Uloi nga mâché68
JF-Expert Member
- Dec 30, 2013
- 486
- 153
Baada ya kufanya maamuzi mabovu yaliyosababisha kushindwa vibaya Uchaguzi wa Rais, ni Wakati sasa wa Viongozi wa UKAWA kujiuzulu kwa kuwa uteuzi wenu wa Mgombea asiye na sifa ndio umesababisha haya yote.
Kwa kutufanya mazuzu, mlianza kutengeneza mazingira ya kutuaminisha kwamba kura zitaibiwa na kutuagiza tulinde kura hali mkijua kwamba mita 200 tusingeweza kuona lolote hata kama kungekuwa na wizi huo! Pia mkadai kura zinazotangazwa na Tume sio za kweli bila kutuonesha hizo mnazodai ni halali na zikiwa zimesainiwa na Mawakala halali.
Hilo nalo ni changa la macho. Ni busara tu kwamba mnapaswa kukubali kwamba mlijitengenezea wenyewe mazingira ya kushindwa kwa kuacha mbachao kwa msala upitao.
Leo tena mnajifanya kususia sherehe za kuapishwa kwa Rais mpya Magufuli badala ya ninyi kujiuzulu. Juzi mkatuagiza tuandamane tukakataa mpaka mtakapotangulia mbele ya maandamano tupigwe wote. Si mlituambia mmebadili gia angani?
Acheni danganya toto na msipoteze muda wetu JIUZULUNI HARAKA!
Kwa kutufanya mazuzu, mlianza kutengeneza mazingira ya kutuaminisha kwamba kura zitaibiwa na kutuagiza tulinde kura hali mkijua kwamba mita 200 tusingeweza kuona lolote hata kama kungekuwa na wizi huo! Pia mkadai kura zinazotangazwa na Tume sio za kweli bila kutuonesha hizo mnazodai ni halali na zikiwa zimesainiwa na Mawakala halali.
Hilo nalo ni changa la macho. Ni busara tu kwamba mnapaswa kukubali kwamba mlijitengenezea wenyewe mazingira ya kushindwa kwa kuacha mbachao kwa msala upitao.
Leo tena mnajifanya kususia sherehe za kuapishwa kwa Rais mpya Magufuli badala ya ninyi kujiuzulu. Juzi mkatuagiza tuandamane tukakataa mpaka mtakapotangulia mbele ya maandamano tupigwe wote. Si mlituambia mmebadili gia angani?
Acheni danganya toto na msipoteze muda wetu JIUZULUNI HARAKA!