Vitendo SACCOS - kukopeshana bila riba

Kuna tofauti mkuu, riba haiangalii hasara, upate hasara au upate faida ni lazima ulipe riba na inachajiwa kila mwaka, na pia lazima ulipe kile ulichokopa.
Mfumo wa Islamic Finance ni tofauti, wao ni kama wanatumia mfumo wa hisa katika biashara kwa muda maalumu mtakaokubaliana kisha baada ya hapo unaachiwa biashara inakuwa yako peke yako. Mfumo huu wa kiislamu hasara ikipatikana wewe uliokopeshwa hutadaiwa kwasababu hiyo ni biashara yenu wote kwa muda maalum. Mnachogawana ni faida ya biashara husika mpaka yule aliyekukopesha atakaporudisha pesa yake na faida kidogo kisha anakuachia biashara inakuwa yako peke yako kama mlivokubaliana. Mfano ni wa kuwapa vijana bodaboda kwa mikataba, huu mfumo ni kama kumkopesha kijana bila riba yeye anapata kitu kwa biashara ile kila siku na wewe unapata na baada ya muda maalumu mliokubaliana kijana anabaki na pikipiki yake. Jee hii ni riba?? Hii si riba bali ni faida ya biashara. Kuna tofauti ndogo kati ya faida na riba, usipokuwa makini utachanganya hivi vitu viwili.
asante nimekuelewa vizuri sana
 
Hiyo ni aina moja na aina nyingine ni kuingia ubia wa bishara husika inayochukuliwa mkopo. Faida inayopatikana mnagawana kwa asilimia husika za kama ubia mwengine wowote mpaka deni litakapokwisha. Asilimia ya deni hupungua kila unapolipa kutokana na faida na asilimia ya faida ya wakopeshaji pia hupungua.

Mwisho wote mnakuwa winners, wote mmepata faida na wote hamjatoa wala kupokea riba.

Tatizo kubwa la kuuelewa mfumo huu ni pale suala la "kukopa" linavyotafsiriwa, kukopesha kwa riba, mkopaji anakabidhiwa pesa akafanyie shughuli aliyoainisha katika kukopa kwake, kama ni kweli au uongo inabaki siri yake na mara nyingine ya wale walioidhinisha akopeshwe, hakuna siri kuwa wengi hupewa mikopo kwenye ma benki ya riba kwa kuwa afisa wa mikopo nae atafaidika kwa kuhongwa kutokana na kopo huo.

Pia ukopeshaji wa riba, uwe wa benki au biashara za watoaji mikopo hujikita zaidi katika kutoa mikopo ili riba ndiyo ilete faida. Hiyo riba ndio biashara yenyewe ya kuingizia faida.

Tofauti na benki au taasisi zisizotoa riba ni kuwa, faida ya tasisi hizi hupatikana katika kuwekeza na si katika riba, ukienda kukopa kibiashara basi wakopeshaji huitathmini biashara yako na kuingia ubia na wewe ili mgawane faida katika hiyo biashara, kwa mfumo huu mtagawana pia na hasara ikitokea bahati mbaya.
swali jingine nisaidie kuelewa ikiwa biashara yangu ikashindwa kufanikiwa tofauti na nilivyotarajia, biashara ikafa hapo inakuaje wataendelea kunidai au utaratibu utakuwaje?
 
Kila mtu inatakiwa ajiandikishe pamoja na namba zake za simu. Siku hizi njia rahisi ni kutumiana pesa kwa njia ya simu.

Unaweza wakati wa kujiandikisha ukatupa namba za account yako ya benki na tutafanya utaratibu wa kukuingizia marejesho kwenye account yako ukipenda.

nyie mkikimbiwa je?
 
Wadau wote,

Napenda kuwafahamisha kuwa jana tarehe 1-5-2017 tulikuwa na kikao kuhusu kuanzishwa kwa SACCOS yetu mpya.

Wahudhuriaji wa walikuwa wa kutosha. Kati yao walikuwepo (wengi wao) ambao ni wawekezaji tayari katika miradi yetu ya awali (nje ya SACCOS tarajiwa), wengine ni wawekezaji watarajiwa. Pia tulimualika Mwenyekiti wa serikali yetu ya mtaa wa Vitendo, ndugu Salehe Dibebile, tulimualika pia na Katibu wa vyama vya ushirika vya kata ya Misugusugu bwana Kussi. Pia tulikuwa na wawekezaji wawili ambao tayari wana miradi yao (nje na yetu) ya machimbo ya michanga.

Kwa kifupi, tulitambulishana, tukajadili ushirika tunaoufikiria na tukakubaliana (bila kuwa na hoja za kupingana). Hoja zilizotamalaki zilikuwa ni za kupeana elimu zaidi ya ushirika na faida zake...
Ikaamuliwa tuuanzishe ushirika haraka iwezekanavyo...

Ikaamuliwa tuanze kwa kukusanya masharti ya saccos tofauti na samples zake, members wote wapitie ili tuweze kuwa na SACCOS yetu tarajiwa haraka iwezekanavyo...

Imeamuliwa pia Abdu Ghafur awe Mwenyekiti wa muda mpaka ushirika wetu utakapo sajiliwa ndiyo kutakapokuwa na masharti ya uchaguzi rasmi. Watakaojiunga wote watakuwa wajumbe mpaka hapo sheria na kanuni rasmi rzitakapo patikana.

Pia Imeamuliwa kuanzia sasa kila atakaependa kujiunga kutakuwa na ada ya kiingilo itakayo saidia katika gharama za usajili na mpaka hapo tutapokuwa na masharti na kanuni zetu rasmi zilizopitishwa na wnahama wote kwa ujibu wa sheria...

Ushirika tutakaoanzisha utafata sheria na kanuni zote za nchi na sheria za vyama vya ushirika za Tanzania...

Ushirika hautakuwa na ukomo wa watakaojiunga mpka hapo itakapotangazwa rasmi baada ya kupata kanuni zilizokubalika na wanahama wote, kujiunga kutakuwa wazi kwa yeyote anaekubalika kisheria, awe popote Tanzania au duniani...

Ada ya kiingilo kwa sasa ni shillihgi 10,000 (elfu kumi) ambazo zitatumwa kwa Mwenyekiti wa muda kwa njia ya Mpesa. Namba ni 0756803528 jina Ghafur Abdallah Mohamed.

Mahesabu yote ya chama yatakuwa wazi kwa wanachama wote, kwa sasa yatapatikana kupitia group la whatsapp la waliojiunga.

Kila atakaelipa ataingizwa kwenye group mahususi la whatsapp litalokuwa kwa ajili ya wanachama tu waliojiunga katika ushirika wetu mpya.

Tumeanza kupokea ada za viingilio na hesabu zote zitapatikana kwenye group mpya ya wanachama walioingia kwa kulipia ada...

Uwe popote ulimwenguni unakaribishwa kujiunga kwa faida ya wote.

Group mpya imeshafunguliwa kwa jina la muda Vitendo SACCOS na members wawili waliolipia ada tayari tumepatikana, maelezo zaidi kwenye group mpya...

Ada ya kiingilo ni shillihgi 10,000 (elfu kumi) ambazo zitatumwa kwa Mwenyekiti wa muda kwa njia ya Mpesa. Namba ni 0756803528 jina Ghafur Abdallah Mohamed

Nawajulisha wote watakaotaka kujiunga muanze kwa kulipia ada ili tufanikishe usajili kwa haraka.

Ili kujiunga, (kwa sasa) inatakiwa utupatie jina kamili, namba za simu, email address na ulipo na utume 10,000 kwa Mpesa.

Tunakaribisha maswali.

Abdul
+255 625 249 605 (whatsapp)
kikao ni lini na wapi nije na elf 10 yangu pia kujifunza
 
swali jingine nisaidie kuelewa ikiwa biashara yangu ikashindwa kufanikiwa tofauti na nilivyotarajia, biashara ikafa hapo inakuaje wataendelea kunidai au utaratibu utakuwaje?

Kuna mambo kadhaa yanafanyika, kwa nia njema kabisa, kabla hujakopeshwa. Kutakuwa kuna jopo (kamati) watakaopitia ombi lako na kujiridhisha kuwa vigezo vya wewe na ushirika kufanya vizuri vimekidhi ukopeshwe na ushirika uwe mbia wako.

Kuna vigezo vya taaluma za ujasiriamali, je vinakidhi? Kama havikidhi na biashara inaonesha ni ya kuleta faida basi utaongezewa ujuzi kwa kupewa mafunzo (crush courses au seminars husika), kwa ufupi kuna vigezo kadhaa inabidi viwe vinakidhi ili ujipatiue mkopo na ushirika wawe wabia wako. Yote ni kuhakikisha unajikomboa na unapata mafanikio na ushirika wanapata mafanikio.

Biashara yako ikifa na ushirika umeingia ubia na wewe ina maana na ushirika umekula hasara pia, kitu ambacho ushirika itajitahidi kufanya isitokee na bahati mbaya ikitokea, tunaongelea kuwa na mifumo ya kulinda miradi mfano, investment insurance.

Napenda uelewe kuwa kila mkopo utaotolewa nao pia ni mradi wa ushirika mpaka deni litakapomalizwa.
 
sasa faida mnaipataje kama hakuna riba?

Tunakua wabia wa mradi wako unaouchukulia mkopo.

Napenda ufahamu kuwa faida inatakiwa kwanza upate wewe na washirika wenzako waliowekeza kwenye saccos ambao ni wote tuliojiunga. Lengo si wakopeshaji kupata faida kwa kukauana mpaka damu kwa njia za riba, lengo ni wabia kujikwamua kiuchumi.

It's a non-interest bearing loan. You don't have to pay the interest so that you don't worry about money growing in your hand. It won't grow, so take your time. Only thing is, if you pay us back fully you get more money. - Mohamed Yunus, father of microcredit and Nobel Peace Prize Winner
 
kikao ni lini na wapi nitakuja na elfu kumi yangu


Kikao cha awali kimeshafanyika tarehe 1-5-2017 na maazimio yaliopitishwa ni pamoja na kuanzishwa ushirika kwa haraka sana, na harakati za kuanzisha ushirika zimeshaanza. Kikao kijacho tutawatangazia hapa hapa JF na kama utakuwa umeshajiunga kwa kulipia kiingilio ha 10,000 basi utajulishwa pia kwa whatsapp na email.
 
Nami naitaji kitafanyikia wapi nije my wasapu 0713329624

Kikao cha awali kimeshafanyika tarehe 1-5-2017, Pwani, Kibaha , Misugusugu, mtaa wa vitendo na maazimio yaliopitishwa ni pamoja na kuanzishwa ushirika kwa haraka sana, na harakati za kuanzisha ushirika zimeshaanza. Kikao kijacho tutawatangazia hapa hapa JF na kama utakuwa umeshajiunga kwa kulipia kiingilio ha 10,000 basi utajulishwa pia kwa whatsapp na email.
 
Kikao cha awali kimeshafanyika tarehe 1-5-2017 na maazimio yaliopitishwa ni pamoja na kuanzishwa ushirika kwa haraka sana, na harakati za kuanzisha ushirika zimeshaanza. Kikao kijacho tutawatangazia hapa hapa JF na kama utakuwa umeshajiunga kwa kulipia kiingilio ha 10,000 basi utajulishwa pia kwa whatsapp na email.
ok ukitutangazia nitakuja mamy
 
Kuna mambo kadhaa yanafanyika, kwa nia njema kabisa, kabla hujakopeshwa. Kutakuwa kuna jopo (kamati) watakaopitia ombi lako na kujiridhisha kuwa vigezo vya wewe na ushirika kufanya vizuri vimekidhi ukopeshwe na ushirika uwe mbia wako.

Kuna vigezo vya taaluma za ujasiriamali, je vinakidhi? Kama havikidhi na biashara inaonesha ni ya kuleta faida basi utaongezewa ujuzi kwa kupewa mafunzo (crush courses au seminars husika), kwa ufupi kuna vigezo kadhaa inabidi viwe vinakidhi ili ujipatiue mkopo na ushirika wawe wabia wako. Yote ni kuhakikisha unajikomboa na unapata mafanikio na ushirika wanapata mafanikio.

Biashara yako ikifa na ushirika umeingia ubia na wewe ina maana na ushirika umekula hasara pia, kitu ambacho ushirika itajitahidi kufanya isitokee na bahati mbaya ikitokea, tunaongelea kuwa na mifumo ya kulinda miradi mfano, investment insurance.

Napenda uelewe kuwa kila mkopo utaotolewa nao pia ni mradi wa ushirika mpaka deni litakapomalizwa.
kwaio unataka kuniambia incase biashara ikafa, investment insurance itacover hio effect au bado sijaelewa?
 
Back
Top Bottom