Asubuhi ya terehe 29 nikaamka salama tayari kwa safari ya kwenda,Singida lakini nilihisi hali ngeni tumboni.
Tumbo lilichafuka nikakimbilia kumeza dawa za kuzuia kuendesha(sio flagil) hatimaye likatulia,nikawasili stendi kukata tiketi ya basi la POLEPOLE likitokea Dar es salaam,gari iliwasili saa saba mchana.
Ilikuwa ni gari chakavu kweli kweli lakini ilikuwa imejaza abiria wa kutosha,vyuma vilijitokea katika baadhi ya siti,nyaya na mikanda ilikuwa mibovu.
Hakika yule dereva alikuwa rafu kweli kweli,mwendo ulikuwa ni mkali aliovertake hovyo akipiga breki hovyo kiasi cha kusumbua mno abiria mara kadhaa alilazimisha magari mengine kusogea pembeni wakati akiovateki angalabu tulikaribia kuumana uso kwa uso na lori la mafuta.
Jirani yangu alikaa dada mmoja mrembo wa haja,hazikupita dakika thelathini akauliza kama nina dakika ili aweze kupiga simu,nikakubali na kumpa simu mara baada ya kumaliza alishukuru na safari ikaendelea.
Tabia ya dada huyu ilinishangaza kidogo,alikuwa anakula kila kituo tunchosimama mara chipsi,mahindi,karanga,juisi,mayai,nyama choma na hata karanga.
Kama ilivyo ada abiria walirundikwa wa kutosha katika varanda na bado waliendelea kupakia na kushusha vituo mbali mbali.
Trafiki waliendelea kupewa elfu tano tano kila walipopiga mkono,hakuna trafiki aliyeingia ndani zaidi ya kumalizana na konda kibingwa.
Hali yangu ilianza kubadilika,kwani tumbo lilizidi kuchafuka ajabu,nilijikaza huku kijasho kikinitoka nikajisemea "niliyokuwa nasikia kwa wengine yananikuta leo"..
Hali ilizidi kuwa mbaya kiasi kwamba uvumilivu ulinifika kikomo,jasho lilinitoka na nilitetemeka kwa mbali nikaona huku ndiko kudhalilika kwenyewe sasa..
Nikamwita konda kumweleza hli yangu akapuuzilia mbali akasema ngoja tufike dodoma,baada ya robo saa hivi nikamweleza kuwa sitoweza tena hivyo wafanye utaratibu wa kuniacha zahanati au stendi,pia niliwaomba wanirudishie nauli nusu..
Waligoma katakata nikaona nitadhalilika kwa sasa nikawambia wanishushe tu,nikashukia Kongwa na kuwahi zahanati...
Baada ya kupewa dawa nikaenda kuripoti polisi juu ya suala la wenye gari kutochukua hatua yoyote kwa abiria aliyeugua,walitoa ushirikiano na nikalala Kongwa kusubiri siku inayofuta.....
Inaendelea.....