Baraghash
JF-Expert Member
- Dec 18, 2012
- 2,713
- 1,786
Rais Islam Karimov, wa Uzbekistan. nchi kutoka kati ya bara la Asia,amefariki dunia kwa ugonjwa wa kiharusi akiwa na umri wa miaka 78.
Alitawala nchi yake kwa mpini wa chuma kwa zaidi ya robo karne tokea nchi yake ilipopata uhuru wake baada kusambaratika utawala shirikisho la Urusi.
Aliweza kutawala muda wote huo kutokana na Sifa yake kuu,yaani kuudumaza,kuukandamiza na hatimae kuusambaratisha kabisa upinzani nchini mwake.
Hakuna habari zaidi zilizopatikana kutokana na tasnia ya habari na uhuru wa kutoa maoni humo ulivyo dhibitiwa na kuminywa nchini humo.Kutokana na utawala wake kuwa wa ki- imla, hakuna mrithi wa moja kwa moja anaetambulika, hivyo kifo chake kmeacha mwanya wenye ufa ya uongozi.
Karimov atakumbukwa kuwa Nduli, katili, mwenye hasira kali, kauli za kutisha na uamuzi wa haraka.Majeshi yake yaliwaangamiza kwa kuwapiga risasi mamia ya waandamanaji wasio kuwa na silaha kwa kosa la kupinga utawala wake mwaka 2005.
Aliwatia ndani Maelfu ya wapinzani wake lakini kubwa zaidi,lisilioweza kusahaulika ni kitendo cha vikosi vyake vilipo wachemsha wapinzani wake kwenye maji ya moto mpaka kufa.
Atakumbukwa pia kwa tabia yake ya kuwapigia makelele, kuwaadhibu, kufuta nyadhifa na kuchagua maofisa wake katika mikutano ya hadhara.
Alikaririwa akisema "niko tayari kunyofoa vichwa vya watu 200 ikiwa kwa kufanya hivyo kuta kuwa ni muhanga wa kuleta amani katika nchi - ikiwa hata mwanangu atafuata njia hyo, basi nita mkata kichwa mimi mwenyewe"
Karimov alipotembelea Jumuia ya ulaya na kukutana na kiongozi wa juu walipeana mikono;kitendo kilicholeta taharuki kubwa na kutuhumiwa kimataifa kwa mkuu huyo wa EU kukubali kupeana mikono na Karimov!
Karimov amezikwa jana
Tumejifunza nini?
Alitawala nchi yake kwa mpini wa chuma kwa zaidi ya robo karne tokea nchi yake ilipopata uhuru wake baada kusambaratika utawala shirikisho la Urusi.
Aliweza kutawala muda wote huo kutokana na Sifa yake kuu,yaani kuudumaza,kuukandamiza na hatimae kuusambaratisha kabisa upinzani nchini mwake.
Hakuna habari zaidi zilizopatikana kutokana na tasnia ya habari na uhuru wa kutoa maoni humo ulivyo dhibitiwa na kuminywa nchini humo.Kutokana na utawala wake kuwa wa ki- imla, hakuna mrithi wa moja kwa moja anaetambulika, hivyo kifo chake kmeacha mwanya wenye ufa ya uongozi.
Karimov atakumbukwa kuwa Nduli, katili, mwenye hasira kali, kauli za kutisha na uamuzi wa haraka.Majeshi yake yaliwaangamiza kwa kuwapiga risasi mamia ya waandamanaji wasio kuwa na silaha kwa kosa la kupinga utawala wake mwaka 2005.
Aliwatia ndani Maelfu ya wapinzani wake lakini kubwa zaidi,lisilioweza kusahaulika ni kitendo cha vikosi vyake vilipo wachemsha wapinzani wake kwenye maji ya moto mpaka kufa.
Atakumbukwa pia kwa tabia yake ya kuwapigia makelele, kuwaadhibu, kufuta nyadhifa na kuchagua maofisa wake katika mikutano ya hadhara.
Alikaririwa akisema "niko tayari kunyofoa vichwa vya watu 200 ikiwa kwa kufanya hivyo kuta kuwa ni muhanga wa kuleta amani katika nchi - ikiwa hata mwanangu atafuata njia hyo, basi nita mkata kichwa mimi mwenyewe"
Karimov alipotembelea Jumuia ya ulaya na kukutana na kiongozi wa juu walipeana mikono;kitendo kilicholeta taharuki kubwa na kutuhumiwa kimataifa kwa mkuu huyo wa EU kukubali kupeana mikono na Karimov!
Karimov amezikwa jana
Tumejifunza nini?