Come27
JF-Expert Member
- Dec 1, 2012
- 7,503
- 7,107
Habari za siku ya leo, kwanza poleni kwa mapumziko ya weekend,
Naomba tujadili vitendo vya wizi maeneo makubwa ya kibiashara kama apa Mlimani City na maeneo ya Magomeni NMB bank.
Kumekuwepo na vitendo vya ukiingia bank za hapo Mlimani city kunakuwa na watu wanakufatilia mpaka utakapotoka na kama ukiingia kwenye maeneo ya Parking ya Mlimani City karibia na barabarani uwezekano wa kutolewa Bastola ni mkubwa sana, na wezi wengi wanakuwa wamepaki gari ya Noah kama watu wengineo uwezi kumtambua na maeneo ya pale Mlimani City karibia wengi wanajulikana mpaka kwa wale walinzi wa Mlimani City.
Na kuhusu ishu ya walinzi uwenda wakawa wana husika nao kwasababu jioni ikishafika pale Mlimani City kunakuwa na machangudoa wanajiuza maeneo ya parking ya magari kama wateja. Sasa pale serikali inaboresha vip? Ulinzi kwa watu wanaofika pale kuchukua pesa.
Na kwa upande wa Magomeni Usalama maeneo ya NMB bank. Kuna vitendo vya wizi sana, unamaliza kutoa pesa bank unatoka na mwizi ndani ya bank mule mule, hivi katika hizi Taasisi zinashindwa kuboresha ulinzi katika sehemu zao za kazi.
Naomba tujadili vitendo vya wizi maeneo makubwa ya kibiashara kama apa Mlimani City na maeneo ya Magomeni NMB bank.
Kumekuwepo na vitendo vya ukiingia bank za hapo Mlimani city kunakuwa na watu wanakufatilia mpaka utakapotoka na kama ukiingia kwenye maeneo ya Parking ya Mlimani City karibia na barabarani uwezekano wa kutolewa Bastola ni mkubwa sana, na wezi wengi wanakuwa wamepaki gari ya Noah kama watu wengineo uwezi kumtambua na maeneo ya pale Mlimani City karibia wengi wanajulikana mpaka kwa wale walinzi wa Mlimani City.
Na kuhusu ishu ya walinzi uwenda wakawa wana husika nao kwasababu jioni ikishafika pale Mlimani City kunakuwa na machangudoa wanajiuza maeneo ya parking ya magari kama wateja. Sasa pale serikali inaboresha vip? Ulinzi kwa watu wanaofika pale kuchukua pesa.
Na kwa upande wa Magomeni Usalama maeneo ya NMB bank. Kuna vitendo vya wizi sana, unamaliza kutoa pesa bank unatoka na mwizi ndani ya bank mule mule, hivi katika hizi Taasisi zinashindwa kuboresha ulinzi katika sehemu zao za kazi.