Vitu gani vinahitajika kufungua kampuni?

Joeli

JF-Expert Member
Apr 25, 2011
4,941
3,402
Nimekuwa na mawazo yangu, lakini kwa sasa nataka kuyaweka in reality, nataka kufungua kampuni hapa tanzania ila sijui pa kuanzia, sijui natakiwa kuwa na vitu gani ili niweze kufungua iyo kampuni. Wataalamu au wenye uzoefu naombeni msaada wenu
 
Tembelea website ya BRELA TANZANIA . Ingia google utaiona, Ina kila Kitu hadi gharama.ukikwama nipm.
 
Nimekuwa na mawazo yangu, lakini kwa sasa nataka kuyaweka in reality, nataka kufungua kampuni hapa tanzania ila sijui pa kuanzia, sijui natakiwa kuwa na vitu gani ili niweze kufungua iyo kampuni. Wataalamu au wenye uzoefu naombeni msaada wenu

Naam mkuu C6 ili uweze kufungua kampuni unatakiwa uwe na vitu vifuatavyo:
  1. Kwanza kabisa unatakiwa uwe na jina la kampuni ambalo unataka kulitumia...ukishalipata nenda BRELA kuhakikisha kama limeshachukuliwa na mtu au la...kama bado unaweza kulilipia ili lisichukuliwe.
  2. Baada ya hapo utatakiwa kuandaa document ambayo inaitwa Memorandum and The Articles of Association ambayo inaelezea kwa kina kuhusu shughuli ambavyo ziatafanywa na kampuni na namna ambavyo kampuni yako itaendeshwa. Kazi hii hufanywa na wanasheria japo siku hizi kuna watu wa kawaida ambao wanaweza kuandika hii document.
  3. Baada ya kumaliza kuandika hii document utaenda BRELA kuchukua fomu kuijaza na kulipia malipo yote yanayotakiwa then utapewa muda wa kusubiri na siku ambayo utatakiwa kwenda kuchukua Certificate of Incorporation.
  4. Baada ya kumalizana na registration kabla ya kampuni kuanza kufanya kazi lazima uwe na leseni na TIN number. Unaanza kwanza kwenda kuchukua TIN TRA ambayo inatolewa bure japo kuipata ni mbinde hadi utoe kitu kidogo then ukishapata hiyo TIN number unaenda manispaa kuchukua leseni yako ambayo nayo pia ina gharama zake.
  5. Ukishamaliza hayo yote then kampuni yako inaweza ku-operate.
 
Last edited by a moderator:
Jamaa hapo juu kakuelezea vizuri sana!! ndivyo hivyo changamka, JAPO kuna urasmu hadi utachoka. Wengine wana fanya shortcut!! usifanye hivyo waweza pata certificates feki, zisizo tambulika na TRA na wadau wengine hata BRELA wenyewe; Chunga sana CONMEN wamejaa pale Lumumba na ktk jengo lile!

Pia tumia wataalam wakuandikie Memorandum & Article of Ass. wapo wa kawaida kama sisi na pia wanasheria. All the best!
 
Naam mkuu C6 ili uweze kufungua kampuni unatakiwa uwe na vitu vifuatavyo:
  1. Kwanza kabisa unatakiwa uwe na jina la kampuni ambalo unataka kulitumia...ukishalipata nenda BRELA kuhakikisha kama limeshachukuliwa na mtu au la...kama bado unaweza kulilipia ili lisichukuliwe.
  2. Baada ya hapo utatakiwa kuandaa document ambayo inaitwa Memorandum and The Articles of Association ambayo inaelezea kwa kina kuhusu shughuli ambavyo ziatafanywa na kampuni na namna ambavyo kampuni yako itaendeshwa. Kazi hii hufanywa na wanasheria japo siku hizi kuna watu wa kawaida ambao wanaweza kuandika hii document.
  3. Baada ya kumaliza kuandika hii document utaenda BRELA kuchukua fomu kuijaza na kulipia malipo yote yanayotakiwa then utapewa muda wa kusubiri na siku ambayo utatakiwa kwenda kuchukua Certificate of Incorporation.
  4. Baada ya kumalizana na registration kabla ya kampuni kuanza kufanya kazi lazima uwe na leseni na TIN number. Unaanza kwanza kwenda kuchukua TIN TRA ambayo inatolewa bure japo kuipata ni mbinde hadi utoe kitu kidogo then ukishapata hiyo TIN number unaenda manispaa kuchukua leseni yako ambayo nayo pia ina gharama zake.
  5. Ukishamaliza hayo yote then kampuni yako inaweza ku-operate.
Mkuu hapo juu ameleza vizuri sana.Ila tatizo utamaliza soli za viatu..sababu hata kusearch jina kwenye website yao haitasaidia sbabu database haiko updated nafikiri kwa makusudi ,na ukifuate utaratibu wa pale ofisini kwao sijui kujaza fomu nk utakesha...cha kufanya waone wataalamu ya mambo hayo amabo wanajua jinsi ya ku fast track the process....documents ni zilezile zenyewe ila mbinu tu tofauti...kama ukihitaji service hiyo ni pm
 
Nimekuwa na mawazo yangu, lakini kwa sasa nataka kuyaweka in reality, nataka kufungua kampuni hapa tanzania ila sijui pa kuanzia, sijui natakiwa kuwa na vitu gani ili niweze kufungua iyo kampuni. Wataalamu au wenye uzoefu naombeni msaada wenu

ukifanikiwa mkuu naomba uniajiri.
 
Wakati wa kuandikisha kampuni, unaweza chagua kama unataka sole propreatorship, partnership au corporation?
 
..nimeshasajili business name BRELA, na nipo katika mchakato wa kumaliza kusajili kampuni na kupata licences, Hakuna usumbufu wowote nimekutana nao pale BRELA na hata kuregister wameniambia itachukua less than 3 working days. Ushauri wangu ni kuwa jitahidi uandae hizo documents (MEMART) tena tumia mwanasheria kaka, achana na maneno ya mtaani na vishoka, fuata taratibu na waone wahusika stahili, UTAFANIKIWA. Na kwa maelezo zaidi tembelea web ya BRELA..i think ni : BRELA.
 
Back
Top Bottom