"Virungu" vimezidi...

"Virungu" vimezidi...

Vipi humu mmeamkaje jamani?naona mko powA kabisa za masiku mingi?kila siku nakuonaga unaenda kazinihihihi kikiki
Ahaa sie mambo bado magumu bana ila kuna michongo nafatilia mambo yatakuwa powa sana
Wewe naweza kukuchukulia hata mchunba ukampa shem ya kuendea sokoni kama ka ist waonaje mkuu
Saaa mkuu nina shida ndugu yangu japo hata ka fifute hivi ntakurudishia kesho
Naona umejiwahi kujitetea kwa kuwa huu ni mwisho wa mwezi
Ebu nigei aasee
 
Ghafla JF imegeuka kua ya watu wote Ni waajiriwa na hua wanapigwa mizinga tu.
 
Ndugu zangu habarini?

Siku hizi imezuka tabia ya watu kuomba pesa hovyo especially ikifikia mwisho wa mwezi.

Yan mtu akisikia una kazi, kila mwisho wa mwezi lazima atengeneze shida.

Tunapenda sana kusaidia ndugu, jamaa na marafiki lakini tambueni hata sisi tunaofanya kazi tuna yetu.

Wengine hatupendi kuombaomba sio sababu sina matatizo ila sababu najiheshimu na ninajitambua. Kuombaomba ni tabia mbaya.

Sikatai kuwa kuna siku nawakopa wenzangu lakini ni mara chache sana na hadi nilazimike kufanya hayo.

Mnapoona tupo kimya, msidhani tuna pesa. Tuna madeni lukuki, tuna makodi, tuna mahitaji binafdi, wategemezi nk.

Mtatuchukia bure na kutusababishia tupate dhambi ndogondogo za kudanganya kuwa tumetimuliwa kazini.
Unashindwa kuwakatalia huko mpaka uje ututangazie?
 
Ndugu zangu habarini?

Siku hizi imezuka tabia ya watu kuomba pesa hovyo especially ikifikia mwisho wa mwezi.

Yan mtu akisikia una kazi, kila mwisho wa mwezi lazima atengeneze shida.

Tunapenda sana kusaidia ndugu, jamaa na marafiki lakini tambueni hata sisi tunaofanya kazi tuna yetu.

Wengine hatupendi kuombaomba sio sababu sina matatizo ila sababu najiheshimu na ninajitambua. Kuombaomba ni tabia mbaya.

Sikatai kuwa kuna siku nawakopa wenzangu lakini ni mara chache sana na hadi nilazimike kufanya hayo.

Mnapoona tupo kimya, msidhani tuna pesa. Tuna madeni lukuki, tuna makodi, tuna mahitaji binafdi, wategemezi nk.

Mtatuchukia bure na kutusababishia tupate dhambi ndogondogo za kudanganya kuwa tumetimuliwa kazini.
Mimi kuna jamaa yangu aliniomba nimkopeshe kiasi fulani nikampa, kabla hajalipa mwezi uliofuata akaniomba tena pesa nikampa, next month akanipiga tena kizinga nkamwambia sina. Akaniblok mana akaniona ni jitu baya nsiyefaa tena.
 
Omba omba sio wa kuwaendekeza, saidia wale ambao unaona kweli wana shida.

Bora wakuite mchoyo kuliko kukuchuna kila wanapojiskia utashtukia hufanyi maendeleo hela zinaishia kugawa kwa watu wasio na faida.
Dada mzuri acha uchoyo
 
Vp kuhusu michango ya harusi mleta mda anaongelea virungu kutoka kwa ndugu au jamaa na marafiki, harusi watu wanachangia sana kadi kama 10 unapokea na zote unachangia ila ndugu akiomba msaada malalamiko kibao basi na harusi tuache kuchangia
Afu wakipatwaga na masaibu wanakimbilia kwa ndugu hao hao.
 
Huwa naomba dolari, japo sipewi ila nitazidi kumbuguzi
 
Back
Top Bottom