Ndugu wanajf
Mambo mengine yanayoyasikika na kushuhudiwa kwa macho kuhusu uchaguzi mkuu wa 2010, yanastahili kupewa jina moja tu VITUKO VYA UCHAGUZI kwani naamini kuwa huwa ni nadra sana kufanyika katika kipindi tofauti na hiki.
Kwa maslahi ya historia ya nchi yetu, nashawishi mambo haya kuwekwa kwenye kumbukumbu kwa kuanzisha thread kuhusu mambo ambayo yanaonekana kuwa si ya kawaida kusikika au kuonekana katika maisha ya kila siku japokuwa mengine hutokea.
Lakini kwa kuwa yanatokea katika kipindi hiki cha uchaguzi na katika harakati za vyama vya siasa au wagombea kutafuta uhalali wa kuchaguliwa na kupewa ridhaa ya kuongoza, hayana budi kuhusishwa moja kwa moja na uchaguzi mkuu wa 2010.
Aidha nashawishika kuyaweka kwenye kumbukumbu kwa sababu mengi yao, hayapewi nafasi katika vyombo vya habari aidha kwa makusudi, bahati mbaya au kutokuwa na mvuto kwa wahariri na waandishi wetu wa habari.
Kwa upande wangu naanza na kituko kifuatacho.
Mgombea Urais kupitia CCM, Bw. J.M. Kikwete, akiwa katika safari ya kampeni Mkoani Rukwa, gari lake lilipata ajali ambayo lau kama angalikuwemo, pengine habari ingekuwa tofauti kwani gari hilo limekuwa written off kiasi ambacho kama comprehensive insurance, basi Insurer ajiandae kununua gari jingine jipya. Mungu saidia JMK alikuwa ametangulia kwa Chopa.
Lakini jambo la ajabu ni kwamba tukio hilo halikutangazwa na chombo chochote. Lakini kubwa kuliko yote ni kwa gari hilo kubanduliwa namba fasta baada ya ajali na kupekelekwa katika kituo cha polisi cha Namanyele likiwa halina namba.
Mambo mengine yanayoyasikika na kushuhudiwa kwa macho kuhusu uchaguzi mkuu wa 2010, yanastahili kupewa jina moja tu VITUKO VYA UCHAGUZI kwani naamini kuwa huwa ni nadra sana kufanyika katika kipindi tofauti na hiki.
Kwa maslahi ya historia ya nchi yetu, nashawishi mambo haya kuwekwa kwenye kumbukumbu kwa kuanzisha thread kuhusu mambo ambayo yanaonekana kuwa si ya kawaida kusikika au kuonekana katika maisha ya kila siku japokuwa mengine hutokea.
Lakini kwa kuwa yanatokea katika kipindi hiki cha uchaguzi na katika harakati za vyama vya siasa au wagombea kutafuta uhalali wa kuchaguliwa na kupewa ridhaa ya kuongoza, hayana budi kuhusishwa moja kwa moja na uchaguzi mkuu wa 2010.
Aidha nashawishika kuyaweka kwenye kumbukumbu kwa sababu mengi yao, hayapewi nafasi katika vyombo vya habari aidha kwa makusudi, bahati mbaya au kutokuwa na mvuto kwa wahariri na waandishi wetu wa habari.
Kwa upande wangu naanza na kituko kifuatacho.
Mgombea Urais kupitia CCM, Bw. J.M. Kikwete, akiwa katika safari ya kampeni Mkoani Rukwa, gari lake lilipata ajali ambayo lau kama angalikuwemo, pengine habari ingekuwa tofauti kwani gari hilo limekuwa written off kiasi ambacho kama comprehensive insurance, basi Insurer ajiandae kununua gari jingine jipya. Mungu saidia JMK alikuwa ametangulia kwa Chopa.
Lakini jambo la ajabu ni kwamba tukio hilo halikutangazwa na chombo chochote. Lakini kubwa kuliko yote ni kwa gari hilo kubanduliwa namba fasta baada ya ajali na kupekelekwa katika kituo cha polisi cha Namanyele likiwa halina namba.