Vituko vya Wanasiasa katika Uchangiaji wa Maabara

tatanyengo

JF-Expert Member
Mar 30, 2011
1,134
280
Ukiwa umebaki takribani mwezi mmoja kufikia kilele cha ujenzi wa maabara katika shule za sekondari zote nchini, kumeibuka tafrani katika maeneo mbalimbal nchini. Tafrani hizo zinatokana na wanasiasa kutumia mbinu mbalimbali ikiwezo nguvu katika kuwachangisha michango.

Mfano, walimu katika halmashauri kadhaa wamekatwa mishahara bila ridhaa yao, baadhi ya viongozi kutoa kauli zinazokinzana (Lusinde - uchangiaji ni hiari, mkuu wa wilaya Fatma Ally - uchangiaji ni lazima), Waziri wa TAMISEMI Kasimu Majaliwa kukanusha kuwa serikali haikuagiza walimu wakatwe mishahara, Mkuu wa wilaya ya Uyui kumsimamisha mtendaji wa kijiji kwa kushindwa kufikia malengo ya uchangiaji na baadhi ya wananchi mkoani Singida kuasi na kuwashambulia watendaji waliokuwa wanachangisha michango ya maabara. Ilimradi tu ni mshike mshike. Kila kiongozi kuanzia wakuu wa mikoa hadi watendaji wa vijiji hakuna anayetaka kuonekana mzembe. Kwa jinsi hali ilivyo hasa vijijini, baadhi ya vijana wamekimbilia porini kukwepa sekeseke la watendaji.

Yawezekana katika eneo lako kuna vituko vinavyohusiana na michango ya maabara, tuendelee kujuzana ili watanzania wafahamu kinachojiri katika nchi yao.
 
Nipo kwenye kitengo cha kuhakikisha maabara zinajengwa mkoani kwangu bora nikae kimya kwa leo!
 
Basi tu ni udikteta. Mzembe ni Profesa Dr JK ambaye alitoa ahadi bila kujua hizo pesa zingetoka wapi au alisahau kuwa itikadi ya chama ni ufisadi na hivyo hela ya walipa kodi haiwezi kutosha kujenga maabara. Sasa muda wa ahadi umetimia anakurupuka kutoa amri za kidikteta kuswaga binadami kama mbuzi wanapelekwa malishoni. Mimi mtendaji akithubutu kukanyaga kwangu namtandika risasi unless kama atakuja na ripoti kamili ya mapato na matumizi ya kata au wilaya ya mwaka wa fedha wa 2013/2014 inyoonesha wapi kuna pengo.
 
Kwani change ya rada imeishia wapi maana walisema wamenunua mdawati kila wilaya hakuna cha dawati hadi leo watoto wanakaa chini.maabara zitajengwa kwa amri vitendea kazi navyo itakuwa amri?maskini watz tunaonewa ndani ya tz yetu.
 
Diwani wa kata yangu kupitia cdm amesimamia vizuri fedha za halmashauri na tumekamilisha maabara katika sekondari zetu 2
 
Kwani change ya rada imeishia wapi maana walisema wamenunua mdawati kila wilaya hakuna cha dawati hadi leo watoto wanakaa chini.maabara zitajengwa kwa amri vitendea kazi navyo itakuwa amri?maskini watz tunaonewa ndani ya tz yetu.

Hilo nalo sijui inaelekea hii michango itakuwa ya kudumu ili maabara ziwezi kufanya kazi.
 
Back
Top Bottom