Pamoja na changamoto kubwa za kimazingira zinazotukabili katika kuijenga CHADEMA mkoa wa Singida, wamekuwapo baadhi ya viongozi ambao wamekuwa mzigo mzito na kwa namna moja au nyingine wanatukwamisha. Hao ni pamoja na aliyekuwa mgombea wa ubunge kwa tiketi ya CHADEMA jimbo la singida mjini, Josephat Isango na anayekaimu nafasi ya Katibu wa BAVICHA kwa sasa, Timothy Peter Thomas. Viongozi hawa mara nyingi wamekuwa wakikataa kushirikiana na wengine , wakiwemo viongozi wa BAVICHA mkoa wakijidai kuendeleza sera ya usomi ndani ya CHADEMA. Mathalani, wote wawili wamekataa kushiriki mikutano iliyoandaliwa na chama mwishoni mwa mwaka jana na mwanzoni mwa mwaka huu na ile iliyoandaliwa mapema na mjumbe wa kamati kuu, Dr. Kitila Kikumbo. Pia, wamekuwa na uhasama kwa muda mrefu hadi kufikia hatua ya kutishiana maisha wao kwa wao, uhasama ambao wengi tunauhusisha na mbio za kuwania ubunge waka 2015 kwani wote wanaonekana wanautaka. Wote waliamua kukwamisha kwa makusudi kabisa mashindano ya BAVICHA wilaya ya Singida mjini mwishoni mwa mwaka jana, mashindano ambayo yaliandaliwa na mwenyekiti wa chama wilaya ya singida nddugu Kumalija. Josephat Isango, ambaye alivuliwa uenyekiti wa BAVICHA kutokana na kuwa na umri wa zaidi ya miaka 40 na baada ya kukmbwa na kashfa ya matumizi mabaya ya fedha za chama ameendelea kungangania uongozi na amekuwa akitoa matamko kwa niaba ya viongozi tulioko Singida akidanganya ameyatoa makao makuu ya chama. Timothy Peter Thomas naye, ambaye bado hajakomaa katika siasa za mikikimikiki anasemekana aliilazimisha kamati tendaji ya wilaya ili impe nafasi ya BAVICHA wakati mara nyingi yuko chuoni Dar es salaam na mwaka jana aligombana na Katibu wa wilaya, Yahaya Ramadhani baada ya kukaimu kwa nguvu nafasi ya katibu wa wilaya. Wote wawili pia wamekuwa wakitoa lugha mbaya kwa baadhi ya viongozi wa CHADEMA mkoani hapa akiwemo Katibu wa wilaya, Yahaya Ramadhani. Ndugu Yahaya ameyathibitisha yote haya katika mazungumzo niliyofanya nae wiki iliyopita tukiwa ofisini, Singida.
CHANZO : MIMI MWENYEWE
Nimesoma tuhuma zote, Mimi nipo, nafikika, tuhuma hizo kama zipo watasema viongozi wa Chama, ila ID hii imetengenezwa juzi, kwa lengo ambalo nimeanza kulifahamu, viongozi wa Chama Mkoani wanajua kuhusu hii ID, wao wanapatikana, wanafikika. Kwa kuwa umeleta kama tuhuma, na najua taratibu za Chama. Weka kwa maandishi peleka kwenye Chama kichukue hatua, Chama hakitaki Ujinga sasa kinataka kuchukua dola. Halafu unapoleta tuhuma weka jina, kuna watu wanadiriki kuweka hadi namba za simu lengo ni kuwa tuwajibishane ili nchi ikombolewe. Unapokuja kwenye mtandao na kuficha ID yako halafu unaileta katika mtazamo huu inabaki ya kishabiki zaidi.