Lord OSAGYEFO
JF-Expert Member
- Feb 19, 2021
- 3,086
- 4,881
Wadau nawasalimu,
Nichukue nafasi hii kuwaomba viongozi wetu wa dini kutumia busara na hekima zao walizojaliwa na Mungu kuwakusanya Marais wote wastaafu bara na visiwani,Makamu wa Rais wote wa bara na visiwani,Mawaziri Wakuu Wastaafu, Maspika Wastaafu, Majaji Wastaafu na watu mashuhuri na viongozi wa dini zote ili kufanya upatanishi kwa wanasiasa wetu kwa maana ya ccm na upinzani.
Kutokana na matukio ya kutisha ya kisiasa yaliyoanza kujitokeza na kushamiri toka utawala wa awamu ya 5 chini ya Hayati Magufuli.
Hakuna mtanzania asiyejua nini kimetokea na nini kinaendelea kutokea.Matukio ya watu kupigwa risasi,kutekwa kupotea kubambikiziwa kesi za ugaidi na uhujumu uchumi wapinzani wamejaa magerezani kwa kesi za kutengenezwa.
Ni wakati sahihi kwa viongozi wa dini kusimamia maridhiano hayo kam a viongozi wa dini wa nchi nyingine wanavyofanya.
Chonde chonde viongozi wetu hakika Mungu atawabariki ktk kufanya upatanishi
Nichukue nafasi hii kuwaomba viongozi wetu wa dini kutumia busara na hekima zao walizojaliwa na Mungu kuwakusanya Marais wote wastaafu bara na visiwani,Makamu wa Rais wote wa bara na visiwani,Mawaziri Wakuu Wastaafu, Maspika Wastaafu, Majaji Wastaafu na watu mashuhuri na viongozi wa dini zote ili kufanya upatanishi kwa wanasiasa wetu kwa maana ya ccm na upinzani.
Kutokana na matukio ya kutisha ya kisiasa yaliyoanza kujitokeza na kushamiri toka utawala wa awamu ya 5 chini ya Hayati Magufuli.
Hakuna mtanzania asiyejua nini kimetokea na nini kinaendelea kutokea.Matukio ya watu kupigwa risasi,kutekwa kupotea kubambikiziwa kesi za ugaidi na uhujumu uchumi wapinzani wamejaa magerezani kwa kesi za kutengenezwa.
Ni wakati sahihi kwa viongozi wa dini kusimamia maridhiano hayo kam a viongozi wa dini wa nchi nyingine wanavyofanya.
Chonde chonde viongozi wetu hakika Mungu atawabariki ktk kufanya upatanishi