Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,800
- 71,222
Taifa lolote linahitaji viongozi bora na wagumu wawezao kuongoza wakati nchi imetulia lakini pia muhimu kama wakati mgumu kama Vita, Njaa, na Maafa mbalimbali.
Sasa tuna kundi kubwa la mawaziri vijana ambao hata kwa hulka zao za nje wanaonyesha hawana uimara huo.
Ona nchi iko kwenye amani kabisa lakini mambo mengi yanawashinda ila wawezalo ni kusimama majukwaani na sifa kwa Rais (tena wakimwita mama), wajibu ambao ni wa viongozi wa chama sio wao.
Yaani hakuna tofauti ya chawa na waziri mpaka unajiuliza ndani ya Baraza la mawaziri (BLM) kweli kunaweza kuwa na mjadala mkali pengine hata kufikia wengine kutishia kujiuzulu kama jambo linaamriwa na haliko sawa au mambo ni kama kwenye bunge hili la sasa?
Kweli tupate vita kama Ukraine ya kuvamiwa na jirani na kucharazwa hasa, hawa wanaweza kutengeneza mikakati bora ya serikali kuendeleza yanayoipasa?
Kwenye hili la hawa vijana mawaziri tuseme wazi tume feli ila tumepata timu bora ya Praise & worship
Tazama tuu hiyo picha, wenye kujua Alama za picha wamepata jibu.
Sasa tuna kundi kubwa la mawaziri vijana ambao hata kwa hulka zao za nje wanaonyesha hawana uimara huo.
Ona nchi iko kwenye amani kabisa lakini mambo mengi yanawashinda ila wawezalo ni kusimama majukwaani na sifa kwa Rais (tena wakimwita mama), wajibu ambao ni wa viongozi wa chama sio wao.
Yaani hakuna tofauti ya chawa na waziri mpaka unajiuliza ndani ya Baraza la mawaziri (BLM) kweli kunaweza kuwa na mjadala mkali pengine hata kufikia wengine kutishia kujiuzulu kama jambo linaamriwa na haliko sawa au mambo ni kama kwenye bunge hili la sasa?
Kweli tupate vita kama Ukraine ya kuvamiwa na jirani na kucharazwa hasa, hawa wanaweza kutengeneza mikakati bora ya serikali kuendeleza yanayoipasa?
Kwenye hili la hawa vijana mawaziri tuseme wazi tume feli ila tumepata timu bora ya Praise & worship
Tazama tuu hiyo picha, wenye kujua Alama za picha wamepata jibu.