Baada ya mahakama ya kazi kushindwa kutoa hukumu hadi Agosti 2, vitisho kutoka kwa wakuu wa mikoa na polisi vinazidi. Huku Arusha polisi wamesema wataanza kupita mashuleni kubaini walimu wasiohudhuria shule na kuwasaka eti wao ndiyo wanaowatisha wale wasaliti wachache ambao wanategemea migongo ya wanaogoma kana kwamba wao wanalipwa tofauti. Kana kwamba hiyo haitoshi serikali imetoa fomu ya walimu kujaza kukubali kugoma au kuendelea na kazi. Hapa udhaifu wa serikali unazidi kuonekana. Hao wanaohojiwa kwenye redio hasa TBC si walimu ila ni mbinu za kuwatisha walimu. Mgomo utaendelea hadi kieleweke! Hao wanaosekana kuhudhuria si kwamba wanafundisha ila wanajipendekeza wachaguliwe kusimamia sensa. Na hata hivyo hawawezi kufundisha masomo yasiyo yao. Yawezekana hawa ndio wale vihio wanaotumia vyeti bandia au za ndugu zao na wanataka wasijulikane.