Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,559
- 41,071
Nchi yetu ipo kwenye mkorogano wa ajabu kwa sababu ya kuwa na viongozi wasioelewa chochote kuhusiana na sheria na katiba. Uduni huu wa viongozi kukosa kuelewa sheria, na wakati fulani hulka ya unafiki, vimewafanya baadhi ya viongozi kuropoka vitu vya ajabu na hata kuingia kusaini na kuridhia mikataba ya hovyo, kama huu wa bandari.
Rais anapowateua wasaidizi ni muhimu kuwateua watu wenye weledi wa kutosha, watu walio wakweli na siyo wanafiki ambao uwezo wao unaishia kwenye kuimba nyimbo za kumsifia tu Rais, hata pale anapokosea. Masiha Kristo aliwahi kunena kuwa, kipofu hawezi kumwongoza kipofu mwenzie la sivyo wote watatumbukia shimoni. Rais siyo mtaalam wa sheria, anamteua Waziri ambaye hana uelewa wala hajishughulishi kuzijua sheria, kuwa waziri wa Mambo ya Ndani ili akasimamie sheria, atafanya nini la maana zaidi ya kuropoka na kuwaagiza polisi wakafanye mambo yaliyo kinyume cha sheria? Kuwa waziri siyo lazima kuwa mwanasheria lakini mtu akishateuliwa kuwa Waziri au katibu mkuu, ni muhimu kwake kuzitambua sheria na vifungu vya katiba vinavyoongoza Wizara anayoiongoza. Maana huwezi ukawa unaapa kulinda kitu ambacho hata hukijui. Utaapaje kuwa utalinda katiba wakati hata katiba yenyewe huijui?
Waziri anathubutu kusema kuwa eti viongozi wa dini sheria haiwaruhusu kushiriki siasa, halafu haitaji hata hiyo sheria, ni sheria gani! Huu ni uropokaji wa kiongozi wa Serikali asiyejua chochote.
Hakuna sheria yoyote, inayomzuia kiongozi yeyote wa dini kushiriki au kufanya shughuli za siasa. Haipo sheria hiyo. Katiba yetu inatamka wazi kuwa mtanzania yeyote anao uhuru wa kushiriki shughuli za siasa, ikiwa ni pamoja na kuomba kuchaguliwa kuwa kiongozi na kuchagua kiongozi. Ndiyo maana, tangu zamani, kuna viongozi wa dini, kama Askofu Mwamasika alikuwa mbunge wa Iringa miaka ya 1970, marehemu Askofu Rwakatare alikuwa mbunge wa kuteuliwa, na sasa Askofu Gwajima ni mbunge wa Kawe, na wengine wengi. Hao wote ni viongozi wa dini na ni viongozi wa kisiasa. Ni Kanisa Katoliki pekee ndiyo linalowazuia viongozi wake wa dini kugombea uongozi wa kisiasa wakiwa bado ni viongozi wa kanisa, lakini siyo zuio la kikatiba au sheria yoyote.
Kinachokatazwa ni kiongozi wa dini kutumia jukwaa la dini kufanya siasa, siyo kiongozi wa dini kufanya shughuli za kisiasa.
Jambo la pili, kupinga uovu kama vile wizi, uporaji, uonevu na upendeleo, rushwa, ufisadi, hila na hadaa, siyo siasa bali ni suala la kimaadili na kiimani; sawa na ilivyo kutetea haki za watu. Haya yanaweza kufanywa kwenye nyumba za ibada, majukwaa ya kijamii na hata kwenye majukwaa ya siasa.
Tunaomba Rais Samia, mkanye kwa nguvu Waziri Masauni, asitoe maneno ya uwongo kuwatisha viongozi wa dini. Yeye Masauni, kwa kuwazuia viongozi wa dini wasishiriki shughuli za kisiasa mahali popote na kwa mazingira yoyote, anakiuka katiba ya JMT. Kutokana na kosa hilo, Masauni anastahili kufukuzwa kutoka kwenye nafasi ya uwaziri kwa sababu anafanya kinyume na kiapo chake cha kulinda katiba.
Rais anapowateua wasaidizi ni muhimu kuwateua watu wenye weledi wa kutosha, watu walio wakweli na siyo wanafiki ambao uwezo wao unaishia kwenye kuimba nyimbo za kumsifia tu Rais, hata pale anapokosea. Masiha Kristo aliwahi kunena kuwa, kipofu hawezi kumwongoza kipofu mwenzie la sivyo wote watatumbukia shimoni. Rais siyo mtaalam wa sheria, anamteua Waziri ambaye hana uelewa wala hajishughulishi kuzijua sheria, kuwa waziri wa Mambo ya Ndani ili akasimamie sheria, atafanya nini la maana zaidi ya kuropoka na kuwaagiza polisi wakafanye mambo yaliyo kinyume cha sheria? Kuwa waziri siyo lazima kuwa mwanasheria lakini mtu akishateuliwa kuwa Waziri au katibu mkuu, ni muhimu kwake kuzitambua sheria na vifungu vya katiba vinavyoongoza Wizara anayoiongoza. Maana huwezi ukawa unaapa kulinda kitu ambacho hata hukijui. Utaapaje kuwa utalinda katiba wakati hata katiba yenyewe huijui?
Waziri anathubutu kusema kuwa eti viongozi wa dini sheria haiwaruhusu kushiriki siasa, halafu haitaji hata hiyo sheria, ni sheria gani! Huu ni uropokaji wa kiongozi wa Serikali asiyejua chochote.
Hakuna sheria yoyote, inayomzuia kiongozi yeyote wa dini kushiriki au kufanya shughuli za siasa. Haipo sheria hiyo. Katiba yetu inatamka wazi kuwa mtanzania yeyote anao uhuru wa kushiriki shughuli za siasa, ikiwa ni pamoja na kuomba kuchaguliwa kuwa kiongozi na kuchagua kiongozi. Ndiyo maana, tangu zamani, kuna viongozi wa dini, kama Askofu Mwamasika alikuwa mbunge wa Iringa miaka ya 1970, marehemu Askofu Rwakatare alikuwa mbunge wa kuteuliwa, na sasa Askofu Gwajima ni mbunge wa Kawe, na wengine wengi. Hao wote ni viongozi wa dini na ni viongozi wa kisiasa. Ni Kanisa Katoliki pekee ndiyo linalowazuia viongozi wake wa dini kugombea uongozi wa kisiasa wakiwa bado ni viongozi wa kanisa, lakini siyo zuio la kikatiba au sheria yoyote.
Kinachokatazwa ni kiongozi wa dini kutumia jukwaa la dini kufanya siasa, siyo kiongozi wa dini kufanya shughuli za kisiasa.
Jambo la pili, kupinga uovu kama vile wizi, uporaji, uonevu na upendeleo, rushwa, ufisadi, hila na hadaa, siyo siasa bali ni suala la kimaadili na kiimani; sawa na ilivyo kutetea haki za watu. Haya yanaweza kufanywa kwenye nyumba za ibada, majukwaa ya kijamii na hata kwenye majukwaa ya siasa.
Tunaomba Rais Samia, mkanye kwa nguvu Waziri Masauni, asitoe maneno ya uwongo kuwatisha viongozi wa dini. Yeye Masauni, kwa kuwazuia viongozi wa dini wasishiriki shughuli za kisiasa mahali popote na kwa mazingira yoyote, anakiuka katiba ya JMT. Kutokana na kosa hilo, Masauni anastahili kufukuzwa kutoka kwenye nafasi ya uwaziri kwa sababu anafanya kinyume na kiapo chake cha kulinda katiba.