Vituko mitandaoni. Tupia chako

Maana unaweza kula ugali ki- D'salaam ukaonekana huwezi kula, hivyo huwezi kumfikisha juu ya kilele bint yao

Nimewaza tu.
Unaweza ukakosa mke kwa mlo tu
Kusema kweli inabidi ule. Tena ule hasa. Usipokula yaweza kuonekana pengine umewadharau hawajui kupika, unaona pengine mazingira ni machafu, unajiona na sababu zingine kibao. Kama huna uwezo wa kula ugali angalau basi ule nyama. Kawaida ni mbuzi utachinjiwa au kuku mzima mzima kila mara utakapokwenda ukweni mpaka baadaye sana utakapozoeleka. Kama huwezi kula mwambie mkeo/mchumba wako akakutetee huko kwa wapikaji!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…