Bro haikuwa Arusha last week kwel. Maana kuna jamaa alidandia gari mara akatereza chaali doh mavumbi tu.Niliwahi taka kuruka kwenye daladala kama makondakta wanavyofanya,aisee siji sahau namna nilivyolamba lami,na ilikua mchana kweupee.
Sent from my SM-J260F using JamiiForums mobile app
Kwa mlioko Dar, Poleni kwa mgao wa kuanzia maji, umeme mpaka mapenzi, ila ndugu zangu tutafika kwa Baba tuko hoi sana maskiini, imagine duniani tunateseka hivii na bado huko naskia kuna moto tena..! Nyieeeeeeh'..!
Nisiwachoshe maana mshajichokea zenu tayari, kuna siku natoka zangu huko 'duniani' ilikuwa mida ya jioni ndiyo narudi zangu nyumbani, ile natoka getini nikakuta kuna watu wengi kweli wamekaa hapo pia wapo dereva toyo wamepaki kwa pembeni kidogo..!
Kama mnavyojua mdada ukipita mbele ya watu wengi ule ujasiri huwa unapotea tu ghafla, unatafuta cha kuzugia.! Luckily, nilikuwa niko na simu mkononi na kuna voice note ya whatsap nilikuwa nimetoka iskiza, ikabidi na mie nianze kurekodi V.N kujibu, shida hasa ilikuwa tu nivuke kwenye wale watu wengi, na venye walikuwa wananikodolea macho ndiyo nikahisi kuzimia kabisa.!
Sikupita hata hatua nyingi barabarani kwenyewe sijafika, nikaanza kuitwa na baadhi ya wale toyo 'swahiibaaa' 'swahibaaa', nikawaskia kiukweli ila nikajikausha mazima, nikaona enhee' washaanza uchokozi hawa bila shaka, maana akili zao huwa wanazijua wenyewe,
Nikaona wee' wasinizoee ndiyo kwanza nikazidi kuzidisha mashauzi na kutembea kwa pozi ili nijifanye niko serious na busy mradi tu waniache, pochi mkononi, maji yangu ya kunywa kisha nikakaza macho kwenye simu yangu nikajitia 'u-business face', dear Lord, laiti ningejua ningesimama niwaskize eti hata.! Lakini ile kiburi ya uzima itakuwa imeenda wapi sahiyo maskiini.!!
Nafika mbele kidogo, nikashangaa mbona kama hatua zangu hazizuiliwi na ile kimini tena nini kimetukia ghafla..!? Haha.! Sitaki kukumbuka ile siku walaqhi'..! Nilitamani ardhi ipasuke nidumbukie huko.! Kumbe watu wote walivyokuwa wananishangaa na toyo wananiita waniambie ni namna zipu ya mini skirt kuna namna nilikuwa imeachia huko nyuma.!
So kadri natembea na yenyewe inazidi kushuka..! Jizoooozi..! Niliishiwa pozi, uso ulinishuka na yale mashauzi yakayeyuka yooote ghafla kama siagi motoni.! Nilijikuta naweka maji chini, pochi na simu bila kujijua wala kujali tena..! Nikakamata skirt yangu nikaibana zipu haraka haraka hapo najikaza nisianguke.! Ningechelewa ningeiokotea magotini.. Haha.! Nyieeeeh'..!
Niliinua vitu vyangu ardhini bila kugeuza hata shingo kwa aibu, nikajikuta napanda daladala niliyokutana nayo ya kwanza ambayo hata haina uelekeo ninaoenda shida yangu tu ni kuondoka lile eneo, catwalk ikapotea ghafla ikawa ni mwendo wa kuruta, nimekaa kwenye daladala nikawa nahisi kama kila mtu anajua kilichotokea.!!
Ila tbh, nilijifunza kitu kikubwa sana siku ile,
anyways, nimejikuta tu nashea.!! Uliwahi aibika mbele za watu.? Ilikuwaje.?
😂😂😂😂dahh1. Wakati tupo shule sekondari nimesoma day. So mida ya jion ilikua tukitoka tunakua tumerundikana wengi sana hapo nje ya geti, wa kupanda vibasi wanapanda, na wengine mdogo mdogo kwa miguu nk. Sisi wa miguu tulikua tunapenda ikipita gari tunaikimbilia tunadandia kwa nyuma then mbele kidogo tunaruka:
Kisa a) Siku hiyo imepita pick up moja ipo speed kiasi nikaona niwaonyeshee mbwembwe wenzangu. Basi nikaanza kuikimbiza ile gari, kumbe mwenye gari nae aliniona akapania kunikomesha maana wenye magari walikua hawapendi kabisa hiyo tabia. Basi ile nakaribia kuishika bodi ya gari dereva akafunga breki ghafla! Kwa kasi niliyokua nayo nilijikuta najibamiza uso nyuma ya ile gari paa! Turu hilooo... aisee niliaibika sana watu walinicheka mnoo.. ila sikukoma
Kisa b) Siku nyingine mimi na jamaa yangu tukadandia tena gari nyingine kwa mtindo ule ule. Baada ya kudandia saa ngapi dereva hajaanza kuchochea mwendo halafu anaelekea uelekeo tofauti na tunapoenda sisi! Tukashauriana turuke hivyo hivyo. Aisee tulianguka kama mafurushi ya mahindi tukaburuzika kwenye vumbi magoti na mikono imechubuka balaa.
2. Kuna wakati nilikua nafanya kazi kwenye kaduka flani ivi. Hiyo sehemu kuna fremu nyiingi za maduka zimejipanga so watu ni wengi. Akapita mdada ana bonge la trako ila sasa nguo yake ikawa imekaa vibaya kwa nyuma. Alivaa sketi ndefu, ila transparent kabisa. Kwa ndani ilikua na kitambaa kizito, ila sasa hicho kitambaa kizito ni kama kilinasia kwenye chupi huku juu (labda wakati wa kuvaa au toilet), kwahiyo chupi, tako na mapaja yote kwa nyuma yakawa yanaonekana laivu! Mimi ki jentroman nikatoka nikawa namuita "We anti..! Dada...! Sister...!" Mwenyewe akageuka, akaniangalia, akaachia boooonge la sonyo kisha akaendelea zake kutembea kwa madaha!! Sasa watu wote wakanigeukia mimi wakawa wananicheka aisee niliaibika mnoo.. nikarudi zangu nimejikunyata kama kuku alienyeshewa na mvua.
3. Siku hiyo bana jamaa kaja na pikipiki XL 125 mtaani, kidume nimeshapewa theories jinsi ya kuendesha nikajidai naweza. Jamaa kaniuliza mara mbilimbili nikamwambia niko vizuri hivi ni vitu vidogo kwangu. Nikakamata chuma pale, piga kiki jino moja kitu kikaitika, shika klachi, vuta mafuta ya kutosha, pachika gia then nikaachia klachi kama nilivyosikia kwenye stori kijiweni. Maamaeee..! Kitu ilipaa tairi ya mbele nikayumba mara mbili ya tatu niliona vumbi tuu...
🤣🤣Tulienda kwenye harusi,muda wa kufungua champagne Mc akatangaza anataka watu nane watu hakuna nikasema ngoja niende na mimi.
Jamani wote champagne zao zilifunguka faster mimi sasa nilijikuta mwenyewe mbele watu wananiangalia na chupa haijafunguka.Niliitikisa ile chupa kama chibuku.
Mpaka kuja kufunguka watu walishachoka kuniangalia,sherehe niliiona chungu sikunyanyuka tena mpaka muda wa kuondoka.
Atakaeelewa alichoandika huyu dada naomba anifafanulie. Sijui ni balimi ndio zinanichanganya?Mimi sijawahi kwa sababu siringiagi watu so nashtuliwa mapema
Ila kuna siku nilishuka kwenye kausafir fulani na huyo niliyemfuata ndio aliniabisha mbaya.
Sijui alikuwa anat'xxxxxxxmba basi alitoka tu njee ile nahamu ya yeye kuja woi.
Siamekuja kaifungia duidu yenye mavu,,,,,,,zi kibao juu ya mkanda alivyokuwa anakuja watu walicheka hadi nikamwona nami nikaanza kucheka nika snap photo akaja nikamwonyesha akairudisha mahali usika akacheka akaona aibu sana . Ila ilikuwa raha sana .
that's too bad aiseeh'..!!Ilikuwa miaka ya 90s kama unatokea ndanda unaelekea mikoa ya Lindi na Mtwara kama km 10 Kuna kijiji kinaitwa nangoo.Daraja lilizolewa na maji wananchi wakakaa pembeni ya barabara wakisimamisha magari ili kuwapa tahadhali.Kuna gari land cruiser ya wazungu walisimamishwa sana ili wapewe tahadhali lakini walidharau huku wakiwapungia mikono wananchi...hamadi wakiwa speed waliruka katika gema la daraja na kupata ajali mbaya iliyoondoka na uhai wa wazungu wote wanne.
Hahahhaaa....1. Wakati tupo shule sekondari nimesoma day. So mida ya jion ilikua tukitoka tunakua tumerundikana wengi sana hapo nje ya geti, wa kupanda vibasi wanapanda, na wengine mdogo mdogo kwa miguu nk. Sisi wa miguu tulikua tunapenda ikipita gari tunaikimbilia tunadandia kwa nyuma then mbele kidogo tunaruka:
Kisa a) Siku hiyo imepita pick up moja ipo speed kiasi nikaona niwaonyeshee mbwembwe wenzangu. Basi nikaanza kuikimbiza ile gari, kumbe mwenye gari nae aliniona akapania kunikomesha maana wenye magari walikua hawapendi kabisa hiyo tabia. Basi ile nakaribia kuishika bodi ya gari dereva akafunga breki ghafla! Kwa kasi niliyokua nayo nilijikuta najibamiza uso nyuma ya ile gari paa! Turu hilooo... aisee niliaibika sana watu walinicheka mnoo.. ila sikukoma
Kisa b) Siku nyingine mimi na jamaa yangu tukadandia tena gari nyingine kwa mtindo ule ule. Baada ya kudandia saa ngapi dereva hajaanza kuchochea mwendo halafu anaelekea uelekeo tofauti na tunapoenda sisi! Tukashauriana turuke hivyo hivyo. Aisee tulianguka kama mafurushi ya mahindi tukaburuzika kwenye vumbi magoti na mikono imechubuka balaa.
2. Kuna wakati nilikua nafanya kazi kwenye kaduka flani ivi. Hiyo sehemu kuna fremu nyiingi za maduka zimejipanga so watu ni wengi. Akapita mdada ana bonge la trako ila sasa nguo yake ikawa imekaa vibaya kwa nyuma. Alivaa sketi ndefu, ila transparent kabisa. Kwa ndani ilikua na kitambaa kizito, ila sasa hicho kitambaa kizito ni kama kilinasia kwenye chupi huku juu (labda wakati wa kuvaa au toilet), kwahiyo chupi, tako na mapaja yote kwa nyuma yakawa yanaonekana laivu! Mimi ki jentroman nikatoka nikawa namuita "We anti..! Dada...! Sister...!" Mwenyewe akageuka, akaniangalia, akaachia boooonge la sonyo kisha akaendelea zake kutembea kwa madaha!! Sasa watu wote wakanigeukia mimi wakawa wananicheka aisee niliaibika mnoo.. nikarudi zangu nimejikunyata kama kuku alienyeshewa na mvua.
3. Siku hiyo bana jamaa kaja na pikipiki XL 125 mtaani, kidume nimeshapewa theories jinsi ya kuendesha nikajidai naweza. Jamaa kaniuliza mara mbilimbili nikamwambia niko vizuri hivi ni vitu vidogo kwangu. Nikakamata chuma pale, piga kiki jino moja kitu kikaitika, shika klachi, vuta mafuta ya kutosha, pachika gia then nikaachia klachi kama nilivyosikia kwenye stori kijiweni. Maamaeee..! Kitu ilipaa tairi ya mbele nikayumba mara mbili ya tatu niliona vumbi tuu...
Tatizo kubwa wanawake wa kibongo kila dakika alipo hasa mabinti, anawaza, K yangu hivi K yangu vile,, yaani mawazo hayaendi mbali,,Wa Africa tofauti na wanawake wa kizungu wao madem wa kizungu ukiwaita Wana kuja kukusikiliza hawa ogopi na hawana wasiwasi Kabisa
Sent using Jamii Forums mobile app
Hujui kuandika ?Mimi sijawahi kwa sababu siringiagi watu so nashtuliwa mapema
Ila kuna siku nilishuka kwenye kausafir fulani na huyo niliyemfuata ndio aliniabisha mbaya.
Sijui alikuwa anat'xxxxxxxmba basi alitoka tu njee ile nahamu ya yeye kuja woi.
Siamekuja kaifungia duidu yenye mavu,,,,,,,zi kibao juu ya mkanda alivyokuwa anakuja watu walicheka hadi nikamwona nami nikaanza kucheka nika snap photo akaja nikamwonyesha akairudisha mahali usika akacheka akaona aibu sana . Ila ilikuwa raha sana .
Sijui mwayaHujui kuandika ?
Kitaa nilichohamia nikitoka kwangu nyumba ya tatu kuingia Barbara kubwa asubuhi wa mama wapo nje wanafanya bizness zao,week ya Kwanza yote nilikua naaamkia,Kuna siku nimeamkia bwana napiga hatua tatu mbele nasikia wanasemezana kwa sauti ya chini "huyu Kaka si mtu mzima kabisa anaamkia amkia tu " hahaha NIMEBADILI NJIAHii kusalimia wamama hata mimi sipendi, unaweza jikuta umekisalimia kitoto kidogo chenye umbo kubwa.