Hatimaye saa saba na nusu tuliwasili mbagala,kwa kweli stendi hii ni mbovu kwelikweli ingawaje kuna matumaini ya uboreshaji wake
Saa nane mchana tuliwasili Ubungo na abiria wanaoishia Dar es salaam walishuka,tulikaa zaidi ya dakika 30 wakijazia abiria wa kuelekea Morogoro.
Ingawaje ilikuwa mchana lakini bado foleni ilikuwa ni kubwa ikichagizwa na ujenzi wa barabara kuu ya Dsm-Morogoro,tulipitia kituo cha mbezi na abiria wakajazwa na kurundikwa hadi kwenye varanda.
Achilia mbali wingi wa Magari yanyofanya safari za Morogoro-DSM bado abiria walikuwa ni wengi mno kiasi kwamba walikua radhi kukaa chini ya varanda.
Kila tuliposimamishwa na trafiki konda alishuka na noti ya elfu tano au elfu kumi naye trafiki hakuwa akiingia garini kusema kwamba huu ni mchezo wao wa kila siku na natumaini wengi wetu huwa tunajionea haya.
Hii inamaan ya kuwa Rushwa haiwezi kuisha leo wala kesho na ni mbaya sana kurundika abiria katika varanda hususani pale inapotokea ajali.
Mnamo saa nne kasoro tuliwasili stendi ya basi Msamvu,kwa stendi hii hongereni Manispaa ya Morogoro ni stendi kubwa na ya kisasa.
Lakini jengo lililopo ghorofani lilionekana kimya kama kwamba halitumiki,ofisi hazijakodishwa na kampuni za mabasi mengi wanakatisha tiketi zao nje kwa mawakala,halmashauri ya Morogoro ijitadthmini kwa kulazimisha makampuni kuwa na ofisi maalumu ili iweze kupata wapangaji wa ofisi zilizo tupu.
Madudu mengine ni maandishi yanayoitambulisha stendi hii KITUO CHA MABASI CHA KISASA MSAMVU,huyu mshauri aliyeyeshauri kiitwe hivyo amekosea sana,je kuna haja gani kuandika neno CHA KISASA?
Eneo la kupumzikia abiria limejaa wafanyabiashara wa vyakula na sikuweza kuona mahali salama kwangu kujipumzisha hadi alfajiri nikaamua tu nitafute Lodge ya bei poa nisije haribu bajeti yangu.
Nikatoa oda kwa bodaboda anipeleke lodge inayotoza chini ya elfu 10 kulingana na bajeti yangu,shughuli ikaja hapa kwani kila mahali chumba ni elfu kumi n tano lakini ukivitazama havina hata hadhi hiyo kabisa.
Lodge zote zimeweka vyoo vya kukaa,hivi nani kawadanganya kuwa kila mtu anapenda aina hii ya vyoo? Mwisho nikakubali lodge mojawapo baada ya kutafuta zisizo na vyoo vya kukaa bila mafanikio,ikabidi niwe naenda kutumia choo cha staff maana sipendi kabisa vyoo hivi labda kiwe changu binafsi.
Inaendelea......
View attachment 1222278