Vituko vya watawala wa Afrika

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,581
46,176
1. Mwaka 1994 Bakili Muluzi aliyekuja kuwa Rais wa Malawi aliwapa ahadi ya kila mwananchi kupewa pea ya viatu endapo watamchagua kuwa Rais wao.Baada ya kuchaguliwa akawaambia wananchi wake hakuna namna angeweza kujua saizi za miguu yao wote ili waweze kupata viatu vyao walivyohaidiwa wakati wa uchaguzi hivyo asingeweza kuitimiza ahadi yake.

2. Mawaziri nchini Cameroon mara nyingi huwa wanalazimika kukutana na Rais wao Paul Biya airport kwa ajili ya shughuli za kiserikali kwa sababu anaendesha nchi yake kutokea Intercontinental Hotel iliyoko Geneva, Switzerland, Ulaya.

Aliwahi kukaa kipindi cha miaka mitatu(2015-2018) bila kuitisha kikao cha baraza la mawaziri.

3. Museveni amemtua mke wake kuwa waziri. Yani waziri wa Elimu wa Uganda ni mke wa Rais. Mtoto wake ni Mkuu wa kikosi maalum cha jeshi.

4.Rais wa Kwanza wa Zimbabwe alikuwa akiitwa Canaan Banana. Wananchi walizoea kufanyia jina lake la Ndizi utani sana.Mwaka 1982 alipitisha sheria ya kuzuia kutumia jina lake katika kwa utani.

5.Mobutu aliyekiwa Rais wa Congo DRC alipiga marufuku matumizi ya majina ya kizungu na kutaka raia wote wabadili majina ya kizungu kwenda ya Kiafrika.Yeye mwenyewe alibadili jina lake kutoka Joseph-Désiré Mobutu hadi Mobutu Sese Seko Kuku Ngbendu Wa Za Banga.

Aliibadilisha nchi yake jina pia kutoka Congo na kuiita Zaire.
 
😹😹 Namba moja inanikumbusha kisa kimoja Huko madafu nation, ambapo baada ya kukusanya michango na misaada mbalimbali (Sum of Billions) kwaajili ya kuwasadia wahanga wa tetemeko la ardhi, alisikika kiongozi mmoja mkubwa akieleza umma kuwa katika ilani yake ya uchaguzi hakuwahi kuahidi kuleta Tetemeko la ardhi. Kisha kutumia fedha za misaada kwa ujenzi wa miundombinu ndani ya kanda yake.
 
IMG_3932.png

Chato punda traffic lights
 
unasema vituko vya watawala wa africa alafu unataja watatu tu
 
Umenikumbusha Bakili Muluzi, wale tulikuwa tunasikiliza MBC (Malawi Broadcasting oorporation). Kulikuwa na nyimbo za kumsifu Bakili mwanzo mwisho......Bakili Mulizi Boma, President wa Muyaya (Rais wa milele).....
 
Afrika hajuwai kuwa serious kabisa toka Dunia imeanzishwa..

Wazungu wametuachia mifumo ya kijinga sana na nidhamu za kifala..

Watu kama MKWAWA wakifufuka leo wanaeza fikiri bado tunaongozwa na wakoloni.

Mbona wazungu walitawala zaidi ya Afrika na walivyotoka nchi hizo hazijawa na mifumo ya kijinga na nidhamu za kifala? Wahindi, Waarabu, Wacaribbean, na wengine walitawaliwa na wakoloni wazungu lakini siyo kama sisi. Tujilaumu sisi wenyewe kwanza.
 
1. Mwaka 1994 Bakili Muluzi aliyekuja kuwa Rais wa Malawi aliwapa ahadi ya kila mwananchi kupewa pea ya viatu endapo watamchagua kuwa Rais wao.Baada ya kuchaguliwa akawaambia wananchi wake hakuna namna angeweza kujua saizi za miguu yao wote ili waweze kupata viatu vyao walivyohaidiwa wakati wa uchaguzi hivyo asingeweza kuitimiza ahadi yake.

2. Mawaziri nchini Cameroon mara nyingi huwa wanalazimika kukutana na Rais wao Paul Biya airport kwa ajili ya shughuli za kiserikali kwa sababu anaendesha nchi yake kutokea Intercontinental Hotel iliyoko Geneva, Switzerland, Ulaya.

Aliwahi kukaa kipindi cha miaka mitatu(2015-2018) bila kuitisha kikao cha baraza la mawaziri.

3. Museveni amemtua mke wake kuwa waziri. Yani waziri wa Elimu wa Uganda ni mke wa Rais. Mtoto wake ni Mkuu wa kikosi maalum cha jeshi.

4.Rais wa Kwanza wa Zimbabwe alikuwa akiitwa Canaan Banana. Wananchi walizoea kufanyia jina lake la Ndizi utani sana.Mwaka 1982 alipitisha sheria ya kuzuia kutumia jina lake katika kwa utani.

5.Mobutu aliyekiwa Rais wa Congo DRC alipiga marufuku matumizi ya majina ya kizungu na kutaka raia wote wabadili majina ya kizungu kwenda ya Kiafrika.Yeye mwenyewe alibadili jina lake kutoka Joseph-Désiré Mobutu hadi Mobutu Sese Seko Kuku Ngbendu Wa Za Banga.

Aliibadilisha nchi yake jina pia kutoka Congo na kuiita Zaire.
Mwaka 2015 JPM aliwaahidi wananchi kuwapa milioni 50 kila kijiji, baada ya kuwa Rais akasema pesa hizo anawajengea miundo mbinu ya barabara, hospitali, ndege na meli!!!!

Sent from my itel A32F using JamiiForums mobile app
 
Mbona wazungu walitawala zaidi ya Afrika na walivyotoka nchi hizo hazijawa na mifumo ya kijinga na nidhamu za kifala? Wahindi, Waarabu, Wacaribbean, na wengine walitawaliwa na wakoloni wazungu lakini siyo kama sisi. Tujilaumu sisi wenyewe kwanza.

Umeliona hilo mkuu!! Yaani tunakuwa watu wa kuamini kuwa mzungu anatakiwa aondoke dunia hii ndio mambo yetu yaende!!! Tutaendelea kulaumu wengine kwa madhaifu yetu tusiyotaka kuyashughulikia mpaka lini??
 
Tumechoka na vitisho vyenu vya mitandaoni wakati mkiambiwa muingie mtaani mnawaogopa hao mnaowatisha! PUMBAVU!!!
Sumu haijaribiwi kwa kuonjwa.Hao watawala wakiamua wanakuua,sasa hapo mpumbavu atakuwa nani?Kuepusha mbawa.
 
Back
Top Bottom