Nape, ili kutenda haki tuanze na viongozi waongo

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,555
41,066
Hivi karibuni tumemsikia waziri Nape akieleza kuwa wale wote waliosema uwongo dhidi ya afya ya makamu wa Rais, atawachukulia hatua.

Mimi ni mtu ninayechukia sana uwongo, na hakika waongo wanastahili kuchukuliwa hatua.

LAKINI

Ili kutenda haki, na ili tuonekane tunachukia uwongo, tuanze kwanza kuchukua hatua dhidi ya viongozi waongo. Halafu ndiyo tushuke chini.

1) Waziri Nape, chukua hatua kwanza dhidi ya Mbarawa aliyeweza kuwadanganta wananchi na Bunge kuhususiana na IGA.

2) Waziri Nape chukua hatua dhidi ya Majaliwa aliyesema kuwa JPM alikuwa ofisini akichapa kazi wakati alikuwa kwenye hatua zake za mwisho za kupigania uhai wake.

3) Waziri Nape, chukua hatua dhidi ya Chalamila aliyesema kuwa JPM alimpigia simu, na akamwabia awasalimie wananchi wa Mbeya, wakati tayari JPM alikuwa marehemu.

4) Waziri Nape, chukua hatua dhidi ya January Makamba aliyesema baada ya matengenezo ya mitambo ya TANESCO, mgao wa umeme utakuwa historia.

Ukishamaliza kuchukua hatua dhidi ya hawa, tuje na hawa walioeneza kuwa Makamu wa Rais alikuwa mgonjwa mahtuti. Lakini hiyo itakuwa baada ya kufanya uchunguzi na kujiridhisha kuwa ni kweli hakuwa hospitalini.

Baada ya hapo, Waziri Nape, weka utaratibu utakaowawezesha wananchi kutoa taarifa juu ya viongozi waongo, ili kila kiongozi atakayesema uwongo, achukuliwe hatua mara moja. Maana serikali imejaa viongozi waongo ambao wameugeuza uwongo kuwa sehemu ya sifa za kiongozi.

Usipofanya hayo, wewe ni mnafiki tu, huna chembe ya kuuchukia uwongo.
 
Waliodanganya mitandaoni ndio anaowalenga!

Labda aanzie kwa waliomchafua Chongolo

Kwa kuwa kosa kubwa ni kusema uwongo, tuwashughulikie waongo wote bila kujali walitoa kauli kwa kutumia midomo au mitandao ya kijamii.

Nape awasiliane na wenzake wote ndani ya serikali ili tuwadhibiti waongo.
 
Mkuu kama unachukia uongo mbona hawa waliomchafua mzee Lowasa miaka 7, alaf wakaja kujaribu kumsafisha kwa mwezi mmoja wa uchaguzi hukuwataja?

Mpaka leo hawajaomba radhi kwa kutudanganya wala kuachia nafasi zao, kama sehemu ya kuonesha kusikitishwa na kitendo chao cha kutudanganya.

Au kunya anye kuku tu, lkn akinya bata kaharisha.

Mimi naamini 75% ya watanzania ni waongo wakiwemo viongozi wa serikali, vyama vya upinzani, tawala na raia wa kawaida.

Tukisema tuache unafiki wa kuwapendelea au kuwakomoa tu viongozi wa upande fulani. I mean tuamue kuwaengua waongo wote katika nafasi zao, basi viongozi wote wa vyama vya upinzani, tawala, serikali na mashirika mbali mbali hawatotakiwa kubaki katika nafasi zao.

Lkn tukisema tupambane na wa upande mmoja ambao sio wako na kuwaacha wale wa upande wako. Jua hapo haulimalizi tatizo bali unalipunguza. Kwani ingawa wale wa upande usiokuwa wako watatoka, wale wa upande wako wataendelea na uongo wao ule ule kama kawa.

Waswahili wanasema tabia haiachi asili. Mtu muongo ataendelea kuwa muongo tu daima. Hivyo kwa mujibu wa hii thread inatakiwa wote wasiwepo katika nafasi zao including yule makamu wa chama fulani aliedanganya eti mlinzi wa hayati Magufuli nae amefariki na corona, wakati mlinzi huyo hakufariki.
download (1).jpeg
DSC_6838.jpg
 
Aanze na Kasimu Majaliwa mwenye miaka 63 lakini kila siku anadanganya umma kua hana mvi hata moja,huo pia ni utapeli kwenye ofisi ya umma!!

Mtu kama huyo hapaswi kuaminiwa abadani!!
 
Mbona sasa hakuna atakayesalimika na kubaki huko Serikalini.
Hivi karibuni tumemsikia waziri Nape akieleza kuwa wale wote waliosema uwongo dhidi ya afya ya makamu wa Rais, atawachukulia hatua.



Usipofanya hayo, wewe ni mnafiki tu, huna chembe ya kuuchukia uwongo.
 
Kiongozi akisafiri lazima wananchi wajulishwe alipo, wananchi wasipojulishwa hawawezi kukaa kimya lazima wahoji, wahisi, na mwisho wajue alipo. Sasa wakuwajulisha ni muajiri wake ambaye ni serikali sasa serikali ipo kimya wanchi nao wawe kimya? Lazima wahoji na wawe na hisia tofauti.

Lakini kwa nini Serikali haifanyi iliyo wajibu wake?

Safari zingine mbona wanchi huwa wanajulishwa kwa nini hili la kusafiri Mpango liwe siri?

Napę Please Sheria Zisiwe za upande mmoja!
 
Aanze na Kasimu Majaliwa mwenye miaka 63 lakini kila siku anadanganya umma kua hana mvi hata moja,huo pia ni utapeli kwenye ofisi ya umma!!

Mtu kama huyo hapaswi kuaminiwa abadani!!
😂😂😂😂mkuu hivi anazo mvi? Sijawahi kuchunguza au anapakaga super black?
 
😂😂😂😂mkuu hivi anazo mvi? Sijawahi kuchunguza au anapakaga super black?
Zoom picha yake yoyote,huoni hata moja,yule mwamba itakua anatumia muda mwingi kupaka super black kuliko kazi,huenda anapaka kutwa mara 3 kama dozi ya mseto na kila sehemu ana mhudumu wake wa salon!!
 
Zoom picha yake yoyote,huoni hata moja,yule mwamba itakua anatumia muda mwingi kupaka super black kuliko kazi,huenda anapaka kutwa mara 3 kama dozi ya mseto na kila sehemu ana mhudumu wake wa salon!!
😂😂😂😂😂daaah

Sitaki kuamini kodi yangu majaliwa anaimalizia kwenye kile kichwa
Sijui ni zile za buku jero😂😂

Joking🤣
 
Hivi karibuni tumemsikia waziri Nape akieleza kuwa wale wote waliosema uwongo dhidi ya afya ya makamu wa Rais, atawachukulia hatua.

Mimi ni mtu ninayechukia sana uwongo, na hakika waongo wanastahili kuchukuliwa hatua.

LAKINI

Ili kutenda haki, na ili tuonekane tunachukia uwongo, tuanze kwanza kuchukua hatua dhidi ya viongozi waongo. Halafu ndiyo tushuke chini.

1) Waziri Nape, chukua hatua kwanza dhidi ya Mbarawa aliyeweza kuwadanganta wananchi na Bunge kuhususiana na IGA.

2) Waziri Nape chukua hatua dhidi ya Majaliwa aliyesema kuwa JPM alikuwa ofisini akichapa kazi wakati alikuwa kwenye hatua zake za mwisho za kupigania uhai wake.

3) Waziri Nape, chukua hatua dhidi ya Chalamila aliyesema kuwa JPM alimpigia simu, na akamwabia awasalimie wananchi wa Mbeya, wakati tayari JPM alikuwa marehemu.

4) Waziri Nape, chukua hatua dhidi ya January Makamba aliyesema baada ya matengenezo ya mitambo ya TANESCO, mgao wa umeme utakuwa historia.

Ukishamaliza kuchukua hatua dhidi ya hawa, tuje na hawa walioeneza kuwa Makamu wa Rais alikuwa mgonjwa mahtuti. Lakini hiyo itakuwa baada ya kufanya uchunguzi na kujiridhisha kuwa ni kweli hakuwa hospitalini.

Baada ya hapo, Waziri Nape, weka utaratibu utakaowawezesha wananchi kutoa taarifa juu ya viongozi waongo, ili kila kiongozi atakayesema uwongo, achukuliwe hatua mara moja. Maana serikali imejaa viongozi waongo ambao wameugeuza uwongo kuwa sehemu ya sifa za kiongozi.

Usipofanya hayo, wewe ni mnafiki tu, huna chembe ya kuuchukia uwongo.
Aah, sheria hii haiwahusu viongozi wa CCM, pia utekelezaji unaanzia kwa waliomsema makamu wa rais tu, tumekubaliana hivyo ili tusifukue makaburi.
 
Mkuu kama unachukia uongo mbona hawa waliomchafua mzee Lowasa miaka 7, alaf wakaja kujaribu kumsafisha kwa mwezi mmoja wa uchaguzi hukuwataja?

Mpaka leo hawajaomba radhi kwa kutudanganya wala kuachia nafasi zao, kama sehemu ya kuonesha kusikitishwa na kitendo chao cha kutudanganya.

Au kunya anye kuku tu, lkn akinya bata kaharisha.

Mimi naamini 75% ya watanzania ni waongo wakiwemo viongozi wa serikali, vyama vya upinzani, tawala na raia wa kawaida.

Tukisema tuache unafiki wa kuwapendelea au kuwakomoa tu viongozi wa upande fulani. I mean tuamue kuwaengua waongo wote katika nafasi zao, basi viongozi wote wa vyama vya upinzani, tawala, serikali na mashirika mbali mbali hawatotakiwa kubaki katika nafasi zao.

Lkn tukisema tupambane na wa upande mmoja ambao sio wako na kuwaacha wale wa upande wako. Jua hapo haulimalizi tatizo bali unalipunguza. Kwani ingawa wale wa upande usiokuwa wako watatoka, wale wa upande wako wataendelea na uongo wao ule ule kama kawa.

Waswahili wanasema tabia haiachi asili. Mtu muongo ataendelea kuwa muongo tu daima. Hivyo kwa mujibu wa hii thread inatakiwa wote wasiwepo katika nafasi zao including yule makamu wa chama fulani aliedanganya eti mlinzi wa hayati Magufuli nae amefariki na corona, wakati mlinzi huyo hakufariki.
View attachment 2840150View attachment 2840151
Na unasema kabisa "wakaja kumsafisha" case closed. Wewe ndo unaonekana ndondocha
 
Na unasema kabisa "wakaja kumsafisha" case closed. Wewe ndo unaonekana ndondocha
Acha uzuzu wa kuabudu na kutetea baba wa wenzako.

Tuliodanganywa ni sisi wananchi, hivyo walitakiwa watuombe radhi kwanza sisi waliotudanganya, alaf ndo waendelee kusafishana.

Naona baba wa wenzako wamekuleta jujuu kuja kuwatetea, wakati watoto wao hawana muda wa kuja kumtetea wakwako.
 
😂😂😂😂😂daaah

Sitaki kuamini kodi yangu majaliwa anaimalizia kwenye kile kichwa
Sijui ni zile za buku jero😂😂

Joking🤣
Za buku jero ngozi ingemuumbua huyu Katelephone anfuja kodi zetu kwa kupaka ya bei ghali!!

Mwaka fulani nilikutana nae Korogwe kwenye msiba wa mke wa Mufti,alikujq kwenye saa 5 hivi hotel moja inaitwa Korogwe Executive lodge,akaingia kuoga na kubadili nguo, nafikiri lengo kuu lilikua kupaka super black ila muda ukawa haitoshi,akatoka amevaa kanzu na kofia wakelekea msibani.

Hadi leo nimekariri ukiona kavaa kofia ujue kokoto halijakubali!!
 
Hivi karibuni tumemsikia waziri Nape akieleza kuwa wale wote waliosema uwongo dhidi ya afya ya makamu wa Rais, atawachukulia hatua.

Mimi ni mtu ninayechukia sana uwongo, na hakika waongo wanastahili kuchukuliwa hatua.

LAKINI

Ili kutenda haki, na ili tuonekane tunachukia uwongo, tuanze kwanza kuchukua hatua dhidi ya viongozi waongo. Halafu ndiyo tushuke chini.

1) Waziri Nape, chukua hatua kwanza dhidi ya Mbarawa aliyeweza kuwadanganta wananchi na Bunge kuhususiana na IGA.

2) Waziri Nape chukua hatua dhidi ya Majaliwa aliyesema kuwa JPM alikuwa ofisini akichapa kazi wakati alikuwa kwenye hatua zake za mwisho za kupigania uhai wake.

3) Waziri Nape, chukua hatua dhidi ya Chalamila aliyesema kuwa JPM alimpigia simu, na akamwabia awasalimie wananchi wa Mbeya, wakati tayari JPM alikuwa marehemu.

4) Waziri Nape, chukua hatua dhidi ya January Makamba aliyesema baada ya matengenezo ya mitambo ya TANESCO, mgao wa umeme utakuwa historia.

Ukishamaliza kuchukua hatua dhidi ya hawa, tuje na hawa walioeneza kuwa Makamu wa Rais alikuwa mgonjwa mahtuti. Lakini hiyo itakuwa baada ya kufanya uchunguzi na kujiridhisha kuwa ni kweli hakuwa hospitalini.

Baada ya hapo, Waziri Nape, weka utaratibu utakaowawezesha wananchi kutoa taarifa juu ya viongozi waongo, ili kila kiongozi atakayesema uwongo, achukuliwe hatua mara moja. Maana serikali imejaa viongozi waongo ambao wameugeuza uwongo kuwa sehemu ya sifa za kiongozi.

Usipofanya hayo, wewe ni mnafiki tu, huna chembe ya kuuchukia uwongo.
Naunga mkono hoja
 
Nape angeanza mutuambia Starlink wamekosa vigezo gani kutuletea huduma hapa!
Anachokifanya hakina maslahi na Watz wengi.
 
2) Waziri Nape chukua hatua dhidi ya Majaliwa aliyesema kuwa JPM alikuwa ofisini akichapa kazi wakati alikuwa kwenye hatua zake za mwisho za kupigania uhai wake.

3) Waziri Nape, chukua hatua dhidi ya Chalamila aliyesema kuwa JPM alimpigia simu, na akamwabia awasalimie wananchi wa Mbeya, wakati tayari JPM alikuwa marehemu.

hili liliniudhi kupita kawaida mpaka nashindwa kuwasamehe kwa kweli.Mtu yuko kwenye jokovu then unasema eti anapiga kazi .daaaaah
 
Back
Top Bottom