ila kwa hili nasema kuwa wanaume wengine hapa wanajisheua tuu....wanaosababisha wanawake wanajibadilisha ni hawa wanaume...Utakuta mwanamme anataka msichana mweupe...angalia asilimia kubwa za wanaume wapo na wanawake gani...
Pia kuna wanawake black ambao ni wazuri kama huyo hapo ila kuna wanawake wengine black hawapendezi...akipaka makeup ndio anakuwa kituko bora apake poda na wanja tuu...
ila mwanamke mweupe hata kama ni mweupe kidogo (maji ya kunde / kahawia ilokolea) huwa hawa wanapendeza mara nyingi hasa akiwa soft...kama wasomali ...n.k..
Jiulize kwanini Wasukuma hutoa mahari kubwa kwa wanawake weupe?
Kwanini kanda za Arusha, Kilimanjaro, Singida, Tanga, Upareni wapo juu sana.... utakuta ni colour ndizo zinazowapaisha...
Msemakweli mpenzi wa Mungu.
Kama ni kuhusu hili suala linatakiwa lianze kwa wanaume, wabadilike kuacha kupenda wanawake weupe
Hili halitofautiani na lile janga la wanawake bapa kupotea, sasa hivi utakuta kila mwanamke ni kajichubua, na anakalio hilo...Je hawa walikuwa wapi? Msichana akishakuwa tuu akijitambua hasa wasichana wa vyuo, Wanaenda kwa mchina kukuza kalio....
Wanaume kwanini mnapenda makalio, au mnapenda nyuma..?
BADILIKENI WANAUME