FirstLady1
JF-Expert Member
- Jul 29, 2009
- 16,792
- 5,373
Wanaachishwa sana tena. Na wengine wanazuiwa kabisa kufanya kazi. Kuna wadada 2, wana Master degrees na wamezuiwa kunyanyua mguu kutafuta kazi.
Hapana dada. Kila ndoa ni taifa huru. Kwa hiyo usidhani wote wanaishi kama nyie. Wapo akina mama pamoja na kukata shule wanalazwa chini na kutandikwa viboko kwa makosa ya kipuuzi kama kuvunja chupa ya chai.
Hata hivyo mimi sipendi tabia za namna hiyo. Mama akiwa huru familia inakuwa na amani zaidi. Na uhuru ni pamoja na kufanya kazi na kuwa na uhuru wa kuamua jinsi ya kutumia mapato yake. Hata hivyo inabidi aangalie mipango mizima ya maendeleao ya familia kwa ujumla!
Ndoa za sasa zinavyokuja na mawimbi na dhoruba kali ...wazo la kuachishana kazi nadhani lingekuwa la mwisho kufikirika