Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 40,948
- 74,431
Sakata la makontena bandarini limeonyesha jinsi nchi ilivyokuwa imeoza na kuwa inapoteza fedha nyingi za umma huku nchi ikiwa inakabiliwa na ukosefu wa fedha hivyo kushindwa kuendesha huduma za jamii.
Kuna watu wazito wamepoteza kazi na wengine bado wanashighulikiwa na vyombo vya dola ili sheria ichukue mkondo wake. Lakini habari zilizopo ni kuwa mengi ya makontena hayo yalikuwa yanatolewa kwa vimemo kutoka kwa wakubwa serikalini kwa maana hiyo hao wameshiriki kuhujumu nchi kwa madaraka yao na kusababisha madhara tunayoyaona ya kukosekana kwa huduma nyingi ikiwemo madawa hospitalini iliyopelekea Watanzania wengi kufariki dunia.
Je, ni nani hao waliokuwa wanaandika hivyo vimemo? Waziri mkuu kesha pewa baadhi ya vimemo hivyo, je sasa hivi si ndio wakati muafaka wa kuweka hadharani majina ya wahusika bila kujali vyeo vyao ili tuweze kumuamini yeye na bosi wake Rais Magufuli kuwa wanayofanya sio maigizo bali ni dhamira ya kweli?
Kuna watu wazito wamepoteza kazi na wengine bado wanashighulikiwa na vyombo vya dola ili sheria ichukue mkondo wake. Lakini habari zilizopo ni kuwa mengi ya makontena hayo yalikuwa yanatolewa kwa vimemo kutoka kwa wakubwa serikalini kwa maana hiyo hao wameshiriki kuhujumu nchi kwa madaraka yao na kusababisha madhara tunayoyaona ya kukosekana kwa huduma nyingi ikiwemo madawa hospitalini iliyopelekea Watanzania wengi kufariki dunia.
Je, ni nani hao waliokuwa wanaandika hivyo vimemo? Waziri mkuu kesha pewa baadhi ya vimemo hivyo, je sasa hivi si ndio wakati muafaka wa kuweka hadharani majina ya wahusika bila kujali vyeo vyao ili tuweze kumuamini yeye na bosi wake Rais Magufuli kuwa wanayofanya sio maigizo bali ni dhamira ya kweli?