Viongozi wetu mtusamehe na kuturehemu

Viongozi wetu mtusamehe na kuturehemu

Pantosha

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2022
Posts
869
Reaction score
1,282
Ni busara sana kuomba kusamehewa pale ambapo umekosea. Watanzania kulalamikia upatikanaji hafifu wa maji safi kwenye mabomba na kukatika katika kwa umeme naona ni kosa kubwa na hatustahili kuiomba serikali iboreshe huduma hizi muhimu kwa jamii.

Malalamiko haya yamekuwa ni kelele kwenye masikio ya baadhi ya watu. Yatupasa kuwaomba hao watu msamaha kwa kuwapigia kelele.

Kwa upande mwingine, tunaomba mturehemu kwani sisi pia tunahitaji huduma hizo muhimu kuishi, kujitafutia kipato na hivyo kuyafanya maisha yetu kuwa ya furaha.

Najua mnaweza kutoa rehema hizi kwetu na tutawasujudia na kuwaimbia nyimbo za sifa.
 
Mtanikumbuka kwa mazuri..enzi za JPM serikali ilikuwa bize kwa miradi ya kimkakati kuhakikisha inaondoa kabisa hizi kero..kulikuwa kuna miradi mingi kuanzia kanda ya ziwa(mradi mkubwa wa maji kutoka ziwa victoria), kaskazini(mradi mkubwa wa maji wa bill 500), magharibi(mradi wa maji kutoka ziwa victoria hadi tabora)na kati.

Miradi ya maji na umeme ilipamba moto. Wengi tuliona Tanzania iliyo bora katika ustawi wa huduma za kijamii. Navuta hadi sasa hizi kero ingekuwa imebaki historia. Hata vyanzo vya maji vililindwa na suma JKT na vilifungwa pia cameras. Haikuwa suala la kupigia kampeni ila ni utekelezaji.

Leo tunarudi miaka kadhaa nyuma. Enzi za umeme na maji tanzania imeshakuwa kero watu keroo keroo(wagosi wa kaya).

Tumerudi enzi za serikali ipo kwenye mchakato, nendeni mkaliangalie, serikali imelipokea..upuuzi upuuzi na ujinga wa wanaongoza umekuwa mwingi mno kuliko kuleta maendeleo.
 
Wa kurehemu,kusujudiwa ni Mungu baba pekee.

Shida tunaishi na tunafanya mambo yetu kwa mazoea.kila mwaka hali ni ile ile miaka nenda rudi.hakuna ubunifu wala ugunduzi. Hakuna mawazo ni namna gani ya kukabiliana na upungufu wa nishati ama maji kuepuka mgao na kukatakata.

Hatukai hata tukatafuta mbadala. Tumeozea.kikubwa mishahara inaingia basi mengine yarajisolve yenyewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, wenzako wanapishana angani huko kuangalia plots zao dubei.
 
Umefikia hatua mbaya sana! Yaani unamuomba mwanasiasa akurehemu!!! Mimi siku zote huwa ninawaombea wanasiasa nao njaa tu iwapate. Na wenyewe siku moja wale kwa jasho kama sisi. Nothing more.
 
Wa kurehemu,kusujudiwa ni Mungu baba pekee


Shida tunaishi na tunafanya mambo yetu kwa mazoea.kila mwaka hali ni ile ile miaka nenda rudi.hakuna ubunifu wala ugunduzi.hakuna mawazo ni namna gani ya kukabiliana na upungufu wa nishati ama maji kuepuka mgao na kukatakata.
Hatukai hata tukatafuta mbadala.
Tumeozea.kikubwa mishahara inaingia basi mengine yarajisolve yenyewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wenye mawazo mbadala huwa wanahesabiwa sio wenzetu hivyo hutengenezewa kashfa na mizengwe mingine ya kuwafifisha ili wasisikike tena !!
 
Ni busara sana kuomba kusamehewa pale ambapo umekosea. Watanzania kulalamikia upatikanaji hafifu wa maji safi kwenye mabomba na kukatika katika kwa umeme naona ni kosa kubwa na hatustahili kuiomba serikali iboreshe huduma hizi muhimu kwa jamii.

Malalamiko haya yamekuwa ni kelele kwenye masikio ya baadhi ya watu. Yatupasa kuwaomba hao watu msamaha kwa kuwapigia kelele.

Kwa upande mwingine, tunaomba mturehemu kwani sisi pia tunahitaji huduma hizo muhimu kuishi, kujitafutia kipato na hivyo kuyafanya maisha yetu kuwa ya furaha.

Najua mnaweza kutoa rehema hizi kwetu na tutawasujudia na kuwaimbia nyimbo za sifa.
Watu mpaka wamefunga salon zao kwa upuuzi wa TANESCO
 
Back
Top Bottom