Vita ya Wabena na Wakinga

Vita ya Wabena na Wakinga

Mgosi Mbena

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2023
Posts
500
Reaction score
608
Mwaka ni 1874 kabla ya wajerumani kuja kusini mwa Tanzania mkoa wa sasa njombe waliishi wabena ambalo kwa kipindi hiko lilikua ni kabila dogo.

Wabena ilikua ni kabila ambalo halina mfumo ambao uko centralised yaan hamna hakukua na mtawala mmoja aliyeongoza wabena wote ila kulikua na tawala ndogo ndogo hii ilikua na advantage lakini pia dis advantage ilikua ilikua ngumu kupambana na tawala kali na empire zenye nguvu kama Wajerumani.

Sasa mwaka 1874 ilitokea Vita kubwa kati ya wabena na wakinga ambayo mainly ilikua ni kuongeza himaya na wanawake. Ikumbukwe wanawake ilichukuliwa ni kitu serious watu walivamia himaya nyingine kuiba vyakula, mifugo na kubeba wanawake kama mateka ambao wakifika kwene himaya yao walikua wanageuzwa wake zao kwa ajili ya kuongeza koo familia zao.

Basi mwaka huo kundi dogo la wabena wa vijiji vivyo zunguka mlima kipengele walianziashisha uvamizi kwene himaya ya wakinga ambao walikua wapo kusini kabisa mwa himaya ya wabena ambapo kwasasa kunaitwa Makete.

Walivizia msimu wa baridi kali kabisa lile la mwezi wa sita ambapo maea nyingi barafu na umande hutua na kufunika ardhi ya makete ndio msimu walio vamia. Huu msimu uliwapa advantage kwani hawakua na jeshi kubwa kama nilivosema wameundwa na tawala ndogo ndogo na maadui zao ilikua ngumu kupigana kutokana na barafu kalii na ilikua ni vita ya kushtukiza.

Katika hali ya taharuki walishambuliwa na kupigwa sana kwa vita ya kushtukiza mpaka majeshi ya ukinga yakakimbilia milimani yakiacha familia na wake zao na vyakula na mifugo. Basi majeshi haya ya wabena yalifanikiwa kuchukua mazao ,mifugo wanawake vijana ambao walibebeshwa mazao kuelekea vijiji vya mlima kipengele.

Inakadiliwa watu zaidi ya 350 walipoteza maisha huku wanawake na mabinti wakichukuliwa.

YAANI MFANO KIJIJINI KWETU.
Kuna wabibi zaidi ya 20 nasimuliwa wao kiasili waliporwa ukingani kipindi cha vita. Hii inaonesha jinsi gani hata kulikua na muingiliano mkubwa na mfanano hasa hili swala la kupora wanawake wa makabila mengine
 
Endelea hivyo hivyo uishie pabaya uje uteswe uzuri halijawahi tokea na halitatokea la kumkosoa huyo mkureshi
Mkureshi alikua mbakaji katika kustawisha dola yake ya kikureshi ila alikomeshwa baada ya kumbaka mwanamke wa kiyahudi na kuwekewa sumu hadi akafa,mkureshi kafa kiboya hajafikia ushujaa kama machifu wengine waliokufa vitani wakitetea dola zao
 
Kule Zenji bar pia ilitokea hio mpaka mdogo wa Dada akaenda kumshuti bwana yule kwamba kwanini amemchukua Dada yake kinguvu na kumuua Baba yake pia
hii historia sijui naweza ipata wap nijisomee mwenyewe
 
Mkureshi alikua mbakaji katika kustawisha dola yake ya kikureshi ila alikomeshwa baada ya kumbaka mwanamke wa kiyahudi na kuwekewa sumu hadi akafa,mkureshi kafa kiboya hajafikia ushujaa kama machifu wengine waliokufa vitani wakitetea dola zao
Mkureshi alikua ni mtu siyo kabila
 
Endelea hivyo hivyo uishie pabaya uje uteswe uzuri halijawahi tokea na halitatokea la kumkosoa huyo mkureshi
aisee naona hyo mkureshi kapamba moto kuliko hata maada yenyewe
 
Mwaka ni 1874 kabla ya wajerumani kuja kusini mwa Tanzania mkoa wa sasa njombe waliishi wabena ambalo kwa kipindi hiko lilikua ni kabila dogo.

Wabena ilikua ni kabila ambalo halina mfumo ambao uko centralised yaan hamna hakukua na mtawala mmoja aliyeongoza wabena wote ila kulikua na tawala ndogo ndogo hii ilikua na advantage lakini pia dis advantage ilikua ilikua ngumu kupambana na tawala kali na empire zenye nguvu kama Wajerumani.

Sasa mwaka 1874 ilitokea Vita kubwa kati ya wabena na wakinga ambayo mainly ilikua ni kuongeza himaya na wanawake. Ikumbukwe wanawake ilichukuliwa ni kitu serious watu walivamia himaya nyingine kuiba vyakula, mifugo na kubeba wanawake kama mateka ambao wakifika kwene himaya yao walikua wanageuzwa wake zao kwa ajili ya kuongeza koo familia zao.

Basi mwaka huo kundi dogo la wabena wa vijiji vivyo zunguka mlima kipengele walianziashisha uvamizi kwene himaya ya wakinga ambao walikua wapo kusini kabisa mwa himaya ya wabena ambapo kwasasa kunaitwa Makete.

Walivizia msimu wa baridi kali kabisa lile la mwezi wa sita ambapo maea nyingi barafu na umande hutua na kufunika ardhi ya makete ndio msimu walio vamia. Huu msimu uliwapa advantage kwani hawakua na jeshi kubwa kama nilivosema wameundwa na tawala ndogo ndogo na maadui zao ilikua ngumu kupigana kutokana na barafu kalii na ilikua ni vita ya kushtukiza.

Katika hali ya taharuki walishambuliwa na kupigwa sana kwa vita ya kushtukiza mpaka majeshi ya ukinga yakakimbilia milimani yakiacha familia na wake zao na vyakula na mifugo. Basi majeshi haya ya wabena yalifanikiwa kuchukua mazao ,mifugo wanawake vijana ambao walibebeshwa mazao kuelekea vijiji vya mlima kipengele.

Inakadiliwa watu zaidi ya 350 walipoteza maisha huku wanawake na mabinti wakichukuliwa.

YAANI MFANO KIJIJINI KWETU.
Kuna wabibi zaidi ya 20 nasimuliwa wao kiasili waliporwa ukingani kipindi cha vita. Hii inaonesha jinsi gani hata kulikua na muingiliano mkubwa na mfanano hasa hili swala la kupora wanawake wa makabila mengine
niliwahi kusikia wabena na wakinga hadi wasangu, walikuwa chini ya Mkwawa, walitawaliwa na chief wa wahehe. labda hayo unayoongea yalitokea baada ya Mkwawa kufa, ila sio wakati wake.
 
Back
Top Bottom