Micro E coli
JF-Expert Member
- Oct 31, 2011
- 938
- 192
Upo kwenye ofisi yenye viyoyozi,unatembelea gari la wizara, hujui manesi tunavyozalisha bila kuvaa gloves mikononi huku tukimwagikiwa na amniotic fluid na damu usoni. Hujuhi tunavyotumia mwanga wa Nokia kuzalisha huku vichanga vikitufia mikononi kwa ukosefu wa vifaa kupumulisha vichanga hivyo. Hufahamu kabisa jinsi ndugu na jamaa za wagonjwa wanavyotumwagia mvua za matusi kwa kushindwa kuwahudumia wagonjwa wao kisa dawa na vifaa hamna.
Nikukumbushe ulivyokuja Mwanza pale ukumbi wa Gandhi, unakumbuka wauguzi walivyokwambia: Tulikwambia hatuijuhi TANA hata kirefu chake, tulikwambia tunavyokatwa hela hiyo NGO yenu kwa lazima tena ada hizo huunganishwa na malipo ya leseni kwa kulazimishwa,sasa BOSI hao wauguzi unaowahimiza wasigome ni wa hapo Dar-es-salaam au?
Unakumbuka tulivyokuuliza uhalali wa sisi kulipia leseni sh. 50,000 huku kada zingine za afya hawalipi chochote na ukatujibu kwa kiburi hasa huyo raisi wa TANA (luteni kanali wa jeshi) huyo jama mwenye mikogo mingi, kiburi,mjivuni,eti ana master ya Uuguzi kutoka UK,kuwa na master ndio kuwa mwizi? Ndiyo wewe ni mwizi, kuna mpango umeuanzisha unataka wauguzi wakatwe ada ya TANA moja kwa moja kwenye mishahara kupitia hazina. Hiyo janja yako tumeshaijua,na ndio sababu mnahimiza wauguzi wasishiriki kwenye mgomo. Umelewa madaraka wewe,kwa akili zenu tana mnadhani bila daktari 'ku-prescribe'muuguzi wa Tanganyika anaweza kufanya lolote? Hata nursing care za kawaida tunaandikiwa tu!
Mwisho wauguzi wote wa Tanzania pamoja na kutojiamini kwetu,pamoja na shida zetu,tusikubali wanyonyaji TANA watwambie la kufanya, kama ni kugoma au kutogoma uamuzi tunao sisi,wanaovaa disposable gloves kuzalishia huku zinatutobokea ni sisi,TANA kazi yao kutembeza bakuli kwa wafadhiri kuomba fedha za kutembelea 'matawi' yao!
Afisa Utumishi mkuu wa jiji la Mwanza,Katibu wa Afya wa jiji ipo siku mawe na miti vitaongea juu yao!...wewe rais wa Tana uliye na degree ya UK ulikuja Mwanza tukakueleza shida zetu ukasema utapeleka kwa wahusika,kwenye kikao kikubwa kilichofanyika Singida ukatupa mrejesho kwamba wizara imetuahid kutatua matatizo yetu hukusema ni lini watatatua shida hizo,kwa uelewa wako huo mbovu na kutuburuza sisi wauguzi unaona ni sawa kwa sababu wewe uko kwenye kimvuli na familia yako,wauguzi tukae natukatae hiyo Tana kwan haina msaada kwetu,uoga wetu unatupeleka sehemu mbaya,toka lini mtwana akamsaliti bwana?
Huyo Rais wa Tana yuko wizarani hivyo lazima aseme pumba kupalilia ajira yake,wauguzi tukimwage hicho chama cha Tana tutengeneze chama chetu ambacho kinajitegemea,na pia tung'ang'ane tuwe na utawala wetu wenyewe sio kila kitu tupite kwa daktari mkuu.
Mwanza wauguzi wa jiji tuna shida hadi tunatamani kuachana hii kazi, watawala hawatutendei haki hata tone,huyu afsa utumishi mkuu Mungu atamlaani kwa kutunyanyasa wauguzi,tumejikunyata kwa uoga wetu na pia hatuoni chama gani cha kututetea, bora tujiunge na chama cha wafanyabiashara wa mboga mboga kwa sababu tutapata lishe bora, na kujiongezea kipato kidogo kwa hiyo biashara nakusahau maswala ya hawa wajinga waliojichagua kutoka wizaran, huyu Rais ni mwanajesh hivyo kila kitu anapata kwa nafuu hata akili yake imedumaa tu, wauguzi mnafikiri atafanya nini kwa maslahi yetu?
Wauguzi tushikamane tutetee haki zetu, namalizia kwa kusema TANA kufa kabisa.
Froida unaongea mpka povu linakutoka mdomoni.
Kazi hiyo kama inawaboa jiungeni na sisi wa mitaani katika shughuli zisizo rasmi na biashara.
Leo tunalipa kodi kibao watu hawafanyi kazi,huduma hatupati na hata ukipata ndo kama unafanyiwa favor.
Tijue moja ,hospitali zote ziuzwe ili hii huduma isituumize walipa kodi.
Upo kwenye ofisi yenye viyoyozi,unatembelea gari la wizara, hujui manesi tunavyozalisha bila kuvaa gloves mikononi huku tukimwagikiwa na amniotic fluid na damu usoni. Hujuhi tunavyotumia mwanga wa Nokia kuzalisha huku vichanga vikitufia mikononi kwa ukosefu wa vifaa kupumulisha vichanga hivyo. Hufahamu kabisa jinsi ndugu na jamaa za wagonjwa wanavyotumwagia mvua za matusi kwa kushindwa kuwahudumia wagonjwa wao kisa dawa na vifaa hamna.
Nikukumbushe ulivyokuja Mwanza pale ukumbi wa Gandhi, unakumbuka wauguzi walivyokwambia: Tulikwambia hatuijuhi TANA hata kirefu chake, tulikwambia tunavyokatwa hela hiyo NGO yenu kwa lazima tena ada hizo huunganishwa na malipo ya leseni kwa kulazimishwa,sasa BOSI hao wauguzi unaowahimiza wasigome ni wa hapo Dar-es-salaam au?
Unakumbuka tulivyokuuliza uhalali wa sisi kulipia leseni sh. 50,000 huku kada zingine za afya hawalipi chochote na ukatujibu kwa kiburi hasa huyo raisi wa TANA (luteni kanali wa jeshi) huyo jama mwenye mikogo mingi, kiburi,mjivuni,eti ana master ya Uuguzi kutoka UK,kuwa na master ndio kuwa mwizi? Ndiyo wewe ni mwizi, kuna mpango umeuanzisha unataka wauguzi wakatwe ada ya TANA moja kwa moja kwenye mishahara kupitia hazina. Hiyo janja yako tumeshaijua,na ndio sababu mnahimiza wauguzi wasishiriki kwenye mgomo. Umelewa madaraka wewe,kwa akili zenu tana mnadhani bila daktari 'ku-prescribe'muuguzi wa Tanganyika anaweza kufanya lolote? Hata nursing care za kawaida tunaandikiwa tu!
Mwisho wauguzi wote wa Tanzania pamoja na kutojiamini kwetu,pamoja na shida zetu,tusikubali wanyonyaji TANA watwambie la kufanya, kama ni kugoma au kutogoma uamuzi tunao sisi,wanaovaa disposable gloves kuzalishia huku zinatutobokea ni sisi,TANA kazi yao kutembeza bakuli kwa wafadhiri kuomba fedha za kutembelea 'matawi' yao!
Haswa natokwa na mapovu kwa kuwa na watu wajinga kama hao waliojipachika vyeo kujiita viongozi wa TANA wanadharilisha taaluma ya UUGUzi soma hii definition ya Nursing AbFroida unaongea mpka povu linakutoka mdomoni.
Kazi hiyo kama inawaboa jiungeni na sisi wa mitaani katika shughuli zisizo rasmi na biashara.
Leo tunalipa kodi kibao watu hawafanyi kazi,huduma hatupati na hata ukipata ndo kama unafanyiwa favor.
Tijue moja ,hospitali zote ziuzwe ili hii huduma isituumize walipa kodi.
|
Ha ha ha!Huku kimekuleta nini,usingefeli form two mtaani ungekuwa unafanya nini! Kampeni 2015 bado, subiri utapata tisheti ya njano na kofia ya kijani. Unaogea usaha,