Viongozi CUF waendelea kulia na CHADEMA

kipuyo

JF-Expert Member
Jul 30, 2009
1,785
1,465
Makamu wa kwanza wa Rais wa serikali ya Umoja wa kitaifa wa Zanzibar Maalim Seif,Habib Mnyaa na Diwani wa Kibaga kwa tiketi ya CUF Bwana Juma Mkumbi wametumia muda mwingi sana kuituhumu chadema kwa ubinafsi,udini na ukanda wakati walipokuwa wanawahutubia wananchi wa Singida mjini katika eneo la stand ya zamani.

Habib Mnyaa anasema kuwa CHADEMA wameshindwa kushirikiana na vyama vingine bungeni kwa kuwa chadema ni wabinafsi na wanawaonea wivu cuf kwa kuwa wapo kwenye serikali.

Aliendelea kuituhumu chadema kwa kusema kuwa walishasema kuwa nchi haitatawalika hivyo haya matukio yanayotokea hivi sasa ni matokeo ya kauli tata za chadema.Bwana Mnyaa alihoji pia uhalali wa wabunge wa chadema kutumia quatation za biblia ndani ya bunge wakati hapo zamani biblia na msahafu zilikuwa zinaingizwa bungeni wakati wa kiapo tu!

Naye Maalim Seif pamoja na kulaani yaliyotokea jana huko Arusha na kuelezea faida zilizopatikana kutokana na serikali ya umoja wa kitaifa pia alionekana kupiga vijembe kwa chadema pale aliposema "kwa sasa imedhihiri chama cha kisiasa ni kipi na chama cha kidini ni kipi"
Kabla ya Hotuba za viongozi wakuu hao wa CUF Diwani wa Kibaga aliwaambia wananchi kuwa ichagueni CUF kwa kuwa mtapatiwa ubwabwa wa uhakika kama walivyofanyiwa watu wa Kibaga walipoichagua CUF.

Alisema kuwa watu wa Kibaga walikula ubwabwa kwa siku tatu fullizo.

Pia Diwani huyo ambaye ni mzaliwa wa Singida alisema kuwa amewachangia wazee wa Ikungi magunia kumi ya mahindi maana mbunge wao amekuwa wa miongozo na vurugu bungeni badala ya kuwasaidia watu waliompeleka bungeni.

My take: CUF haina tena mvuto huku bara na hata watu waliohudhuria mkutano huo hawakuwa wengi sana.

 
Hivi CUF bado kipo? Mtaani kwetu ukizungumzia CUF ni kama simulizi ya zamani, ambayo wahusika wamepotea njia na hawajui watapumzika wapi.
 
Hivi CUF bado kipo? Mtaani kwetu ukizungumzia CUF ni kama simulizi ya zamani, ambayo wahusika wamepotea njia na hawajui watapumzika wapi.
Ajabu, injili ya CUF inahubiriwa na watu wa visiwani huku bara. Hivi huku hawana viongozi?
 
Cuf ina watoto Wa mjini twende wapi nyie wachaga na Cdm yenu nendeni kilimanjaro cuf haiwezi cuf imeshikwa na watoto Wa mjini Ndio mana kila misukosuko ikipata chama kipo vilevile nyie Zito anawagalagaza mfukuzeni muone vipande
 
Utamu wa fungate naona sasa unaelekea mwisho. Ngoja niwape TIPS: Cuf wameagizwa makusudi ili kuichafua CHADEMA. Lakin hawatafanikiwa ng'OO
 
Ajabu, injili ya CUF inahubiriwa na watu wa visiwani huku bara. Hivi huku hawana viongozi?

Cuf imekaa kitaifa zaidi katibu Mkuu anatoka visiwani mwenyekiti bara Ndio mana Lipumba akienda zenji anafanya mkutano Seif akija bara anafanya nyinyi slaa katibu anatoka bara Mbowe bara mmewazarau chadema Wa Zanzibar Hamna uwiano
 
na cha ajabu katibu mkuu wa cuf amepandishwa jukwaani na mkuu wa wilaya y Singida mjini.
hapo inadhihirisha kuwa lao ni 1 ccm na cuf.
wamelenga zaidi kuichafua CDM.
 
.Pia Diwani huyo ambaye ni mzaliwa wa Singida alisema kuwa amewachangia wazee wa Ikungi magunia kumi ya mahindi maana mbunge wao amekuwa wa miongozo na vurugu bungeni badala ya kuwasaidia watu waliompeleka

Umesomeka diwani, waeleze pia mbunge yupo busy na kutetea magaidi nchini badala ya kusaidia wapiga kura wake
 
CUF WHO?.....HAWA JAMAA ndio adui namba 1 wa demokrasia na upinzani hapa tanzania afanzali CCM kuliko hawa jamaa,sababu hawatabiriki.wote tunajua CCM wanatabirika.ila hawa jamaa ,ila kwa wapinzani wa kweli TZ we need to stay very far from CUF.....HAWANA NIA NZURI
 
eti wamesema ni pekee waliowza kuiendesha kambi rasimi ya upinzani bngeni kiufasaa.
eti CDM wao ni wa fujo tuu.
 
Mbona CUF wanarudia nyimbo zile zile anazoimba HUSBAND WAKE wa pale Lumumba, wambieni watulie kwenye ndoa, ushirikiano na mnafiki wa nini?
 
Wanatafuta nini bara wakati hawataki muungano? Mchambawima hakukaliki au?

Kwani Chadema inautaka huo Muungano?
Hukumbuki kauli ya Mbowe kuwa hawana Shida na 'vikura' vya Zanzibar Mil 1 wakati Dar es Salaam inaizidi mara 4.
 
ALLAH AKHBAR!TANZANIA YETU TWAIZAMISHA WENYEWE,Yaani kweli leo hii CUF washasahau tulivyoumia mioyoni mwetu walipopakaziwa ni chama cha kidini???Ama kweli walikata tamaa na kuamini hawaiwezi tena ccm hivyo kwayo waliona ni bora kuungana nayo pamoja na madhila yote yatukumbayo kutokana na ccm."UKOMBOZI WA MTANZANIA MNYONGE UWAPI BASI PALE TUNAPOAMUA KUSHIRIKI MEZA MOJA NA MNYONYAJI CCM"???
 
Back
Top Bottom