Viongozi wa Serikali kuwa viongozi wa chama sio afya kwa ustawi wa utawala bora!

Bome-e

JF-Expert Member
Jan 3, 2014
17,104
26,070
Wanabodi,mambo ambayo yametokea katika awamu ya 5 yamenifanya nione umhumi wa kutenganisha kofia hizi mbili ili kuleta matokeo chanya zaidi katika utawala bora usiohodhisha madaraka kwa mtu mmoja!

Chama cha siasa kilichotoa Rais kinapaswa kufanya tathimini ya utekelezaji wa sera na ilani yake unaofanywa na serikali!

Sasa kwenye vikao hivyo unakuta wale wale viongozi wa serikali ndio wanakuwa viomgozi wa chama,hapo ndio unajiuliza nani anafuatilia utendaji wa mwenzake!Yaani kwa lugha nyepesi ni kama unajifanyia tathimini mwenyewe na hapo ndio kunaibuka mgongano wa maslahi!
Nitoe mifano michache,

-2015 kikosi kazi na think tank ya CCM ilikaa na kuja na ilani!Katika mambo ambayo walijadili kama chama na kuyaweka katika ilani ni pamoja na kipengele kinachoeleza kuwa watawapa fursa ya kuendelea na masomo watoto wote ambao watapata ujauzito mara baada ya kujifungua!Vichwa makini ndani ya CCM viliona jambo hilo ni muhimu,Rais akazunguka kuinadi ilani hiyo nchi nzima!

Alipochaguliwa moja kwa moja akabadili muelekeo na kusema kwenye utawala wake marufuku mtoto atakayepata mimba/kujifungua kurudi katika mfumo rasmi !Katika hilo nilitegemea CCM iisimamie serikali kutekeleza ilani waliyokubaliana,ndio hapo unakuta Mwenyekiti ni huyo huyo ambaye ametenda kinyume na ilani ya chama!Hapo tunaona kuwa kofia hizi mbili zikivaliwa na mtu mmoja,dhana nzima ya chama kusimamia serikali katika utekelezaji wa ilani inakwama!

Tunachoona hapa ni viongozi wengine,wajumbe wa NEC na kamati kuu kunywea maana Boss ni yule yule pande zote,serikalini na chamani!

-Pia tumeona kauli zisizo nzuri zikitolewa na mkuu wa nchi mara watz wanapokutwa na Majanga,lakini hakuna wa kumwambia kutoka kwenye chama kuwa unakosea maana yeye mwenyewe ndiye mwenyekiti!

-Tumeona namna ambavyo tofauti zake na viongozi wastaafu amelazimisha chama kizibebe!Hajaridhishwa na maongezi yalivyofanyika dhidi ya Membe,kinana na Makamba hivyo ameamua kuiamuru kamati ya maadili kufikisha report ili ajiridhishe na kilichotokea,ameona kama kamati ilikuwa soft kwa wahojiwa!Hapa tunaona mgongano wa maslahi kwenye kofia hizi mbili!

-Tunaona Rais anavyoagiza wizara ya ardhi irudishe ardhi kwa halmashauri,lakini anawashauri halmashauri wajenge hata ofisi ya chama wakirejeshewa ardhi hiyo!Sasa hapo ndio unaona anashindwa kujua kuwa sio kazi ya halmashauri kujenga ofisi za chama chochote cha siasa!

-Kofia hizo mbili zimewafanya wanaccm wengi kuwa ndio mzee,maana hawana namna kwani wanaona kwa vitendo kuwa siyo afya kuwa na mawazo tofauti na Mwenyekiti ambaye ndiye Rais!

Niishie hapo!
 
Hawaelewi sababu ni mbili kubwa, UKAIDI NA UZINDAKI WA KUTOPENDA KUBADILIKA na kingine UMBUMBU WA VIONGOZI WA CHAMA.

Binafsi ni sisiem ila sipendi huu upuuzi wa viongozi kushika nyazifa mbili CHAMA na SERIKALI uwajibikaji na ubabe unakuwa mkubwa.

stupid AFRICA
 
Mkuu umeamka vibaya nini?Umechangia kwa hasira sana!
Sidhani kama huko CCM kuna mtu anayeweza kupendekeza kuwa hizi kofia mbili zitenganishwe!
 
Nafasi zote alizonazo Rais Magufuli, uenyekiti na urais ni za kuchaguliwa hivyo huwezi kupiga marufuku na hii itaonesha wazi kabisa mna kusudi jingine.

Labda uko upinzani sijui kukoje lakini CCM jambo lolote hata dogo kiasi gani linapitia kwenye vikao na kupatiwa baraka za vikao. Hata Serikali Kuna utaratibu wa vikao pia.

Nafasi ya uenyekiti na urais zote ni za kimamlaka hivyo wote waliopo chini ya hizo nafasi waheshimiwe. Kwenye vikao vya CHADEMA , Mbowe akikohoa tu wengine wanahofu( ni utani tu nimechomekea). Unaposema CCM ni ndio mzee tu unapotosha, kama kanuni na taratibu zinaruhusu kutoa maoni watatoa na wanatoa.
 
KARLO MWILAPWA,
Mkuu,think tank ya CCM ilikaa 2015 na kuja na ilani ambapo ilitamka mtoto wa kike atakayepata ujauzito atapewa fursa ya kuendelea na masomo atakapojifungua! Magufuli amebatilisha hilo kwa amri yake mwenyewe,hata mama Samia Suluhu alikuwa hajui!

Ndio maana kwenye mkutano mmoja mama samia suluhu akasema juu ya watoto wanaopata mimba kuendelea na masomo,baada ya siku moja JPM akatoa tamko kuwa kwenye utawala wake hakuna kitu kama hicho!

Sasa ukirudi kwenye chama,yeye ndiye mwenyekiti!Ni nani wa kumueleza kuwa tulikaa tukakubaliana hiki,kwanini umeenda kinyume? Yaani JPM kawaona watunga ilani ni wajinga!

Suala la kuchaguliwa au kutochaguliwa sio msingi wa hoja!Sasa mmeweka utaratibu wa atakyeshinda urais atapigiwa kura ya Ndiyo a u Hapana,basi!Hakuna mtu mwingine kuchukua fomu!

Kofia hizi mbili si afya kabisa kwa utawala bora!
 
KARLO MWILAPWA,
Mkuu,think tank ya CCM ilikaa 2015 na kuja na ilani ambapo ilitamka mtoto wa kike atakayepata ujauzito atapewa fursa ya kuendelea na masomo atakapojifungua! Magufuli amebatilisha hilo kwa amri yake mwenyewe,hata mama Samia Suluhu alikuwa hajui!

Ndio maana kwenye mkutano mmoja mama samia suluhu akasema juu ya watoto wanaopata mimba kuendelea na masomo,baada ya siku moja JPM akatoa tamko kuwa kwenye utawala wake hakuna kitu kama hicho!

Sasa ukirudi kwenye chama,yeye ndiye mwenyekiti!Ni nani wa kumueleza kuwa tulikaa tukakubaliana hiki,kwanini umeenda kinyume? Yaani JPM kawaona watunga ilani ni wajinga!

Suala la kuchaguliwa au kutochaguliwa sio msingi wa hoja!Sasa mmeweka utaratibu wa atakyeshinda urais atapigiwa kura ya Ndiyo a u Hapana,basi!Hakuna mtu mwingine kuchukua fomu!

Kofia hizi mbili si afya kabisa kwa utawala bora!
Well said GT.
Vp Stiglaz GEJI na Standadi GOJI ilani ilisemaje!!!???
 
Nafasi zote alizonazo Rais Magufuli, uenyekiti na urais ni za kuchaguliwa hivyo huwezi kupiga marufuku na hii itaonesha wazi kabisa mna kusudi jingine.

Labda uko upinzani sijui kukoje lakini CCM jambo lolote hata dogo kiasi gani linapitia kwenye vikao na kupatiwa baraka za vikao. Hata Serikali Kuna utaratibu wa vikao pia.

Nafasi ya uenyekiti na urais zote ni za kimamlaka hivyo wote waliopo chini ya hizo nafasi waheshimiwe. Kwenye vikao vya CHADEMA , Mbowe akikohoa tu wengine wanahofu( ni utani tu nimechomekea). Unaposema CCM ni ndio mzee tu unapotosha, kama kanuni na taratibu zinaruhusu kutoa maoni watatoa na wanatoa.

Uongo mtupu hapo kwenye red, maamuzi ya kukataza shughuli za kisiasa yalipitishwa na kikao gani cha ccm? Maamuzi ya kuwawinda na kuwaua wapinzani wa kisiasa yalipitishwa na kikao gani cha ccm? Mbona hamjamwambia Magufuli lolote kuhusu Makonda ambaye amekuwa doa kubwa kwa nchi mpaka anawekewa vikwazo?
 
Mtoa mada unahoja ya msingi. Ni muhimu kutenganisha kofia raisi na m.kiti wa chama. Nadhani katiba ya Warioba walipendekeza hili.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndio mkuu,dhana ya chama kusimamia serikali inatoka wapi kama Rais ndiye mwenyekiti?Wajumbe kamati kuu unakuta ni mwenyekiti ambaye ni Rais,Rais Zanzibar,Makamu wa Rais,Waziri Mkuu NK!Hapo wanajisimamia au wanasimamiwa!
 
CCM wamerithi mifumo dhaifu ya hofu ya madaraka. Baba wa taifa alibariki mfumo huo kwa hoja za msingi zama zile.Taifa lilikuwa la kijamaa na palikuwa na tishio dhahiri mabepari kutumia mwanya wowote .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CCM wamerithi mifumo dhaifu ya hofu ya madaraka. Baba wa taifa alibariki mfumo huo kwa hoja za msingi zama zile.Taifa lilikuwa la kijamaa na palikuwa na tishio dhahiri mabepari kutumia mwanya wowote .

Sent using Jamii Forums mobile app
Kabisa,na wanatumia mfumo huo kuhodhi madaraka!Kama wanataka kumuenzi Nyerere basi wapunguze madaraka waliyopewa kikatiba maana Nyerere alitahadharisha,ni wakati sasa wa kuchukua hatua!
 
Uongo mtupu hapo kwenye red, maamuzi ya kukataza shughuli za kisiasa yalipitishwa na kikao gani cha ccm? Maamuzi ya kuwawinda na kuwaua wapinzani wa kisiasa yalipitishwa na kikao gani cha ccm? Mbona hamjamwambia Magufuli lolote kuhusu Makonda ambaye amekuwa doa kubwa kwa nchi mpaka anawekewa vikwazo?
Hata marufuku ya watoto wakipata ujauzito kutorudi shule limetoka kwake na si kwa chama!Chama hata hakina habari,mtu anajiamulia kwakuwa mwanawe alipata mimba akiwa mwanafunzi na hakumrudisha shule basi afanye kuwa suala la kitaifa,yaani anaendesha nchi kama anavyoendesha familia yake!
 
Back
Top Bottom