya kutoka kwa PM! Very sad enough hii hotuba imeingia kwenye hansard za bunge.
 
Tz ya viwanda ni ndoto wakati hata chakula ni shida huko mikoani, viwanda bila chakula cha kutosha wapi na wapi
 
Viwanda vya kuuza kahawa ile chungu ya kwenye tuvikombe tweupe tudogo tudogo.Hafu wateja wake wanajua kila kitu mpaka siku ya kurudi yesu kristu wanaifahamu,uliza chochote tu pale utapata jibu,wanafahamu pia kuwa Sadam Hussein alikuwa Rais wa Kuwait.Wajinga ndiyo waliwao.
 
" Alisema katika matokeo ya sensa hiyo hadi kufikia mwaka 2013, Tanzania ilikuwa na jumla ya viwanda 49,243 ambapo viwanda vidogo vinavyoajiri mtu mmoja hadi wanne vilikuwa ni asilimia 85.13 na viwanda vidogo vyenye watu watano hadi 49 vilikuwa asilimia 14.02.

Alisema matokeo hayo pia yalionesha kuwa viwanda vya kati vyenye watu 50 hadi 90 vilikuwa ni asilimia 0.35 na viwanda vikubwa vyenye watu kuanzia 100 na kuendelea ni asilimia 0.5.

Hivyo, Asilimia 99.15 ya viwanda vyote nchini ni viwanda vidogo ".
 
Hivyo viwanda viko wilaya gani na mkoa gani?
Ni mashine za kusaga mahindi ndio hivyo viwanda kweni hapo mtaani kwenu hakuna hicho kiwanda kimoja !? [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Nafikiri wamehesabu na wale wamama wanaoponda kokoto kule Africana ni kama viwanda.

Ni kama wakati wa JK..
Kila siku tulikuwa tunaambiwa ajira zimeongezeka... kumbe wanahesabu bodaboda zilizosajiliwa kwa biashara TRA na wale waokota makopo ya plastic... Shame!!
[emoji106] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Kumbe huyu fundi sofa aliyepanga barazani kwangu naye ana miliki kiwanda kwa tafsiri ya serikali
 
Ni mashine za kusaga mahindi ndio hivyo viwanda kweni hapo mtaani kwenu hakuna hicho kiwanda kimoja !? [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]


Jamani huh ni uhuni live mtaani kwetu hakuna kiwanda cha kukoboa na kusaga mahindi.
Mimi naona wameandika Mashine ya kusaga na kuoboa mahindi.
 
Labda viko majumbani kwao make mie huku niliko siyo mkoa wala wilaya ..tokea wameingia hawa jamaa sijaona kiwanda chochote kipya hata cha kukaanga vitumbua, sijaona
Na hautakuja kuviona kamwe. Unaishi jijini habari mpya kwako ni ile unayoiona ITV au Channel Ten, utaweza vipi kuziona fursa zilizojaa kila mkoa. Kama wewe wapo wengi sana.
 
Labda viko majumbani kwao make mie huku niliko siyo mkoa wala wilaya ..tokea wameingia hawa jamaa sijaona kiwanda chochote kipya hata cha kukaanga vitumbua, sijaona
Hata cha Azzam
 
bwana mfalme amesema tangu ameingia pale ikulu amefungua kiwanda 1 tu na ukweli hakuna viwanda vipya Zaidi hata 5 awamu hii ....siku hizi hata machine ya chaki inaitwa kiwanda tena na msomi kanisa anajiita Dr.....leo anasema machine za tofali ni viwanda; basi nadhani ile size ya kiwanda unga au juice vya SSB sijui tutaitaje ambavyo vimeajiri watu 3,000 plus...ikiwa machine tofali ya watu 3 inaitwa kiwanda; walipoanza kutoa ahadi walidhani ni mwendo kasi? tunataka viwanda wasilete utani....hakuna watoto wala wapumbavu karne hii
 
Back
Top Bottom