Vituko mitandaoni. Tupia chako

Wladimir "Dr. Steelhammer" Klitschko alipokutana na Anthony Joshua enzi zile bado anatembeza vitasa sawasawa. Klitschko alikula uppercut moja matata sana en route to being knocked out ...na akastaafu mazima.

Ila yeye na kakake bondia (Vitali Klitschko ambaye kwa sasa ndiye meya wa jiji la Kyiv kule Ukraine) wamegeuka mashujaa baada ya kukataa kuondoka nchini Ukraine ilipovamiwa na Urusi. Pamoja na kwamba ni mamilionea na wangeweza kuondoka na kwenda kuishi po pote duniani, walikataa na moja kwa moja wakajiunga na jeshi ili kupigania nchi yao. Bado wanapambana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…