Viongozi 22 wa kitaifa CHADEMA kuzindua kampeni kanda ya Kaskazini

Chadema kama Institution inahitaji kujifanyia Self Assessment maana kwa sasa inaonekana kuwa Chama ni viongozi hao wachache walio karibu na Mwenyekiti. Pasipo kuziba makovu ya uchaguzi wa ndani wa chama chenu, Mbowe na timu yake wasijidanganye kuwa kutakua na kusonga mbele. Watabakia viongozi wa majukwaani na matamko kama wanavyoambiwa. Hivi kwa nini baadhi ya hizo resources zisitumike kufanya mikutano ya hadhara ya kujitathmini? wako wapi wale maelfu ya vijana waliokua wanasukuma magari ya viongozi wakati wa kampeni ya kumnadi mgombea wao? Hivi ni kweli hawana kitu wala hisia yoyote kwa wakati huu? Kwa nini Mbowe na kundi lake hawaigi hata machache yanayofanywa na wapinzani wao? Tumeona Mwenyekiti wa CCM akiongea kwenye mkutano wao mkuu juu ya mabovu ya chama chao na kutangaza wazi kuwa vyeo kama vya Makamanda wa Vijana ( ambao ni wazee wakutupa anyway) na wenyeviti wa wenyeviti ni abomination, pasipo kujali kuwa hao waliovishika wananguvu kiasi gani ndani ya chama chao. The time has come when Mbowe and Chadema wafahamu kuwa kujifunza hakuna mwisho. Leo hii tamko la mikutano mikubwa kwa kugombea udiwani? mbona hao watu waliweza kuteka hizo nafasi pasipo nguvu za the so called the giants. Its just that kwa sisi tunaosoma sana kila habari matangazo ya Chadema ni kama an anti climax. Najua kuna wanaoweza kusema dada anatafuta kick aonekane, si kweli, tuambiane ukweli jamani hata kama sisi ni marafiki, au ndugu ili tupate kuwa bora zaidi kila siku. kwa sasa hivi tutake tusitake Chadema siyo news kwa anybody including Chadema wenyewe maana tunao mtaani na tunawasikia wanavyolalama.

..mikutano ya hadhara si imezuiwa?

..hatuwezi kudai cdm wafanye mikutano ya hadhara wakati hatukuwaunga mkono walipotangaza operation ukuta.

..pia hili tangazo limetolewa na katibu wa cdm kanda ya kaskazini. Ukumbuke cdm imegawanywa kikanda hivyo kila kanda ina uhuru ktk maamuzi na vipaumbele vyake.

..binafsi ningekuunga mkono kama ungewachagiza viongozi wa kanda nyingine nao wajizatiti ktk kampeni hizi zinazokuja.

..vilevile ungependekeza cdm kiwape resources( siyo watu) za kutosha ili kuendesha kampeni za uchaguzi mdogo.

..i dont think it is feasible kwa sasa hivi, ukizingatia ubaguzi dhidi ya wanaotoka kanda ya kaskazini, kupeleka viongozi toka kanda hiyo kwenda kufanya kampeni maeneo mengine ya Tz.

..katika uchaguzi mdogo wa kalenga cdm ilipeleka wapiga kampeni na wasimamizi toka arusha. Matokeo yakw ccm wakaanza kampeni za ubaguzi kwamba cdm haiwaamini wana iringa/kalenga.

..mwisho nakuunga mkono kwamba cdm inahitaji mawazo na mbinu mpya. Vilevile inahitaji ianze sasa hivi kutafuta a viable presidential candidate for 2020.
 
Mmmh tumefkia huku??? Mbeya waliotupa majimbo manne wachagga??? Kilombero huko wachagga??? Buyungu je??? Bukoba??? Dah inasikitisha sana karne ya 21 watu tuna mawazo mfu kma haya

Hao awajielewi anaejielewa awezi kukipa kura chama cha wachaga mafisadi.
 
It's well and good for northerner zone to get first priority on manpower and funds during campaign but when it comes to demonstration, the other zone gets the first priority!

This is CHADEMA's way of doing politics!

Yaani kata nne ambazo ziko kwenye eneo linalojulikana kama ‘’ngome ya CHADEMA’’ zinapewa viongozi 22 wa kitaifa na wabunge wakati wa kampeni. Mwingine anaweza kusema, this is favouritism and misallocation of party resources!

Mimi ninasema, uongozi wa juu wa CHADEMA umefikia kikomo kwa sababu umekosa focus na maarifa ya kukisukuma chama mbele zaidi.[/QUO
and ur CCM anyway
 
Viongozi 22 wa kitaifa wa Chadema wanatarajia kushiriki uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata nne za mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro kuanzia kesho.

Kampeni hizo zitazinduliwa kwenye Kata ya Duni, mjini Babati ambako chama hicho kimemteua Ally Muhidini kugombea udiwani.

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Aman Golugwa amesema watazindua kampeni kwa kila kata ikiongozwa na viongozi wa kitaifa na wabunge.

Golugwa amesema wabunge 22 wa Chadema Kanda ya Kaskazini wamepangwa kusimamia kata hizo na kwamba wanne watakuwa katika kata moja. Pia, madiwani 352 wa chama hicho katika kanda hiyo watashiriki kwenye kampeni.

“Tumejipanga kushinda kata zote, katika uchaguzi uliopita tulishinda kata moja tu kati ya hizi nne,” amesema.

Golugwa amesema uzinduzi wa kampeni kwenye kata nyingine tatu utatangazwa baadaye. Hata hivyo, amesema wameshaanza kampeni za nyumba kwa nyumba ili kuhakikisha Januari 22 wanashinda viti hivyo.

CHANZO: Gazeti la Mwananchi
Waje walete changamoto maana huku CCM imewapumbaza sana watu. ...
 
Hao awajielewi anaejielewa awezi kukipa kura chama cha wachaga mafisadi.
Haahaaaa mkuu ina maana watu 6 million (according to NEC ) wote vichaa?? Hapo kuna wanaotusupport ila hawakupiga kura je inamaanisha almost nusu ya wapiga kura waTZ hawajielewi??? Kwanni mliweka vyama vingi kma mnajua walio nje ya ccm hawajielewi??? Kwanni hamheshim kutofautiana kimawazo na mitazamo??? Sasa mlitaka wamchague nani kma nyie MNAOJIELEWA mmeshindwa kuwatoa katika dimbwi la umaskini kwa miaka 50 ??
 
Yaani mnashangaa Chadema kupeleka nguvu kubwa maeneo wanayokubalika! Mimi nilifikiri mngekishangaa chama kinachoweka wagombea maeneo ambako hakikubaliki. Hivi nyie mnafikiri SISIEM inalala usingizi kuhusu kanda ya Kaskazini? Sasa kama mwenzako halali usingizi akiwaza akunyang'anye ulichonacho halafu wewe mwenye nacho unabweteka eti kwa vile unakubalika! Wengine siasa hamuijui kabisa. Kuna nyakati za kusambaza Chama na kuna nyakati za uchaguzi ambapo nguvu yote lazima iende kwenye eneo la uchaguzi maana hapo ndipo penye ama kupata au kukosa. Halafu watu wanaongelea eti mikutano ya hadhara ya kusambaza chama! Ina maana kuna mtu hajui hata kwamba hiyo mikutano imezuiliwa?
 
Chadema INA viongozi WENGI na wangazi mbali mbali. Ninachosema nikuwa viongozi 22 kuwa sehemu moja si mbaya na sehemu nyingine zitapata viongozi wa kutosha. Nawaomba chadema wasidharau ngazi yoyote ya uchaguzi hasa hizi za chini kwani huwa ndio msingi wa ushindi huku juu, kwahiyo lazima itumike nguvu kubwa kuzichukua hizo nafasi
 
mikakati mibovu halafu utasikia wanalalamikia tume,kun haja gani ya kupiga kampeni''kwenu''unakobalika badala ya kwenda usikokubalika ili uuze sera na ujiwekee akiba ya baadaye ,makosa yaleyale ya kupita na helicopta wakati wengine wakikata mbunga barabarani.
Muulize Hilary Clinton atakwambia madhara ya kujiaminisha unakubalika mahali
 
Back
Top Bottom