Unachotakiwa kujua ni kwamba kwanza yupo kwenye Development bado hajafikia kiwango hasa cha Artificial General Intelligence (AGI)na uwezo wa kutambua vitu katika muktadha wake ikiwemo hisia na context kwa ujumla kwa hiyo mara nyingi anakariri kwa weredi mkubwa kulingana na Data alizokuwa trained kwa hiyo usitegemee majibu yake yakawa exactly kama binadamu anayeweza kufanya critical thinking hata kutambua mood au hisia za muulizaji na inasemekana ili kufikia kiwango cha Artificial General Intelligence (AGI) inaweza kutumia miongo kadhaa kutokea sasa pamoja na advancement zote hizo, na pia ikumbukwe huu ndio kama mwanzo wa hii era ya AI ni sawa na ilivyokuwa bitcoin miaka ya 2013 - 14.
Ingawa uwezo kamili wa akili ya binadamu haujawahi fikiwa na kitu chochote kilichowahi tengenezwa isipokuwa vitu hivyo viko more specific to certain tasks only lakini sio General purpose ndio maana mwanadamu aliye Daktari anaweza ku play kama tabibu hospital lakini akirudi nyumbani ni Baba, tena mume wa mtu lakini huyo huyo ni mwenyekiti wa Saccos yao na ni mtunza fedha wa jumuiya anayosali na hapohapo ndio Kaka mkubwa kwa familia anayotoka na anajua kuendesha gari yake bila kusababisha ajali na pote huko anaplay part differently kitu ambacho hakuna machine au computer inaweza kufanya, ingawa zenyewe in terms of speed, performance and correctness zipo vizuri lakini bado hazifikia Human intelligence (GI). Kwa kuwa hazifikirii na hazina uwezo wa kujifunza zenyewe kama anavyofanya binadamu mpaka ziwe trained for a certain specific purpose kwa Data fulani